authjeremmy
Member
- Nov 5, 2019
- 8
- 10
Salamu kwenu wote.
Jina langu ni Jeremiah Rotich, kutoka nchi ya Kenya. Ningependa kuchukua fursa hii kuwatangazia kuwa nimeanzisha shirika/ mradi linalowania kutengeneza Mfumo wa Matumizi (Operating System) kwa lugha ya Kiswahili. Wengine wenu mnaweza kuwa mnafahamu uwepo wa kilinux iliyoanzishwa mwakani 2003. Ila kwa maoni yangu, sioni ikiwa mradi huo ulitufikia sisi sote kwa maana hamna mfumo hadi sasa unaotumia lugha ya Kiswahili kwa hali msingi.
Jina la mradi ni Swahilinux na unapatikana katika wavuti hii ya Swahilinux. Tunawaomba nyote kujiunga na kundi letu kwenye Twitter, Telegram au kuchangia kwa tafsiri kwa kujiunga na jukwaa letu la Tafsiri
Mfumo utakaotokana na mradi huu utajengwa kwa msingi wa Linux (Linux Kernel) na toleo la kwanza la majaribio litatoka Desemba mwaka huu (2019).
Asanteni.
Jina langu ni Jeremiah Rotich, kutoka nchi ya Kenya. Ningependa kuchukua fursa hii kuwatangazia kuwa nimeanzisha shirika/ mradi linalowania kutengeneza Mfumo wa Matumizi (Operating System) kwa lugha ya Kiswahili. Wengine wenu mnaweza kuwa mnafahamu uwepo wa kilinux iliyoanzishwa mwakani 2003. Ila kwa maoni yangu, sioni ikiwa mradi huo ulitufikia sisi sote kwa maana hamna mfumo hadi sasa unaotumia lugha ya Kiswahili kwa hali msingi.
Jina la mradi ni Swahilinux na unapatikana katika wavuti hii ya Swahilinux. Tunawaomba nyote kujiunga na kundi letu kwenye Twitter, Telegram au kuchangia kwa tafsiri kwa kujiunga na jukwaa letu la Tafsiri
Mfumo utakaotokana na mradi huu utajengwa kwa msingi wa Linux (Linux Kernel) na toleo la kwanza la majaribio litatoka Desemba mwaka huu (2019).
Asanteni.