Mfanyakazi wa ndani yatima, amenusurika kifo kwa kunywa sumu kwa mateso

BASHADA

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
513
148
Wana JF, naomba ushauri wenu huyu binti niliye naye story yake inasikitisha sana, mpaka wakati mwingine inaniliza.

Kama mjuavyo maisha yetu haya ya Mr & Mrs kuwahi maofisini lazima utafute msichana wa kazi. Kwa kuanzia, mke wangu alitafuta msichana ambaye ni ndugu kwa upande wa kwao lakini tumeona ni pasua kichwa. Baadaye tukaamua kutafuta binti mwingine kupitia kwa ndugu wengine. Kuna dada akatuambia yeye ana wasichana wawili, kwa hiyo kama tuko tayari atatupatia mmoja, na kwa kweli tulishukuru, huyo binti akaletwa.

Ili kujua undani wake nikapeleleza maisha yake ili nisije nikauziwa mbuzi kwenye gunia. Katika kupiga naye story, nikagundua kuna maswali nikimuuliza, especially kuhusu familia yake binti akawa hanipi majibu, na kwa baadhi ya maswali aliishia kulia tuu. Nikaona ngoja nimuache nifanye upelelezi kwa namna nyingine. Nikampigia huyo dada aliyekuwa naye, na baadaye nikatafuta namba ya simu ya mtu aliyemuunganisha na huyo dada. Kwa sababu huyo mtu (pia ni relative wetu) anakaa jirani na familia ya binti, nikajua nitapata data kamili. Na niligundua mambo yafuatayo;
  1. Binti aliacha shule akiwa form two na sasa alitakiwa kuwa form three (off course hili hata binti mwenyewe aliniambia.
  2. Binti hana wazazi wote wawili, japo yeye hajui hilo. Wazazi wake walifariki yeye akiwa mdogo sana, hivyo alikabidhiwa kwa ndugu mwingine wa kike (bila shaka ni mama mdogo). Binti amekua akijua yule ndiye mama yake mpaka leo anajua hivyo.
  3. Binti kila akimwuliza huyo mama kuhusu alipo baba yake, huishia kupigwa, matusi na vitisho vingine.
  4. Binti aliachishwa shule na mama yake na kuishia kufanyishwa kila aina ya kazi (ilikuwa ni mateso). Kwa sababu ya hayo mateso, binti alishawahi kunywa sumu ili afe, lakini aliwahiwa matibabu na akapona.
  5. Mama huyo yuko na mwanaume mwingine (baba wa kambo wa binti) ambaye alikuwa hajali maisha ya binti.
  6. Binti alipoona mateso yanazidi pale nyumbani aliamua kutoroka, ndipo alipofika kwa huyo dada ambaye ameamua kumforward kwangu.

Majuma machache tangu binti afike kwangu, huyo mama akapata namba zake, akamwambia arudi nyumbani kwa sababu shuleni wanamsumbua anatakiwa arudi shule (kwa kuanzia alaikuwa anatumia lugha nzuri). Nikachukua jukumu la kufanya tena research kujua undani wa hilo jambo, na kama ni kweli nilikuwa tayari kumrudisha. Ikumbukwe kuwa binti wakati anawasiliana na mama alidanganya alipo. alitaja mkoa mwingine wa mbali kabisa kumbe yeye yuko kwingine.

Utafiti wangu ukabaini kuwa hakuna cha shule wala nini, kwa sababu hata wadogo zake na binti pia walishaachishwa shule na ni mwendo wa kazi za nyumbani kwa kwenda mbele. Binti alipoona vile akamwambia ataenda lakini siyo haraka hivyo. Mama akakasirika na kuanza kuporomosha matusi ya ajabu ambayo siwezi kuyaandika hapa. Mwisho wa story, akaaga kwa maneno haya "Nahesabu kuwa umekufa, Bwana alitoa na Bwana ametoa, Jina la Bwana na libarikiwe. Nisikuone ukija kwangu kwa mema au kwa mabaya, ikiwa ni kwa uzima au ni kwa kifo, huyo uliye naye atajua kila kitu"

