BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 676
- 1,634
Mimi ni mmoja wa wateja niliyeagiza gari kutoka nje ya nchi. Gari langu limefika bandarini tangu wiki iliyopita, lakini hadi sasa halijatolewa kutokana na changamoto kubwa ya mifumo, hususan mfumo wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).
Kwa kweli hali hii inakatisha tamaa sana. Tangu mfumo huo uanze kutumika hivi karibuni, umekuwa kikwazo kikubwa kwa sisi wateja. Sipo peke yangu—tupo wengi tumekwama bandarini tukikosa huduma kwa wakati.
Ukifika bandarini, hasa katika ofisi za TBS, utakutana na msongamano mkubwa wa watu waliokwama kama mimi. Hakuna mwendelezo mzuri wa huduma, na majibu yanayotolewa hayana uwazi wala uhakika.
Kinachouma zaidi ni kwamba muda wa bure wa kuhifadhi gari bandarini unaendelea kuisha, na gharama za ziada (storage) zinaendelea kuongezeka kila siku—mzigo wote huo unaangukia kwa mteja.
Tunaomba sana mamlaka husika, hususan TBS, wachukue hatua za haraka kuboresha mfumo huu na kuhakikisha unafanya kazi kwa ufanisi. Hali ya sasa siyo rafiki kwa wafanyabiashara wala wananchi wa kawaida.
Swali letu ni moja tu—hali hii itaendelea hadi lini?”
Ufafanuzi ~ TBS: Mawakala wa Forodha na Waagizaji wa Bidhaa nchini wafuate Taratibu wakati wa kuomba kibali kupitia TANeSW
Kwa kweli hali hii inakatisha tamaa sana. Tangu mfumo huo uanze kutumika hivi karibuni, umekuwa kikwazo kikubwa kwa sisi wateja. Sipo peke yangu—tupo wengi tumekwama bandarini tukikosa huduma kwa wakati.
Ukifika bandarini, hasa katika ofisi za TBS, utakutana na msongamano mkubwa wa watu waliokwama kama mimi. Hakuna mwendelezo mzuri wa huduma, na majibu yanayotolewa hayana uwazi wala uhakika.
Kinachouma zaidi ni kwamba muda wa bure wa kuhifadhi gari bandarini unaendelea kuisha, na gharama za ziada (storage) zinaendelea kuongezeka kila siku—mzigo wote huo unaangukia kwa mteja.
Tunaomba sana mamlaka husika, hususan TBS, wachukue hatua za haraka kuboresha mfumo huu na kuhakikisha unafanya kazi kwa ufanisi. Hali ya sasa siyo rafiki kwa wafanyabiashara wala wananchi wa kawaida.
Swali letu ni moja tu—hali hii itaendelea hadi lini?”
Ufafanuzi ~ TBS: Mawakala wa Forodha na Waagizaji wa Bidhaa nchini wafuate Taratibu wakati wa kuomba kibali kupitia TANeSW