Mfululizo wa Kesi ya Ugaidi iliyokuwa ikimkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake watatu

Analia na kusema Baba uwasamehe Makonda na Sabaya kikosi kazi changu cha mauaji naomba uwabadilishe wapate kutubu kwa sababu hatukujua kuwa kuna mateso namna hii.
Mbinguni hakuna mateso!! ..wachungaji fake wamekudanganya!!!....Makonda hateseki anakula Bata South paleee Lady Brand,...hujui! ila unaendeshwa na roho za visasi!
 
Mbinguni hakuna mateso!! ..wachungaji fake wamekudanganya!!!....Makonda hateseki anakula Bata South paleee Lady Brand,...hujui! ila unaendeshwa na roho za visasi!
Kuna mbinguni au jehanum ukifa hapa duniani kuna mambo mawili ukifa mchafu unaenda jehanum na ukifa mtakatifu unaenda mbinguni.
 
Kuna mbinguni au jehanum ukifa hapa duniani kuna mambo mawili ukifa mchafu unaenda jehanum na ukifa mtakatifu unaenda mbinguni.
Safi sana kumbe una akili!.....kaenda mbinguni umesha kiri kwa kinywa chako Ndo inavotakiwa....na Mbinguni hakuna Ukigeu geu!......ukisema ameenda mbinguni una maanisha ivo!! safi sana!...MOTO UKO JEHANUMU TU!
 
Safi sana kumbe una akili!.....kaenda mbinguni umesha kiri kwa kinywa chako Ndo inavotakiwa....na Mbinguni hakuna Ukigeu geu!......ukisema ameenda mbinguni una maanisha ivo!! safi sana!...MOTO UKO JEHANUMU TU!
Wewe mjinga tu unataka tumkufuru Mungu kwa vile nimekuona wewe ni kichaa na umenikuta naoga bafuni umekwapua nguo zangu siwezi endelea kukufukuzia maana utanifanya na mimi niendelee kuwa kichaa,na kichaa wako hana namna huko aliko alijifanya Mungu akaabudiwa na wajinga kama wewe lakini utiukufu wake ukapotea mara moja kwa vile yupo MUNGU MMOJA TU na si mwizi wa kura na muuaji.
 

Historia ya kesi ya Mbowe na Wenzake

Freeman Akamatwa Mwanza 21Julai 2021

Mnamo tarehe 21 Julai mwaka 2021, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza lilimtia nguvuni Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa akiwa hoteli ya Kingdom mtaa wa Ghana alikokifikia, alipokuwa ameenda kwenye ziara za shughuli za chama chao. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ramadhani Ng'anzi alithibitisha kumshikilia kiongozi huyo.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alishikiliwa kwa mahojiano baada ya kukamatwa akidaiwa kutaka kuendesha Kongamano la Katiba ambalo awali lilikuwa limezuiwa na Polisi.

"Baada ya kumkamata, wenzetu wa Dar es Salaam nao walitueleza kuwa wanamtafuta kwa makosa mengine anayodaiwa kuyafanya huko; hivyo tulimsafirisha kwenda Dar es Salaam anakoendelea kuhojiwa," alisema Kamanda Ng'anzi.

Pia, soma: Polisi: Mbowe amepelekwa Dar kwa Mahojiano, atarejeshwa Mwanza


Freeman Mbowe Atuhumiwa kwa Kupanga njama za Ugaidi na Kudhuru viongozi wa Serikali 22 Julai 2021
Mwekiti wa CHADEMA alisafirishwa moaka Dar Es Salaam ambapo alifikishwa kituo Kikuu cha Polisi na kisha kupelekwa nyumbani kwake ambapo baadhi ya vifaa vyake kama laptop, tablet za watoto wake na modem vilichukuliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi, naye aliambiwa ataunganishwa pamoja na watuhumiwa wengine wa Ugaidi.

Pia, soma: Freeman Mbowe atuhumiwa kwa Ugaidi na kupanga njama za Kuua Viongozi wa Serikali


Kuhusu kilichotokea katika Kesi Mahakamani, fungua viungo (LINKS) hapo chini:

SEPTEMBA, 2021
- Mahakama ya Uhujumu Uchumi: Mvutano mkali kesi ya Mbowe na wenzake. Hatma ya kesi kujulikana Septemba 6 (03/09/2021)

- Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi ACP Ramadhani Kingai afunguka upande wa Jamhuri (15/09/2021)

- Naibu Msajili Mahakama ya Uhujumu aainisha masharti ya kusikiliza kesi ya Mbowe (16/09/2021)

- Kesi ya Mbowe na Wenzake: Polisi Wazuia watu kuingia kufuatilia, Mawakili wa Utetezi watoka nje. Kesi yarejea na kuahirishwa mpaka 17 Sept (19/09/2021)

- Yaliyojiri kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi - Sept 17, 2021 (17/09/2021)

- Yaliyojiri kesi ya Mbowe na Wenzake: Upande wa Mashtaka waendelea kutoa ushahidi. Kesi yaahirishwa mpaka Septemba 24, 2021 (20/09/2021)

- Mahakama yatupilia mbali Kesi ya Mbowe ya Kikatiba dhidi ya IGP, DPP na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (23/09/2021)

- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi - 27/09/2021 (27/09/2021)

- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa - 28/09/2021 (28/09/2021)

- Maamuzi ya kesi ndogo katika Kesi ya Mbowe na Wenzake kutolewa Oktoba 19, 2021 (29/09/2021)


OKTOBA, 2021
- Kesi ndogo ya Mbowe iliyopangwa kutolewa hukumu tarehe 19/10/2021 yasogezwa mbele (17/10/2021)

- Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake Watatu kuendelea tena tarehe 26/10/2021 (25/10/2021)

- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe: RPC Kingai aeleza Mbowe alivyopanga kumdhuru Ole Sabaya. Kesi yaahirishwa hadi 27 Oktoba 2021 26/10/2021

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake. Shahidi Justine Eliya Kaaya, amtaja Ole Sabaya. Kesi imeahirishwa hadi Oktoba 28, 2021 27/10/2021

- Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe na wenzake: Kaaya amaliza kutoa ushahidi. Shauri kuendelea 29/10/2021 28/10/2021

- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu, Coplo Hafidh Abdallah Mohamed atoa ushahidi wake, kesi kuendelea Jumatatu 01 November 2021 29/10/2021

NOVEMBA, 2021

- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na rushwa. Shauri kuendelea kesho Nov, 2, 2021 (01/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Mbowe na Wenzake: Shahidi Afred Kapala wa tiGO atoa Ushahidi, Kesi kuendelea, Nov 03, 2021 (02/11/2021)

- Yaliyojiri kesi ya Mbowe leo Novemba 3, 2021: Shahidi Upande wa Mashitaka ashindwa kutokea Mahakamani, kesi yaahirishwa hadi Novemba 4, 2021 (03/11/2021)

- Kesi ya Mbowe Novemba 4, 2021: Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi, Sebastian Madembwe atoa ushahidi. Kesi yaahirishwa hadi Novemba 5, 2021 (04/11/2021)

- Yaliyojiri kesi ya Mbowe leo Novemba 05, 2021: Inspector Mahita Mohamed atoa ushahidi (05/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu kesi ya Mbowe na wenzake. Superitendent Jumanne Malangahe atoa ushahidi, Kesi imeahirishwa hadi Nov 9, 2021 (08/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi kwenye kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake, kesi imeahirishwa hadi - Nov 10, 2021 (09/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu kesi ndogo ya Mbowe, Superitendent Jumanne Malangahe atoa Ushahidi (10/11/2021)

- Kesi ndogo ya Freeman Mbowe: Shahidi akamilisha ushahidi wake, Shahidi mwingine kuendelea tarehe 12/11/2021 (11/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe na wenzake, kesi imeahirishwa mpaka 15, Nov 2021 (12/11/2021)

- Yaliyojiri kesi ya Freeman Mbowe na wenzake, kesi imeahirishwa mpaka 16, Nov 2021 (15/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe: Jaji aahirisha kutoa uamuzi mpaka tarehe 17/11/2021 saa tatu asubuhi (16/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 17, 2021: Kesi yaahirishwa mpaka tarehe 18/11/2021 saa tatu asubuhi] (17/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 18, 2021. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 22, 2021 (18/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Novemba 22, 2021. Mahakama yatupilia mbali hoja tatu za utetezi. Kesi imeahirishwa hadi Novemba 23, 2021 (22/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Detective Afande Goodluck atoa Ushahidi, Kesi yaahirishwa hadi Novemba 24, 2021 (23/11/2021)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe -Inspector Lugawa ISSA Maulid atoa Ushahidi, Kesi yaahirishwa hadi Novemba 25, 2021 (24/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Upande wa Utetezi waanza kutoa ushahidi. Kesi yaahirishwa mpaka 26 Novemba, 2021 (25/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, kesi ya Mbowe na wenzake 3 - Kesi imeahirishwa hadi Nov. 29 2021 (26/11/2021)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu divisheni ya Makosa ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, kesi ya Mbowe na wenzake - 30 Nov 2021 (30/11/2021)


DESEMBA, 2021
- Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na wenzake - Desemba 1, 2021. Shahidi asimulia alivyowekwa chumba cha mateso gerezani. Uamuzi kusomwa Desemba 14, 2021 (Dec 1, 2021)

- Mahakama yatupilia mbali mapingamizi ya utetezi, maelezo ya Mohamed Lingw'enya yapokelewa na Mahakama. Kesi kuu kuendelea Des. 15, 2021 (Dec 14,2021)

- Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeman Mbowe (CHADEMA) na wenzake watatu yaahirishwa mpaka Januari 10, 2022 (Dec 20, 2021)


JANUARI, 2022
- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe - Januari 10, 2022. Shahidi namba 8 aendelea kutoa ushahidi. Kesi imeahirishwa hadi kesho 11/01/2022 (Jan 10, 2022)

- Yaliyojiri katika kesi ya Freeman Mbowe leo Januari 11, 2022. SP Jumanne Malangahe amaliza kutoa ushahidi. Kesi yaahirishwa hadi Januari 13, 2022 (Jan 11, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani katika kesi ya Freeman Mbowe na wenzake, Januari 13, 2022. Kesi imeahirishwa hadi Januari 14 2022 (Jan 13, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake watatu. Kesi imeahirishwa hadi 17, January 2022 (Jan 14, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake watatu. Kesi imeahirishwa hadi Januari 18, 2022 (Jan 17, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kwenye Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Kesi yaahirishwa hadi 19/01/2022 (Jan 18, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Freeamn Mbowe na wenzake watatu - Januari 19, 2022 (Jan 19, 2022)

- Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe na Wenzake leo 20/01/2022. Shahidi 10 amaliza, shahidi wa 11 mwingine kuanza ushahidi kesho 21/01/2022 (Jan 20, 2022)

- Yaliyojiri katika kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na Wenzake tarehe21/01/2021. Kesi imeahirishwa hadi 24/ 01/ 2022 (Jan 21, 2022)

- Yaliyojiri kesi ya Mbowe 24/01/2022: Shahidi wa 11, H4347 Goodluck amaliza ushahidi wake. Shahidi wa 12 kuendelea tarehe 26/01/2022 (Jan 24, 2022)

- Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake (Jan 26, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi ya Mbowe na wenzake: Luteni Denis Urio, Shahidi wa 12 anaendelea kutoa Ushahidi wake (Jan 27, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake. Shahidi wa 12 Luteni Urio kuendelea kutoa ushahidi Januari 31, 2022 (Jan 28, 2022)