Huyo mama ametuma sms nyingi za vitisho na laana, lakini binti anasema mbona hayo siyo matusi, ni cha mtoto ukilinganisha na matusi aliyokuwa anapewa na mateso siku za nyuma. Binti ameapa hatorudi tena. Yuko much more comfortable kukaa kwangu, anapenda sana watoto, ni mchapa kazi mpaka utafurahi. Changamoto mbele yangu naomba ushauri wa mambo yafuatayo;
  • Analilia kwenda shule ndiyo njozi yake kuu. Na mimi natamani aende shule lakini uwezo si mkubwa kivile. Ningependa aende shule ambayo iko serious kidogo, sitaki st. Kayumba, ila hizo shule ambazo walau atatoka vizuri ziko expensive and i may not afford now. Naweza kumhakikishia uniform za shule, pocket money, chakula na matibabu. Lakini ada kwa sasa sitaweza, naomba ushauri wenu nifanyeje? maana asiposoma hana amani.
  • Pili, ishu ya wazazi wake kuwa walifariki tena kwa ugonjwa huu wa sasa (ngoma), lakini yeye alifanyiwa check up na dada aliyemchukua hana tatizo (yuko salama). Sometimes binti ana wasiwasi kama yule ni mama yake kwa jinsi anavyomtreat.
  • Please, changamoto ni nyingi naomba ushauri wenu nimsaidiaje huyu binti? Especially shule, angepatikana mtu au taasisi itakayoweza kumlipia ada, hizo gharama zingine ningempatia, maana ananichukulia kama mzazi/mlezi wake na amesema hatathubutu kuondoka kwangu.
 
Ni binti wa umri gani? Kusoma pia ni kipaji, unahisi anakipaji cha kusoma? Kama unamuona yupo kawaida tu ni bora aende VETA ila shule anaweza kupoteza mda kama umri umeenda na ukizingatia ni mschana
 
Ni binti wa umri gani? Kusoma pia ni kipaji, unahisi anakipaji cha kusoma? Kama unamuona yupo kawaida tu ni bora aende VETA ila shule anaweza kupoteza mda kama umri umeenda na ukizingatia ni mschana

utafiti, she is 17 yrs now. Ana determinations sana ya kusoma, ujue kwa sababu anajua hali yake kimaisha, na wadogo zake wanavyohangaika anatamani siku moja ukurasa wa maisha yake ubadilike. Na ninavyomwona sidhani kama atathubutu kuchezea chance ikitokea. Hata option ya VETA pia nimeshafikiria bado napima the best option for her.
 
Last edited by a moderator:
Huyo bosi wake apigwe kisu cha ------ au anyongwe.au ni matasa hayo nini!..loading error...
 
^^
Kuna mambo katika Maisha inabidi tuyafanye hata kama si kwa kikombe kilichojaa!
Mpeleke shule hata kama unaiita ya st Kayumba, ni mahali atakapojichanganya na kujisahaulisha misongo ya mawazo inayomwandama.
Fanya kwa ajili ya Mungu.
(Ikiwa tu nimeelewa vema)
^^
 
utafiti, she is 17 yrs now. Ana determinations sana ya kusoma, ujue kwa sababu anajua hali yake kimaisha, na wadogo zake wanavyohangaika anatamani siku moja ukurasa wa maisha yake ubadilike. Na ninavyomwona sidhani kama atathubutu kuchezea chance ikitokea. Hata option ya VETA pia nimeshafikiria bado napima the best option for her.
Namuomba niishi nae baada ya muda nitamsomesha...
 
pole yake binti jaribu kuuliza uliza taasisi unaweza pata msaada pia jaribu kenton high school huwa wanatoa punguzo kwa yatima ni akiwa na vithibitisho anaweza kusoma bure kabisaaaa
muhimu mwambie asiwe na haraka fatilia taratibu huku ukimpa moyo
 
Mpeleke veta angalau apate taaluma yeyote atakayo penda ss kwao ndo wameshamkataa mungu akuepushie baya ila kama binadam likitokea itakuwaje ni bora ikiwezekana uchukue maelezo yk ht kwa mwenyekiti ili badae usisumbuliwe na mm mdg wake
 
Namuomba niishi nae baada ya muda nitamsomesha...

Evelyn Salt, Samahani kwa sasa sifikirii hilo, ninachohitaji ni kuona anapata faraja ya maisha yake na kutimiza ndoto zake. Hata mimi napenda kukaa naye kwanza ndipo nimsomeshe, lakini umri unasonga. Hicho ambacho wewe unamhitaji ndo mimi pia nakihitaji. Samahani
 
Last edited by a moderator:
Nenda ukaongee na Kipingu mwenye shule ya Lord Baden Powell mnaweza gawana majukumu.... Kuna watu uwa anawasaidia sana...
 
BASHADA,

I wish you all the best in assisting this girl! Mungu akutangulie wewe na familia yako katika kutafuta jinsi nzuri ya kumsaidia.

I once did some consultancy work in Tanga visiting certain public secondary schools... I met quite some cases of similar nature, pitiful sites of orphans (mostly because of HIV/AIDS), some very very young, starving and abandoned by relatives.. yearning for a helping hand to pursue education... walking a long distance to school, torn uniforms.. starving yet taking care of their siblings.. I could write a thousand pages on their plight.. Ilikuwa inasikitisha sana sana... I did what I could from the little I had to pay for some of them especially those in Form IV who had failed to pay fees for National Examinations... I didn't know them and they didn't' know me but we 'connected' in Ulimwengu wa Roho...

WanaJamii, Lend out a helping hand whenever you can, it goes a thousand miles to heal broken souls!!!

PP
 
Pole sana,ht mm ninae wa dizain hiyo lkn wangu amekuwa specific. Anataka asome QT miaka miwili kisha ajiunge veta kusomea ufundi cherehani,nipo nasubiri mwanangu achangamke kidogo ndio nimfanyie taratibu za hiyo QT ambayo mara nyingi huwa ni evening school. Kiukweli ananilelea mwanangu vzr na ana nidham sn hivyo ht sioni shida kumsaidia kwsbb ht yy anaonesha anaonesha ana moyo wa kujifunza.
Napenda kutoa wito pia kwa familia zilizo na wasichana wasaidizi,tuwapende na tuwathamini kwani wao ndio hukaa na familia zetu na watoto wetu kwa muda mrefu tofauti na sie wenyewe,hivyo ukimpenda na kumjali ni vigumu ht kukutesea watoto au kufanya jambi baya nyumbani kwako.
 
Ni binti wa umri gani? Kusoma pia ni kipaji, unahisi anakipaji cha kusoma? Kama unamuona yupo kawaida tu ni bora aende VETA ila shule anaweza kupoteza mda kama umri umeenda na ukizingatia ni mschana

Umenena vema mkuu, hiyo option itamsaidia kuweza kutimiza mambo yote mawili kwa wakati mmoja, namaanisha kusoma na kusaidia majukumu ya nyumbani kwa sababu VETA most of them sio full time.

Hii itampa kupata faraja ya kuwepo nyumbani na wakati huohuo kufurahia mwanzo mpya wa maisha ya kujifunza kitu kwenye maisha yake.
 
utafiti, she is 17 yrs now. Ana determinations sana ya kusoma, ujue kwa sababu anajua hali yake kimaisha, na wadogo zake wanavyohangaika anatamani siku moja ukurasa wa maisha yake ubadilike. Na ninavyomwona sidhani kama atathubutu kuchezea chance ikitokea. Hata option ya VETA pia nimeshafikiria bado napima the best option for her.

Mtoto wakike hanazamana shekh
 
Last edited by a moderator:
Touching. Very touching. Na the good thing ni kuwa penye nia pana njia. Good luck mkuu.
 
Huyo mama ni gaidi sana aisee...eti "nakuhesabia umeshakufa...bwana ametoa na bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe"... hii kali aisee
 
Back
Top Bottom