Kilamuluzi
Senior Member
- May 20, 2014
- 116
- 20
Habari ndugu wana jamvi,
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sana juu ya uendeshaji wa hii serikali yetu juu ya matumizi ya vyombo vya umma kama ni halali ama hapana!
Nianze na hivi vichache;mfano mtu anateuliwa kuwa waziri,je,ni lazima apewe nyumba ya kuishi na serikali?ni lazima ahudumiwe gharama za chakula,kusomesha watoto wake shule na serikali?kama ni sawa kuna sababu gani za kumlipa mshahara mtu anaehudumiwa na serikali namna hii?
Ndugu zangu naombeni mnisaidie kama haya ni matumizi sahihi ya kodi zetu kwa viongozi tulionao,na kama sio sahihi ni kwa nini tusibadili mfumo wa kuendesha serikali yetu?
Mfano mzuri upo hapa Rwanda,wakati waziri anateuliwa kuwa waziri alikuwa kwenye nyumba yake,hivyo serikali haiwajibiki kumpatia nyumba nyingine ataendelea kutumia hiyo hiyo aliyokuwa nayo kabla hajawa waziri.
Kingine matumizi ya magari ya serikali ni wakati wa kazi tu,baada ya hapo gari zote za serikali zinalala yadi ya serikali hakuna gari inalala nje ya hii yadi labda kwa kibali maalumu.
Kuna mambo mengi ambayo tunahitaji kuyabadilisha ili tuweze kuongozwa vizuri na hawa viongozi wetu bila kuathiri au kugharimu pesa nyingi za mlipa kodi wa Tanzania.
Tafadhali naomba mchango wako wa mawazo juu ya hii kadhia iliyopo hapa nchini kwetu Tanzania.
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sana juu ya uendeshaji wa hii serikali yetu juu ya matumizi ya vyombo vya umma kama ni halali ama hapana!
Nianze na hivi vichache;mfano mtu anateuliwa kuwa waziri,je,ni lazima apewe nyumba ya kuishi na serikali?ni lazima ahudumiwe gharama za chakula,kusomesha watoto wake shule na serikali?kama ni sawa kuna sababu gani za kumlipa mshahara mtu anaehudumiwa na serikali namna hii?
Ndugu zangu naombeni mnisaidie kama haya ni matumizi sahihi ya kodi zetu kwa viongozi tulionao,na kama sio sahihi ni kwa nini tusibadili mfumo wa kuendesha serikali yetu?
Mfano mzuri upo hapa Rwanda,wakati waziri anateuliwa kuwa waziri alikuwa kwenye nyumba yake,hivyo serikali haiwajibiki kumpatia nyumba nyingine ataendelea kutumia hiyo hiyo aliyokuwa nayo kabla hajawa waziri.
Kingine matumizi ya magari ya serikali ni wakati wa kazi tu,baada ya hapo gari zote za serikali zinalala yadi ya serikali hakuna gari inalala nje ya hii yadi labda kwa kibali maalumu.
Kuna mambo mengi ambayo tunahitaji kuyabadilisha ili tuweze kuongozwa vizuri na hawa viongozi wetu bila kuathiri au kugharimu pesa nyingi za mlipa kodi wa Tanzania.
Tafadhali naomba mchango wako wa mawazo juu ya hii kadhia iliyopo hapa nchini kwetu Tanzania.