Mfanyakazi Geita Gold anyanyaswa kijinsia na Bosi?

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
Na Yusuf Aboud

ADELINA John Katunzi, hataweza kusahau na kusamehe mzungu David Human, ndani ya mgodi wa dhahabu wa GGM (Geita Gold Mine).

Anashikilia kuwa mzungu huyo alitumbukiza mkono ndani ya chupi yake na kugusa uke wake kwenye lango la kutokea mgodini humo, wilayani Geita.

Adelina alifukuzwa kazi wiki mbili toka afanyiwe operesheni kutokana na ugonjwa wa apendiksi (kidole tumbo). Operesheni ilifanyiwa hospitali ya Mwananchi jijini Mwanza.

Akijua hajajaza fomu za kudai mafao yake kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF), Adelina alikataa kurudisha kitambulisho cha kazi, ili awe anakitumia kuingia mgodini kufuatilia madai yake.

Ilikuwa katika kukurukakara za kutaka arejeshe kitambulisho, mkuu wa ulinzi, David Human aliishiwa subira, kwani angeweza kungoja mlinzi wa kike aje kumpekua Adelina.

Badala yake alitumbukiza mkono sehemu nyeti za mwanamke huyo kwa madai ya kutafuta kitambulisho, "kitendo kilichofanya nilie kwa sauti huku walinzi watatu wa lango kuu wakishuhudia," anasimulia Adelina.

Katika ushahidi wake mahakamani, unaoendana na ule wa mashahidi wengine watatu (walinzi) wa upande wa mashitaka, Adelina anadai alisukumwa na kubanwa kwenye ukuta, akakamatwa mikono, na Human akatumbukiza mkono kwenye chupi yake na kugusa sehemu zake nyeti.

Lakini polisi, katika maelezo yaliyosomwa mahakamani walidai kuwa Human alikamata "makalio, matiti na uke" wa Adelina. Mtetereko huu unasadikiwa kuathiri sana kesi hiyo.

Katika hukumu yake ya tarehe 18 Agosti 2008, hakimu Zabron M. Kesase wa mahakama ya wilaya Geita, anasema "...ni shahidi wa kwanza (Adelina) anayepaswa kulaumiwa kwa kusababisha yote haya."

Hakimu Kesase alisema katika hukumu, "Angekuwa (Adelina) amerejesha kitambulisho kwa wakubwa zake, yote haya yasingetokea. Hivyo namwona mshitakiwa hana hatia na namwachia huru."

Katika kesi hiyo Na. 147 ya 2007 hakimu ananukuu hati ya mashitaka inayosema mshitakiwa alimshika Adelina matiti, makalio na sehemu nyeti.

Hakimu anajenga hoja kwenye tofauti za kauli ya hati ya mashitaka na ushahidi uliotolewa mahakamani, kwamba hakuna hata mmoja, hata Adelina mwenyewe, aliyesema mshitakiwa alishika makalio au matiti ya Adelina.

Haikufahamika iwapo polisi waliandika kwa makusudi, hati ya mashitaka inayotofautiana na madai ya Adelina ili kujenga mashaka yawezayo kumsaidia mshitakiwa.

Adelina alifukuzwa kazi tarehe 5 Machi 2007. Barua ya kumfukuza ilisainiwa na Meneja Mark Jackson wa kampuni ya ATS ambayo inatoa huduma za chakula mgodini. Ingawa Adelina alikuwa analipwa na ATS, vitambulisho vyote vya wafanyakazi mgodini ni vya GGM.

Sababu za kumfukuza zinaelezwa kuwa ni "kampuni kukosa imani" naye. Basi.
"...unafahamishwa kwamba uongozi umeamua kukatisha mkataba wako wa ajira kuanzia leo tarehe 17/02/2007 baada ya kukosa imani na wewe kwenye kazi yako…" anaeleza Jackson.

Barua ilimtaka Adelina kurudisha vifaa vyote vya kampuni alivyokabidhiwa na kuahidiwa kulipwa haki zake anazostahili.

Adelina anakiri alirudisha vifaa vyote vya kampuni isipokua kitambulisho. "Nilikataa kurudisha kitambulisho kwa sababu nilikuwa nawadai mafao yangu kutoka mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF).

"Na pale mgodini huwezi kuingia bila kitambulisho; nilijua watanizuia kuingia kwa kuwa nawadai," anaeleza.

Baada ya Adelina kugoma kutoa kitambulisho, meneja Mark Jackson, anadaiwa kuwaamrisha walinzi watatu waliokuwa kwenye lango kuu wachukue kitambulisho kwa nguvu.

Walinzi hao, Richard Maganga, Niclaus Misenya na Amos Makongoro walikataa kutii amri ya Jackson kwa madai kuwa angekaguliwa na kushughulikiwa na mlinzi wa kike na siyo wao wanaume.

Kilichofuata ni Jackson kupiga simu kwa mkuu wa walinzi, David Human na Adelina akazuiwa kutoka nje ya lango.

Adelina anasimulia, "Alipokuja David akaniuliza, ‘wewe ndiye Adelina John?' Nikamjibu ndiye mimi. Akaniambia kwa ukali, ‘lete kitambulisho.' Nikamwambia siwapi mpaka mnilipe haki zangu zote."

Adelina anasema, wakati huo alikuwa ameweka kitambulisho kwenye matiti; ndipo alikihamisha na kukitumbukiza kwenye chupi kwa mbele.

"Alipoona nimeweka kitambulisho kwenye chupi akanikamata na kutumbukiza mkono; alishindwa kukitoa kitambulisho badala yake akanishika ukeni," anasimulia Adelina huku chozi likitiririka kutoka jicho lake la kulia.

Purukushani hizi ziliishia pale Adelina alipokubali kuingia kwenye gari la mgodi na kwenda moja kwa moja hadi ofisi ya mwanasheria wa GGM akiongozana na Human na meneja wa ATS.

Adelina anasema mwanasheria alimsihi akabidhi kitambulisho, pendekezo ambalo alikubali, lakini akamfafanulia kuwa anaweza kumshitaki aliyemwingiza mkono katika sehemu za nyeti.

Kwa mwaka wa nne sasa, mwanamke huyu mwenye umri wa miaka 31, mtariki na mwenye watoto wawili, hajalipwa mafao yake.

Richard Maganga, mmoja wa mashahidi upande wa mashitaka na ambaye ushahidi wake ulifanana kabisa na ule wa Adelina, naye tayari amefukuzwa kazi tangu mwaka 2008. Alikuwa amefanya kazi ya ulinzi mgodini kwa miaka minane.

Ingawa alikuwa mlinzi, barua yake ya kufukuzwa ilimhusisha Maganga na wizi wa mafuta ya mashine/mtambo wa kunyanyulia mizigo.

"David alitulazimisha mimi na wenzangu wawili tumnyang'anye Adelina kitambulisho chake, lakini tulikataa," anaeleza Maganga nakukana tuhuma za wizi akihoji, "Kama ni wizi si wangenipeleka mahakamani?"

"Sasa Adelina alipopeleka kesi mahakamani nilitoa ushahidi kama nilivyoshuhudia. Ushahidi wangu ulizingatia kilichotendeka kama Adelina alivyoeleza. Bila shaka hilo ndilo lilinifukuzisha kazi," anasema Maganga.

Kama ilivyo kwa Adelina na Maganga, ndivyo ilivyo kwa Emmanuel Lesilwa. Alianza kazi 2004. Aliachishwa kazi 16/05/2008.

Anadai alifanyiwa operesheni ya apendiksi mwaka 2007, katika hospitali ya Mwananchi iliyoko mjini Mwanza, ambayo ndiyo inatibu wafanyakazi wa mgodi wa GGM.

