Salaam WanaJambo wenzangu. Habari ya wikendi?? Sasa leo nimepita pale kwenye "www.issamichuzi.blogspot.com" nikakutana na habari hapo chini kuhusu sheria ya ajira ya serikali ya mwaka 2002. Najua ni sheria na imepitishwa na Bunge lakini kwa mawazo yangu machanga naona sheria hii sio muafaka kwa nchi changa (kimaendeleo na sio kiutawala) kama Tanzania. Naomba wenzangu mnipanue mawazo lakini mimi naona yafuatayo yatakuwa ni matatizo yake:
1. Ufanisi wa idara na wizara utakuwa mdogo kutokana na watu kuwa ni walewale - damu mpya yenye fikra mpya
2. Watu ambao wapo nje ya serikali na wao qualified hawataweza kuingia katika nafasi ambazo zinawahusu na badala yake itabidi waingie chini na kupanda ngazi. Serikali sio jeshi na sheria hii itakatisha tamaa wale walio nje ya serikali/nchi kurudi na kujenga taifa lao. Hapa kuna utata ukizingatia kuwa Serikali ya JK inajitahidi ku "support" vita dhidi ya "talent/manpower poaching by the developed world".
3. Hii itasababisha kusiwe na ushindani ndani ya serikali sababu wengi watajua kuwa wao wapo ndani na cheo kikitokea ni chetu - hakuna "external competition". Na hii vilevile inaweza kupelekea baadhi ya maofisa/senior people kuwa "discourage technically" vijana/watu wapya kwenye idara/wizara na hivyo kujihakikishia kuwa "Kingdom come I will be in power and get all comming posts/promotions"
4. Last but not least, nafasi hizi ni za uteuzi. Hapa bwana tutarudisha yaleyale ya kupeana lawama. Wote tunajua kuwa hata uteuzi wa Raisi lazima apelekewe majina, sasa ni criteria gani itatumika kwenye kufanya "vetting" ya candidates? Urafiki/undugu (ambao wote tunajua utachukua nafasi ya juu), ukabila (haupo lakini nadhani tutaurudisha kwa mtaji huu), malipo "in kind" (hii wote tunajua inategemea nani anaweza kutufichia madhambi yetu)??
Kwa maoni yangu hii sheria ni kwa ajili ya kuwalinda/kujilinda wale tulio ndani bila kufukiria wale walio kwenye sekta binafsi na zaidi wale walio nje ya nchi!!! Yeyote aliyefikiria kitu kama hiki na kukataa kuweka "free competition" nadhani hajui kuwa tuendako ni mambo ya ushindani na "uchetu" na sio "umimi" na "usisi"!!!!!
Naomba kuwakilisha...
Mfumo mpya wa ajira serikalini
Na Pascal Mayalla
Serikali haitaajiri watumishi wa umma wa kuanzia ngazi za maofisa waandamizi, bali sasa nafasi za kazi katika ngazi hizo, zitakuwa ni za uteuzi na zitagawiwa kwa watu wenye sifa walio ndani ya utumishi wa umma kinyume na ule utaratibu wa kuzitangaza kwa ushindani wa uwazi kwa kila mtanzania mwenye sifa kuwa na haki ya kuomba.
Uamuzi huo, umetangawa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bibi Hawa Ghasia, katika hafla ya kumuaga Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji msataafu, Lameck Mfalila, makamishina wa tume hiyo na wafanyakazi waliostaafu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Waziri Ghasia emesema, uamuzi huo wa serikali, unafuatia mabadiliko ya Sheria ya Utumishi Namba 7 ya Mwaka 2002, yaliyofanywa na Bunge hivi katika kipengele cha ajira katika utumishi wa umma kwa ngazi za maofisa waandamizi sasa sio za ushindani wa wazi.
Waziri Ghasia amesema, lengo la mabadiliko hayo ni kuipunguzia serikali mzigo wa kuendesha mafunzo ya mara kwa mara kwa maofisa wanaoajiriwa toka nje ya serikali, na kusisitiza kuwapandisha vyeo maofisa wa serikali wenye sifa na utendaji wao unajulikana kutaleta tija zaidi kuliko kuajiri watanzania wenye sifa ambao utendaji wao haujulikani.
Hata hivyo Waziri Ghasia amesema uamuzi huo hauna maana kuwa watanzania wenye sifa walio nje ya serikali sasa hawana nafasi tena katika uongozi wa utumishi wa umma, ila bado watanzania wenye sifa wataendelea kuajira katika utumishi wa umma pale ambapo hakutakuwa na watumishi wa umma wenye sifa zinazotakiwa.
Naye Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bibi Thecla Shangali, amewasisitizia watumishi wa umma kuzingatia taratibu sheria na kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ili utendaji wa serikali upate mafanikio yaliyokusudiwa na kuleta tija kwa maendeleo ya taifa.
Mwenyekiti mstaafu wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu, Lameck Mfalila, amesema anajivunia sifa ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa tume hiyo iliyoundwa mwaka 2002 na mafanikio makubwa ya tume hiyo iliyoyapata katika kipindi kifupi ambapo ni pamoja na kubadilisha sura na mitazamo ya watumishi wa umma toka utumishi wa zamani ambao ni utumishii tuu mpaka sasa kwenye utumishi wa umma unazingatia matokeo huku ukifanya kazi kibiashara kwa kufuata kanuni za mikataba ya huduma kwa wateja.