- Yaliyojiri Mahakama Kuu Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi Februari 01, 2022 (Jan 31, 2022)


FEBRUARI, 2022
- Yaliyojiri kesi ya Mbowe 01/02/2022. Luteni Denis Urio amaliza kutoa ushahidi wake. Shahidi wa 13 kuanza 04/02/2022 (Feb 1, 2022)

- Yaliyojiri kesi inayomkabili Mbowe na wenzake leo Februari 4, 2022. Kesi imeahirishwa. Shahidi wa 13 kuendelea kutoa ushahidi Februari 7, 2022 (Feb 4, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 08/2022 (Feb 7, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 9, 2022 (Feb 8, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022 (Feb 9, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake 3: Shahidi Tumaini Swila ashindwa kufika mahakamani. Kesi imeahirishwa hadi Februari 14, 2022 (Feb 10, 2022)

- Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake 3. Shahidi wa 13, Tumaini Swila kuendelea kutoa ushahidi Februari 15, 2022 (Feb 14, 2022)

- Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe na Wenzake. Tumaini Swila amaliza ushahidi. Mawikili wa Serikali wafunga Ushahidi. Jaji kutoa uamuzi 18/02/2022 (Feb 15, 2022)

- Mbowe na Wenzake 3 wakutwa na kesi ya kujibu. Kesi imeahirishwa hadi Machi 4, 2022. Watuhumiwa kuanza kujitetea (Feb 18, 2022)


MACHI, 2022
- Mbowe aachiwa huru na wenzake watatu baada ya DPP kuwasilisha hati ya kutotaka kuendelea na kesi (March, 4, 2022)
Asante sana kwa team
 
Pia, sheria zilizotumika wakati wa kesi, kuanzia ile ya Ugaidi, Forensic, PGO, Evidence, na nyingine zitawafungua macho wanasheria wetu waweze kutambua nini kinahitajika pale wakili anapokuwa anatimiza majukumu yake mahakamani akiwa kama afisa wa mahakama, hasa kwenye kuchambua vifungu husika.
hii ndio imetufundisha PGO
 
Hii ndio sticky itakayokuwa na manufaa kwa muda wote, fundisho lililotokana na hii kesi kuanzia majaji kununuliwa kwa kupewa vyeo, haki za watuhumiwa kupigwa teke na polisi, polisi kutojua vifungu vya sheria ya PGO licha ya kuwa ndio muongozo wa majukumu yao ya kila siku, ni baadhi ya mambo ambayo yatakuwa funzo kwa vizazi vijavyo Tanzania.

Zaidi, wanafunzi wa sheria watakuwa na uwanja mpana wa kujifunza kwa vitendo sheria, mfano; maswali yaliyokuwa yakiulizwa na mawakili wa pande zote mbili hasa upande wa utetezi, mfano: kuwaondoa kwenye reli mashahidi wa mchongo wa jamhuri waliokuwa wamekaririshwa majibu vitawafungua akili mawakili na wanafunzi wa sheria.

Pia, sheria zilizotumika wakati wa kesi, kuanzia ile ya Ugaidi, Forensic, PGO, Evidence, na nyingine zitawafungua macho wanasheria wetu waweze kutambua nini kinahitajika pale wakili anapokuwa anatimiza majukumu yake mahakamani akiwa kama afisa wa mahakama, hasa kwenye kuchambua vifungu husika.

All in all, ujasiri wa Mbowe kama mwenyekiti wa Chadema umekuja kuacha alama itakayodumu vizazi na vizazi hapa Tanzania kama mpigania mabadiliko aliyekuwa haogopi chochote provided anaamini anachopigania kilikuwa sahihi, hakuogopa CCM, polisi, mahakama, wala gereza wakati akiongoza mapambano yake.
Hii kesi itakuwa ya mfani na imekinda heshima ya Mwenyekiti kwa miaka 1000 ijayo
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom