Mfumo wa maisha ya wanawake wengi hapa Tanzania

Ulongupanjala

JF-Expert Member
Apr 9, 2013
7,659
12,279
Wadau hamjambo?

Nimekuwa nifuatilia kwa karibu mfumo mzima wa maisha ya wanawake wengi hapa Tz hasa wale wanaojiita wa kisasa.

WIGI NA KUWEKA DAWA NYWELE.
Wanawake kwa wasichana wengi wameathirika na mfumo wa kuvaa WIGI na kuweka nywele dawa,madhara yake ni makubwa na mara kadhaa nimeshuhudia wanawake hao wakilalamika kuumwa vichwa kutokana na mizigo ya mawigi iliyo vichwani mwao au kuuguza maumivu yaliyotokana na kuchomwa na mashine za kukaushia nywele pindi wanapoweka dawa.

Huwa najiuiza hizi ni baadhi ya athari za moja kwa moja,vipi kuhusu athari nyingine ambazo huchukua muda kuonekana??

Kama Mungu amekuumba mzuri amini nakuambia hata ukinyoa KIPARA bado utaoneka kuwa mzuri lakini sio kuweka mizigo kichwani inayokunyima raha na kuugulia maumivu makali.

Wengine hata kuwapa haki zao za NDOA waume zao inakuwa SHIDA kwa kuogopa kuharibu nywele zao FEKI.Jiamini mtoto wa kike..!

Kesho nitaendelea na mfumo wa uvaaji wa visuruali vya kubana A.K.A Skin tight unaoleta madhara makubwa kwa wanawake/wasichana wa nchi hii ambao ni mabingwa wa kuiga kila kitu..Tuombe uzima..!
 
ila wengine tunaficha siri za vichwa na wigs vichwa kama wema na upara si tutakosa darlz
 
sawa...ila kwa kweli mambo mengine ni unkwepabo kwa kweli. mwanamke ameumbiwa urembo babu..
 
mnh waja leo waondoka leo huyu,haya wasalimie mlalo sijui sitimbi loool
 
Shida ya wanawake wengi,wanatafuta uzuri wa dukani.Siku hizi wanawake wengi mmeongeza hitaji muhimu la kuwa na wigi au nywele bandia kichwani.Ndio maana mpaka bi..ra bandia mnauziwa.Hamtaki vitu genuine..!!


sawa...ila kwa kweli mambo mengine ni unkwepabo kwa kweli. mwanamke ameumbiwa urembo babu..
 
Mkuu hutaki wake zetu wapendeze?...wakizeeka wataacha for wacha waendelee tu
 
Shida ya wanawake wengi,wanatafuta uzuri wa dukani.Siku hizi wanawake wengi mmeongeza hitaji muhimu la kuwa na wigi au nywele bandia kichwani.Ndio maana mpaka bi..ra bandia mnauziwa.Hamtaki vitu genuine..!!
kwan mtu akiweka mnywele bandia ambayo ameinunua kwa hela yake wewe anakukera nini best? usitake watu waishi kama unavyotaka wewe..
 
kwan mtu akiweka mnywele bandia ambayo ameinunua kwa hela yake wewe anakukera nini best? usitake watu waishi kama unavyotaka wewe..

Insu sio hela yake au ya kuhongwa. Ni madhara yanayotokana na hivi vitu vya kuigaiga inafikia mwanamke akivua wigi utafikiri mchawi jinsi alivoharibika kuanzia nywele zake hadi ngozi ya kichwa! hivi huwa hamjiulizi utaendelea kuvaa wigi mpaka lini?! na sio mawigi tu na wengine wengi wanatumia vitu ambavyo ni hatari sana kwa afya zao, mf; vipodozi vyenye kemikali hatari na huku anajua vimekatazwa! Kila siku kansa zinazidi kuongezeka kisa? unataka kuwa mzuri kama nyau! ------- kabisa!
 
Insu sio hela yake au ya kuhongwa. Ni madhara yanayotokana na hivi vitu vya kuigaiga inafikia mwanamke akivua wigi utafikiri mchawi jinsi alivoharibika kuanzia nywele zake hadi ngozi ya kichwa! hivi huwa hamjiulizi utaendelea kuvaa wigi mpaka lini?! na sio mawigi tu na wengine wengi wanatumia vitu ambavyo ni hatari sana kwa afya zao, mf; vipodozi vyenye kemikali hatari na huku anajua vimekatazwa! Kila siku kansa zinazidi kuongezeka kisa? unataka kuwa mzuri kama nyau! ------- kabisa!

kwani nyau ni mzuri?
 
Insu sio hela yake au ya kuhongwa. Ni madhara yanayotokana na hivi vitu vya kuigaiga inafikia mwanamke akivua wigi utafikiri mchawi jinsi alivoharibika kuanzia nywele zake hadi ngozi ya kichwa! hivi huwa hamjiulizi utaendelea kuvaa wigi mpaka lini?! na sio mawigi tu na wengine wengi wanatumia vitu ambavyo ni hatari sana kwa afya zao, mf; vipodozi vyenye kemikali hatari na huku anajua vimekatazwa! Kila siku kansa zinazidi kuongezeka kisa? unataka kuwa mzuri kama nyau! ------- kabisa!

Pamoja na yote hayo bado ndio wanaoishi muda mrefu kweli kuna Mungu!
 
Insu sio hela yake au ya kuhongwa. Ni madhara yanayotokana na hivi vitu vya kuigaiga inafikia mwanamke akivua wigi utafikiri mchawi jinsi alivoharibika kuanzia nywele zake hadi ngozi ya kichwa! hivi huwa hamjiulizi utaendelea kuvaa wigi mpaka lini?! na sio mawigi tu na wengine wengi wanatumia vitu ambavyo ni hatari sana kwa afya zao, mf; vipodozi vyenye kemikali hatari na huku anajua vimekatazwa! Kila siku kansa zinazidi kuongezeka kisa? unataka kuwa mzuri kama nyau! ------- kabisa!

My waifu wangu anajua akiweka yale sijui ni kama katani zilizotiwa masizi , tunapeana likizo kwa sababu wakati wa kujianda kuingia uwanjani mimi huwa ninapenda kushikashika nywele za my waifu sio nishike makatani yenye mzsizi for this case HAVAI YALE MADUDE ANAOGOPA LIKIZO. hata hivyo ninampenda sana na nikigusa nywele zake ninajisikia burdani kuu..............kumbe hayo madude ndo mnayaita wigii !!!!!!
 
Nani kakudanganya kuwa kupendeza kwa mwanamke kuko kwenye kuvaa WIGI na kuweka nywele DAWA,akipata kansa ya UBONGO,una pesa za kumtibia India? Au unataka akipata tatizo umtelekeze? Ndio maana siku hizi wanawake wengi wana stress zisizo na sababu na ni za kudumu..!!!


Mkuu hutaki wake zetu wapendeze?...wakizeeka wataacha for wacha waendelee tu
 
Back
Top Bottom