Mfumo wa Uongozaji Safari wa BeiDou wa China utaathiri kivipi maisha ya Muafrika?

Yoyo Zhou

Member
Jun 16, 2020
68
110
d62a6059252dd42ae78a5ee43f9886b3c8eab82c.jpeg
















































China Jumanne ilirusha satilaiti ya mwisho ya Mfumo wa kuongozea wa BeiDou(BDS), ambapo inaonesha kukamilika kwa uendelezaji wa mfumo huo nchini, miaka 26 baada ya ujenzi wa BeiDou-1 kuanza rasmi mwaka 1994, na kuwa mmoja kati ya mifumo minne ya mtandao wa uongozaji duniani, ikiwa sambamba na GPS wa Marekani, GLONASS wa Russia na Galileo wa Umoja wa Ualaya.

Hivi sasa duniani kuna nchi 130 ambazo kila siku idadi ya satilaiti za Beidou zinazozunguka katika anga zake za juu nikubwa zaidi kuliko GPS, na 100 kati ya hizo ni nchi za Asia na Afrika. Satilaiti nyingine zinamaanisha usahihi na utegemezi. Basi Beidou ina uhusiano gani na mwafrika wa kawaida, na ni jinsi gani itahudumia maisha yako katika pande mbalimbali?

Kila siku baada ya kuamka, tunakunywa chai. Beidou inatumiwa sana katika mfumo wa kilimo cha kisasa. Na inawezekana kuwa mikate unayokula inatengenezwa kwa ngano iliyovunwa na magari ya kuvunia yasiyo na dereva yakiongozwa na Beidou.

Baada ya kula chakula, unapanga kwenda kazini. Kabla ya kutoka nyumbani, unaangalia utabiri wa hali ya hewa kwenye simu, na BeiDou inaweza kukupatia huduma hiyo yenye usahihi mkubwa halafu utajua leo unalazimika kubeba mwavuli au la, na hata BeiDou inaweza kutoa tahadhari ya kutokea kwa maafa na kulinda usalama na maisha yako.

Baada ya kutoka, ukipanda Daladala au Matatu, BeiDou inaweza kujua mahali pa kila gari, na ukiona kibao cha kidijitali chenye vituo, utaweza kujua basi lijalo litafika baada ya dakika ngapi. Huduma hizo tayari zimetumiwa katika miji ya Shanghai na Beijing nchini China na kiwango chake cha usahihi ni asilimia 95.

Kama ukiendesha gari binafsi, programu za kuongoza safari zinazotumia huduma za Beidou zinaweza kutusaidia kukwepa msongamano wa magari. Hali halisi ni kuwa program nyingi za ramani zilizopo katika simu zetu zinatumia mfumo wa BeiDou. Habari zinasema duniani simu milioni 700 za aina ya Android zinatumia huduma za BeiDou.

Sasa unatoka kazini na kurudi nyumbani. Baada ya kula chakula, unataka kutazama televisheni, na unapata habari moja inayohusu kulinda wanyamapori. Kwa kutumia mfumo wa BeiDou, kila mnyama pori anaweza kupandikizwa kifaa mwilini mwake cha kujua mahali pake alipo, halafu walinzi wanaweza kujua mienendo yao ili kuzuia vitendo vya ujangili.

Mbali na kutoa huduma za uongozaji safari, BeiDou pia inaweza kutoa huduma nyingine nyingi. Kwa mfano, BeiDou ina vitu maalumu ambavyo havipo kwenye GPS. Kile kinachoonekana waziwazi ni ujumbe. Watejawanaweza kutumiana ujumbe mfupi kwa satilite. Bila kujali wewe upo katika jangwa lisilo na kivuli cha mti au bahari isiyo na mpaka, BeiDou inaweza kutoa huduma za uokoaji wa maisha yako.

Kama alivyosema msanifu mkuu wa mfumo wa BeiDou Bw. Sun Jiadong, “mipaka ya matumizi ya BeiDou ni kufikiria tu.”
 
“Mipaka ya matumizi ya BeiDou ni kufikiria tu.”
-
“Mipaka ya matumizi ya akili ni kufikiria tu.”
 
Mkuu hakuna kitu cha bure hiyo huduma ya Beiduo lazima ilipiwe ili upate ile huduma standard.

Miaka ya nyuma kwenye navigation hali ikikuwa ngumu kwa kutumia nyota,jua,mwezi(Celestial Bodies). Baada ya GPS kuja watu walijua wamepata ahueni kubwa ilibidi walipie huduma.

Na baada ya tukio la ugaidi mwaka 2001 USA ilibidi aweke vizuizi kwenye matumizi ya GPS ambapo waliweka daraja la Military na Civilians use.Walifanya hivyo kujilinda na wabaya ambapo ukitumia civilian GPS kuna error kama mita kadhaa hivyo uwezi kupata target sahihi.

Hili utumie GPS halisi ambayo ni military purpose inakubidi ulipie huduma na hii waliuziwa nchi,makampuni na taasisi.

GPS ipo chini ya department of defense ya USA, jamaa walipoweka barrier hii ikawafanya jumuiya ya Ulaya na wao waanzishe Galileo, Urusi wakaja na Glonass, China wakaleta Beidou.

GPS mpaka kukava dunia nzima walitumia miaka mingi, mwanzo ilikuwa unapata GPS kwa maeneo ukiwa baharini.

Kwa sasa GPS na Glonass ndio zina cover worldwide.

Ngoja tuone Beidou kama itacover dunia nzima,ufanisi wake utakuwa vipi?
 
Huyo mkenya alichofanya hapo ni kutoa Tu matumizi ya Hizo global position system na matumizi hayo unayapata pia kwenye GPS, Glonass, Galilleo ama hata hio BEidou. Hajafanya utafiti wowote kwamba ni bora zaidi Africa.

Vyema mtu ukitaka best positioning system uhakikishe kifaa chako kina support positioning system nyingi kadri iwezekanavyo, hakuna ambayo ipo perfect.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom