Mfumo wa 'second selection' kwa waliofaulu kidato cha kwanza ni ushamba na uharibifu wa future

Luqman mohamedy

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
892
1,226
A.alaykum wakuu,
Leo hii nimepata taarifa zilizonshtua kutoka kwa mtoto wa jirani yangu mmoja aliyehitimu darasa la saba na kufaulu kwa kiwango cha 'C'..Taarifa hii ni kwamba yeye na wahitimu wengine wenye kiwango cha ufaulu kisichokua wastani wa 'A' au 'B' watasubiri second selection ili kupangiwa shule mwezi february

Nadhani wenye kumbukumbu ama tuliopita zamani tunakumbuka huu mfumo wa second selection na adha zake ikiwa ni pamoja na;

1.Mtoto akiwasili shuleni baada ya chaguo la pili anawakuta wenzie wamesogea kimasomo kiasi flani kwahiyo inampa ugumu kwenda sambamba na wenzake.

2.Kuna baadhi watakaoahirisha masomo kabisa kwenye familia zenye wazazi wasio na msimamo wa elimu,taani wengine watakua washakabidhiwa biashara za kuisaidia familia.

3.Inamuathiri mtoto kiisaikolojia na kujiona looser na aliowakuta wamemzidi mno na hii inamtengenezea inferior state itakayomuathiri kwenye perfomance yake.

Mi nadhani huu mfumo hauna maana kama mtu ataweza kwenda shule february kwanini asipelekwe sasa hivi???
Mbona miaka kadhaa nyuma baada ya kuanzishwa shule za kata iliwezekana???
 
Shule za kata nazo ni Dili kwa sasa, hawataki kupokea watoto Mburura (Viraza) ni bora wazazi wakawapeleka Gereji watoto wao mapema.

Kufeli kwa mtoto wako darasa la saba, ni majibu dhahiri kuwa, mzazi/wazazi na mwanafunzi husika, hawana nia na malengo katika swala zima la Elimu...!
 
Mkuu unalolisema ni kweli lakini hivi unajua kama kunawatu walienda second selection na wakafanya vizuri zaidi ya wale waliochaguliwa first selection unadhani ni kwanini...sababu anaeenda second selection anakuwa na imani kuwa uwezo wake ni mdogo hivyo huwa anakomaa zaidi ili kuwafikia wale aliowakuta mwisho wa siku anatoboa anawaacha watu midomo wazi
Kwahiyo mimi sioni kama kunatatizo labda mtoto mwenyewe tu aamue kushindwa
 
Mkuu unalolisema ni kweli lakini hivi unajua kama kunawatu walienda second selection na wakafanya vizuri zaidi ya wale waliochaguliwa first selection unadhani ni kwanini...sababu anaeenda second selection anakuwa na imani kuwa uwezo wake ni mdogo hivyo huwa anakomaa zaidi ili kuwafikia wale aliowakuta mwisho wa siku anatoboa anawaacha watu midomo wazi
Kwahiyo mimi sioni kama kunatatizo labda mtoto mwenyewe tu aamue kushindwa
Kuna watu walifeli darasa la saba, wakaenda shule private, wakafanya vizuri kuliko waliofaulu.

Pia,second selection mara nyingine hutokea kwanafasi fulani kutochukuliwa.

Watu wamefaulu kwenda shule za serikali, wameamua kuacha hizo nafasi, wakaenda shule za seminary kwa mfano, nafasi ikawa wazi, shuleikaja kujua baadaye, sasa nafasi hiyo itajazwa vipi kama si kwa second selection?
 
A.alaykum wakuu,
Leo hii nimepata taarifa zilizonshtua kutoka kwa mtoto wa jirani yangu mmoja aliyehitimu darasa la saba na kufaulu kwa kiwango cha 'C'..Taarifa hii ni kwamba yeye na wahitimu wengine wenye kiwango cha ufaulu kisichokua wastani wa 'A' au 'B' watasubiri second selection ili kupangiwa shule mwezi february

Nadhani wenye kumbukumbu ama tuliopita zamani tunakumbuka huu mfumo wa second selection na adha zake ikiwa ni pamoja na;

1.Mtoto akiwasili shuleni baada ya chaguo la pili anawakuta wenzie wamesogea kimasomo kiasi flani kwahiyo inampa ugumu kwenda sambamba na wenzake.

2.Kuna baadhi watakaoahirisha masomo kabisa kwenye familia zenye wazazi wasio na msimamo wa elimu,taani wengine watakua washakabidhiwa biashara za kuisaidia familia.

3.Inamuathiri mtoto kiisaikolojia na kujiona looser na aliowakuta wamemzidi mno na hii inamtengenezea inferior state itakayomuathiri kwenye perfomance yake.

Mi nadhani huu mfumo hauna maana kama mtu ataweza kwenda shule february kwanini asipelekwe sasa hivi???
Mbona miaka kadhaa nyuma baada ya kuanzishwa shule za kata iliwezekana???
Kimsingi si vizuri mtu aliyefaulu kusubiri na kuingia shule siku kadha baada ya wenzake kuanza masomo. Kwa hilo nakubaliana na mleta mada. Kiuhalisia ni kuwa hatuna mfumo uliowekwa kulishughulikia swala hili. Tujiulize hizo nafasi huwa zinatoka wapi. Nyingi ni zile zinazo achwa na wale wanaokwenda shule binafsi na shule za dini. Serikali inapochagua form1 hata form 5 huwa wanaziweka kando shule hizi. Wazazi wakisha amua vinginevyo ndo nafasi zilizobaki hupewa wale ambao wanaufaulu lakini hawakupata awamu ya kwanza.
Naamini serikali ikiamua hili linaweza kushughulikiwa hasa kwenye enzi hizi za tehama. Wangeweza kutoa uchaguzi wao watu wakaconfirm ndani ya muda fulani na wakapanga kujaza nafasi. Washirikiane na shule binafsi na za dini katika hili na litapunguza hii kadhia.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom