Wanangwa,
Jana nilikuwa kanisani, mimi ni m- KKKT, na kama mnavyojua KKKT ni moja kati ya Taasisi kubwa sana hapa Tanzania ya kidini. Sasa wakati Mzee wa kanisa anasoma matangazo kikaja kipengele cha mapato, akasoma yote kisha akasema "Baki usharikani ni Tshs kadhaa", pia akataja asilimia iliyokwenda Jimboni.
Hapo hapo nikaikumbuka hoja ya Lissu, kumbe makusanyo yote ya sadaka hayaendi moja kwa moja Jimboni (Dayosisi) bali kuna asilimia tu ndiyo inakwenda na nyingine yote inabakia usharikani kutekeeza mambo ambayo wanaona bado hawajayamaliza kwa sababu matitizo ya usharika wetu si sawa na matatizo ya sharika zingine. Kwa mfano sisi tunaweza kuwa tunahitaji kujenga nyumba ya mchungaji lakini wenzetu wa sharika nyingine wao nyumba washajenga tayari ila wanahitaji gari la kanisa ama kujenga kituo cha kulelea watoto yatima nk.
Naungana na Lissu kwamba ukitaka kujenga Taasisi yoyote imara duniani ni lazima ukaimishe madaraka ya kibajeti katika kila ngazi ya kiuongozi. Na kwa kutumia mfumo huu wa Serikali za majimbo zenye mamlaka hata rushwa itapungua sababu tukitaka kumpa mtu atujengee barabara ama shule tunamjua fika hadi nyumbani kwake na kama akituzingua basi tunamshughulikia. Sasa huu ndiyo uhuru tulioulilia mwaka 1961 toka kwa mkoloni, kuamua nini kianze na kipi kisubiri kutokana na mapato yetu wenyewe.
Kwa hiyo maamuzi ya nini kifanyike kwenye Usharika wetu hatugonji Dayosisi kutuamulia hapana TUNAAMUA WENYEWE, wao tunawajulisha tu. Mahesabu ya hela zetu tunayo wenyewe.
Hiki ndicho Lissu cha ChademaDM wanamaanisha, na tangu jana nimekuwa muumini mkubwa wa Serikali ya majimbo.
Jana nilikuwa kanisani, mimi ni m- KKKT, na kama mnavyojua KKKT ni moja kati ya Taasisi kubwa sana hapa Tanzania ya kidini. Sasa wakati Mzee wa kanisa anasoma matangazo kikaja kipengele cha mapato, akasoma yote kisha akasema "Baki usharikani ni Tshs kadhaa", pia akataja asilimia iliyokwenda Jimboni.
Hapo hapo nikaikumbuka hoja ya Lissu, kumbe makusanyo yote ya sadaka hayaendi moja kwa moja Jimboni (Dayosisi) bali kuna asilimia tu ndiyo inakwenda na nyingine yote inabakia usharikani kutekeeza mambo ambayo wanaona bado hawajayamaliza kwa sababu matitizo ya usharika wetu si sawa na matatizo ya sharika zingine. Kwa mfano sisi tunaweza kuwa tunahitaji kujenga nyumba ya mchungaji lakini wenzetu wa sharika nyingine wao nyumba washajenga tayari ila wanahitaji gari la kanisa ama kujenga kituo cha kulelea watoto yatima nk.
Naungana na Lissu kwamba ukitaka kujenga Taasisi yoyote imara duniani ni lazima ukaimishe madaraka ya kibajeti katika kila ngazi ya kiuongozi. Na kwa kutumia mfumo huu wa Serikali za majimbo zenye mamlaka hata rushwa itapungua sababu tukitaka kumpa mtu atujengee barabara ama shule tunamjua fika hadi nyumbani kwake na kama akituzingua basi tunamshughulikia. Sasa huu ndiyo uhuru tulioulilia mwaka 1961 toka kwa mkoloni, kuamua nini kianze na kipi kisubiri kutokana na mapato yetu wenyewe.
Kwa hiyo maamuzi ya nini kifanyike kwenye Usharika wetu hatugonji Dayosisi kutuamulia hapana TUNAAMUA WENYEWE, wao tunawajulisha tu. Mahesabu ya hela zetu tunayo wenyewe.
Hiki ndicho Lissu cha ChademaDM wanamaanisha, na tangu jana nimekuwa muumini mkubwa wa Serikali ya majimbo.