Yaani labda mimi sielewi ni kwanini rambirambi, michango hata ya wafanyakazi wa serikali na ahadi zinatolewa kwa pesa za karatasi. Siku hizi kuna bank ATM, Tigo pesa, MPESA....... sasa kwanini serikali ina halalisha matumizi ya pesa kama vile makaratasi tena ukizingatia pesa zetu thamani iko chini sana. Wananchi hawawezi kuanza kutumia bank kama wanaona viongozi wa serikali wanatoa pesa za madafu kwenye kila tukio la michango.