Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,156
- 4,510
Mtuhumiwa amekamatwa akiwa Jijini Dar es Salaam alikokimbilia
Mkewe ambaye ni Mwalimu wa Sekondari ya Kirenyi Arusha amelazwa Hospitali ya Selian Arusha kwa matibabu
Madaktari wanasema anaendelea vema japo Kiganja cha Mkono wake wa kulia kimetengana na viungo vingine vya mwili
Mungu amponye na ampe wepesi
===
Mfanyakazi wa shirika la umeme Tanesco jijini Dar es salaam Ombeni Alfayo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kitendo kukata mkono mkewe na kusababisha kiganja Cha mkono wa kulia kutengana na sehemu nyingine ya mkono.
Akiongeza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Arusha ACP Salum Hamduni Alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya Saa 5:45 asubuhi maeneo ya siwandeti ,Iliopo kata ya Kiranyi Tarafa ya Enaboishu wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha Ambapo alimkata mke wake Veronica Kidemi (30) mmasai na mwalimu wa shule ya sekondari Kiranyi na mkazi wa siwandeti ambapo alimjeruhi kwa kumkata na kitu chenye ncha Kali katika mikono yake miwili.
Alisema kuwa uchunguzi unaendelea Ili kubaini chanzo Cha tukio hilo ingawa taarifa za awali zinasema kuwa chanzo Ni wivu wa kimapenzi ,ambapo aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo alikimbia Mara Baada ya kufanya tukio hilo na tayari ameshakamatwa katika jiji la Dar es salaam Mara Baada ya upelelezi kukamilika na atafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria aidha pia majeruhi amelazwa katika hospital ya selian-ngaramtoni.
Akiongelea tukio hilo mwalimu huyo Veronica Kidemi Alisema kuwa mume wake huyo alikuwa anamtishia Mara kwa Mara ,na alikuwa akimpiga Mara kwa Mara na inatokana na wivu alionao mume wake.
“Aliniita kutokea kazini nikaenda nilipotoka nikamkuta amejificha jikoni ndio akaanza kunikimbiza na kunikatakata mapanga hapa unapoona mkono unaniuma huu mmoja na huu mungine nimewekewa chuma ” Veronica
Kwa upande wake daktari bigwa wa mifupa wa hospital Seliani Robert Julius amethibitisha kumpokea akiwa anavuja damu nyingi na wakaanza kumpatia matibabu na kwa sasa anaendelea vizuri.
Mkewe ambaye ni Mwalimu wa Sekondari ya Kirenyi Arusha amelazwa Hospitali ya Selian Arusha kwa matibabu
Madaktari wanasema anaendelea vema japo Kiganja cha Mkono wake wa kulia kimetengana na viungo vingine vya mwili
Mungu amponye na ampe wepesi
===
Mfanyakazi wa shirika la umeme Tanesco jijini Dar es salaam Ombeni Alfayo anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kitendo kukata mkono mkewe na kusababisha kiganja Cha mkono wa kulia kutengana na sehemu nyingine ya mkono.
Akiongeza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Arusha ACP Salum Hamduni Alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya Saa 5:45 asubuhi maeneo ya siwandeti ,Iliopo kata ya Kiranyi Tarafa ya Enaboishu wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha Ambapo alimkata mke wake Veronica Kidemi (30) mmasai na mwalimu wa shule ya sekondari Kiranyi na mkazi wa siwandeti ambapo alimjeruhi kwa kumkata na kitu chenye ncha Kali katika mikono yake miwili.
Alisema kuwa uchunguzi unaendelea Ili kubaini chanzo Cha tukio hilo ingawa taarifa za awali zinasema kuwa chanzo Ni wivu wa kimapenzi ,ambapo aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo alikimbia Mara Baada ya kufanya tukio hilo na tayari ameshakamatwa katika jiji la Dar es salaam Mara Baada ya upelelezi kukamilika na atafikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria aidha pia majeruhi amelazwa katika hospital ya selian-ngaramtoni.
Akiongelea tukio hilo mwalimu huyo Veronica Kidemi Alisema kuwa mume wake huyo alikuwa anamtishia Mara kwa Mara ,na alikuwa akimpiga Mara kwa Mara na inatokana na wivu alionao mume wake.
“Aliniita kutokea kazini nikaenda nilipotoka nikamkuta amejificha jikoni ndio akaanza kunikimbiza na kunikatakata mapanga hapa unapoona mkono unaniuma huu mmoja na huu mungine nimewekewa chuma ” Veronica
Kwa upande wake daktari bigwa wa mifupa wa hospital Seliani Robert Julius amethibitisha kumpokea akiwa anavuja damu nyingi na wakaanza kumpatia matibabu na kwa sasa anaendelea vizuri.