Jumla ya makamishna watano wa tume hiyo ewamestaafu na mwenyekiti wao sambamba na wafanyakazi 3 wa tume hiyo akiwemo, Naibu Katibu wa tume hiyo, Bibi Prisilla Ole Kambainei.
Mwisho wa kunukuu
1. Ufanisi wa idara na wizara utakuwa mdogo kutokana na watu kuwa ni walewale - damu mpya yenye fikra mpya
2. Watu ambao wapo nje ya serikali na wao qualified hawataweza kuingia katika nafasi ambazo zinawahusu na badala yake itabidi waingie chini na kupanda ngazi. Serikali sio jeshi na sheria hii itakatisha tamaa wale walio nje ya serikali/nchi kurudi na kujenga taifa lao. Hapa kuna utata ukizingatia kuwa Serikali ya JK inajitahidi ku "support" vita dhidi ya "talent/manpower poaching by the developed world".
3. Hii itasababisha kusiwe na ushindani ndani ya serikali sababu wengi watajua kuwa wao wapo ndani na cheo kikitokea ni chetu - hakuna "external competition". Na hii vilevile inaweza kupelekea baadhi ya maofisa/senior people kuwa "discourage technically" vijana/watu wapya kwenye idara/wizara na hivyo kujihakikishia kuwa "Kingdom come I will be in power and get all comming posts/promotions"
4. Last but not least, nafasi hizi ni za uteuzi. Hapa bwana tutarudisha yaleyale ya kupeana lawama. Wote tunajua kuwa hata uteuzi wa Raisi lazima apelekewe majina, sasa ni criteria gani itatumika kwenye kufanya "vetting" ya candidates? Urafiki/undugu (ambao wote tunajua utachukua nafasi ya juu), ukabila (haupo lakini nadhani tutaurudisha kwa mtaji huu), malipo "in kind" (hii wote tunajua inategemea nani anaweza kutufichia madhambi yetu)??
Kwa maoni yangu hii sheria ni kwa ajili ya kuwalinda/kujilinda wale tulio ndani bila kufukiria wale walio kwenye sekta binafsi na zaidi wale walio nje ya nchi!!! Yeyote aliyefikiria kitu kama hiki na kukataa kuweka "free competition" nadhani hajui kuwa tuendako ni mambo ya ushindani na "uchetu" na sio "umimi" na "usisi"!!!!!
Naomba kuwakilisha...
Mfumo mpya wa ajira serikalini
Na Pascal Mayalla
Serikali haitaajiri watumishi wa umma wa kuanzia ngazi za maofisa waandamizi, bali sasa nafasi za kazi katika ngazi hizo, zitakuwa ni za uteuzi na zitagawiwa kwa watu wenye sifa walio ndani ya utumishi wa umma kinyume na ule utaratibu wa kuzitangaza kwa ushindani wa uwazi kwa kila mtanzania mwenye sifa kuwa na haki ya kuomba.
Uamuzi huo, umetangawa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bibi Hawa Ghasia, katika hafla ya kumuaga Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji msataafu, Lameck Mfalila, makamishina wa tume hiyo na wafanyakazi waliostaafu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Waziri Ghasia emesema, uamuzi huo wa serikali, unafuatia mabadiliko ya Sheria ya Utumishi Namba 7 ya Mwaka 2002, yaliyofanywa na Bunge hivi katika kipengele cha ajira katika utumishi wa umma kwa ngazi za maofisa waandamizi sasa sio za ushindani wa wazi.
Waziri Ghasia amesema, lengo la mabadiliko hayo ni kuipunguzia serikali mzigo wa kuendesha mafunzo ya mara kwa mara kwa maofisa wanaoajiriwa toka nje ya serikali, na kusisitiza kuwapandisha vyeo maofisa wa serikali wenye sifa na utendaji wao unajulikana kutaleta tija zaidi kuliko kuajiri watanzania wenye sifa ambao utendaji wao haujulikani.
Hata hivyo Waziri Ghasia amesema uamuzi huo hauna maana kuwa watanzania wenye sifa walio nje ya serikali sasa hawana nafasi tena katika uongozi wa utumishi wa umma, ila bado watanzania wenye sifa wataendelea kuajira katika utumishi wa umma pale ambapo hakutakuwa na watumishi wa umma wenye sifa zinazotakiwa.
Naye Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bibi Thecla Shangali, amewasisitizia watumishi wa umma kuzingatia taratibu sheria na kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ili utendaji wa serikali upate mafanikio yaliyokusudiwa na kuleta tija kwa maendeleo ya taifa.
Mwenyekiti mstaafu wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu, Lameck Mfalila, amesema anajivunia sifa ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa tume hiyo iliyoundwa mwaka 2002 na mafanikio makubwa ya tume hiyo iliyoyapata katika kipindi kifupi ambapo ni pamoja na kubadilisha sura na mitazamo ya watumishi wa umma toka utumishi wa zamani ambao ni utumishii tuu mpaka sasa kwenye utumishi wa umma unazingatia matokeo huku ukifanya kazi kibiashara kwa kufuata kanuni za mikataba ya huduma kwa wateja.
Jumla ya makamishna watano wa tume hiyo ewamestaafu na mwenyekiti wao sambamba na wafanyakazi 3 wa tume hiyo akiwemo, Naibu Katibu wa tume hiyo, Bibi Prisilla Ole Kambainei.
Mwisho wa kunukuu