Ndibalema
JF-Expert Member
- Apr 26, 2008
- 10,956
- 4,648
Mtu mmoja aliyejulika kwa jina la Ritha Mrema (48) mkazi wa njiro amefariki dunia mara baada ya kupigwa risasi na mfanyakazi wake wa ndani katika paji la uso.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi wa mkoani hapa Basilio Matei wakati akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa tukio hilo lilitokea June 17 majira ya usiku katika eneo la Njiro Block F ambapo ambapo mtuhumiwa Omary Ally (18) alimpiga risasi tajiri yake ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Njiro.
Kamanda amesema kuwa wakati walipokuwa wakimuhoji mtuhumiwa alisema kuwa ilikuwa ni majira ya usiku katika nyumbani kwao walisikia kishindo cha wezi wakivunja ili kuaingia ndani, ndipo marehemu akaignia ndani na kuchukua bastola na kumpa mfanyakazi wake huyo wa ndani aitumie.
Alisema kuwa mara baada ya kukabithiwa kijana huyo wakati alipokuwa ana jiandaa kwa ajili ya kukabiliana na wezi hao ndipo alipo jikuta amempiga tajiri yake .
"kijana huyu alikuwa hajui kutumia silaha. Sasa mara baada ya kukabidhiwa na tajiri bastola hiyo wakati akiikoki badala ya kuwageuzia wale wezi alikosea na kumgeuzia tajiri yake na kumpiga katika paji la uso"alisema Kamanda Matei.
Basilio alisema kuwa wakati tukio hilo likitokea mume wa marehemu alikuwa hayupo na ilisemekana kuwa alikuwa amesafiri kibiashara kwenda nje ya nchi na alimuachia mkewe silaha hiyo kwa ajili kujilinda. Alisema kumuachia mtu silaha unayomiliki kihalali ni kinyume cha sheria ya umiliki wa silaha kutokana na mwanamke huyo kutokuwa na ujuzi pamoja na leseni ya kutumia silaha hiyo.
Aidha kamanda alisema mtuhumiwa mpaka sasa anashikiliwa na jeshi la polisi hadi hapo uchunguzi utakapo kamilika na kufikishwa mahakamani kwa ajili ya kujibu shitaka, bila shaka la kuua bila kukusudia
SOURCE: MICHUZI BLOGSPOT.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kamanda wa polisi wa mkoani hapa Basilio Matei wakati akiongea na waandishi wa habari alisema kuwa tukio hilo lilitokea June 17 majira ya usiku katika eneo la Njiro Block F ambapo ambapo mtuhumiwa Omary Ally (18) alimpiga risasi tajiri yake ambaye ni mwalimu wa shule ya msingi Njiro.
Kamanda amesema kuwa wakati walipokuwa wakimuhoji mtuhumiwa alisema kuwa ilikuwa ni majira ya usiku katika nyumbani kwao walisikia kishindo cha wezi wakivunja ili kuaingia ndani, ndipo marehemu akaignia ndani na kuchukua bastola na kumpa mfanyakazi wake huyo wa ndani aitumie.
Alisema kuwa mara baada ya kukabithiwa kijana huyo wakati alipokuwa ana jiandaa kwa ajili ya kukabiliana na wezi hao ndipo alipo jikuta amempiga tajiri yake .
"kijana huyu alikuwa hajui kutumia silaha. Sasa mara baada ya kukabidhiwa na tajiri bastola hiyo wakati akiikoki badala ya kuwageuzia wale wezi alikosea na kumgeuzia tajiri yake na kumpiga katika paji la uso"alisema Kamanda Matei.
Basilio alisema kuwa wakati tukio hilo likitokea mume wa marehemu alikuwa hayupo na ilisemekana kuwa alikuwa amesafiri kibiashara kwenda nje ya nchi na alimuachia mkewe silaha hiyo kwa ajili kujilinda. Alisema kumuachia mtu silaha unayomiliki kihalali ni kinyume cha sheria ya umiliki wa silaha kutokana na mwanamke huyo kutokuwa na ujuzi pamoja na leseni ya kutumia silaha hiyo.
Aidha kamanda alisema mtuhumiwa mpaka sasa anashikiliwa na jeshi la polisi hadi hapo uchunguzi utakapo kamilika na kufikishwa mahakamani kwa ajili ya kujibu shitaka, bila shaka la kuua bila kukusudia
SOURCE: MICHUZI BLOGSPOT.