Aliporudi kazini meneja wake, Felix Adolf alimwabia utendaji wake umeshuka na akamwachisha kazi hata kabla kidonda cha operesheni kupona.

Usalama kazini ni mdogo. Sababu za kufukuzwa au kuachishwa kazi ni dhaifu. Uelewa wa wafanyakazi jinsi ya kujitetea, kulinda na kupigania haki zao ni haba.

Source: MwanaHalisi
 
Hawa wezi wa dhahabu zetu na bado wanatudhalilisha hivi ngeleja husikii haya manyanyaso kwa wananchi au umeridhika na bahasha??
 
uandishi mwingine ni wa hovyo sana..
sasa chupi imeingiaje hapo.????
na hiyo headline ya chupo ya adelina,really?????
 
Kuna manyanyaso mengi sana kwenye sector ya madini..Hilo swala la job security ni halipo kabisa. Unaweza fukuzwa kama kuku!! Huyo David Human nadhani ni Kaburu, na kaburu ubabe/Wizi ndo vitendo vyao..kazi hawajui zaidi ya kufck machines in the plant.

Nampa pole huyo dada...ila natumai haki yake atapata tu ni ucheleweshwaji au kuna mambo yapo nyuma ya pazia (huenda ana deni na kampuni etc)
 
HII HABARI NI YA LINI? NA HII KESI NI YA LINI? Mbona kama haieleweki na ina maelezo mengi ya kujirudiarudia ambayo yanaribu radha na mtiririko mzuri wa point
 
Sioni kosa la Mzungu hapo

Nilipoona Hii Comment yako mkuu, mpaka machozi yamenitoka.

Mi si mwandishi mzuri, Lakini huwa kuna wakt natamani nikutane na rais nimuulize hili swali.. "KWA NINI UMEAMUA KUIUZA NCHI YETU KWA WAGENI, NCHI AMBAYO BABA WA TAIFA AMEPAMBANA VILIVYO KUIPA UHURU?"

Nahisi kuna watu wanaokaa mbali na migodi wanashangaa hali hii kutokea lakini mtu aliyeandika story nimependa sana.

Hili tukio wakt linatokea mi nilikuwepo live. Na haya matukio huku kwetu yamezoeleka kabisa. Wazungu wanafanya kila wanachotaka na hakuna wa kubisha.

Wengine wanafanya haya halafu wanakwambia nenda mahakamni kama unaona umeonewa. Ni kama wafanyakazi wa migodini ni watumwa ndani ya nchi yao. Ukienda mahakamni nako Hakimu either ataomba rushwa ama ataanza kuiskiliza kesi yako huko mtaani ili ajue ni jinsi gani atapata pesa kutoka kwa hao wazungu. Ukitaka kufanya kazi kwa amani inabidi uwe mnafiki kwa wazungu ndo uatishi kwa raha mstarehe. Kuna matukio mengi ya kutisha ambayo kama nikamua kuyaeleza hapa yote kila mtu hatisoma hii thread kwa kuwa nimmengi mno.

Wazungu wanatufanya sie kama vifaa vya kazi na si binadamu.

Kuna Boss wangu ni mzungu mgeni amabaye alikuwa kama na miaka miwili tu hapa Tz. Lakini alikuwa anawasimulia wafanyakazi wenzangu kuwa.." Hapa TZ ukitaka kuishi kwa amani inabidi uwe na pesa halafu uelwane na wahindi basi.. in Tanznia there is no law. If you have money and good communication with Indian you get VISA and you live comfotably even if its the whole family of yours. Juzi watanzania wenzetu wamefia mgodini chini ya ardhi lakini wanaokuja kufanya uchunguzi ni wazungu wenzao, wataalam wa nchi yetu mko wapi.

Mheshimiwa Slaa baba uko wapi. Njoo huku migodini angalau uongee na watanzania uone wanvyoteseka.
Ahh yaani nchi inakatisha tamaa. Sasa hivi watanzania wanfukuzwa kazi kwa visingizio vya wizi halafu wanakwambia nenda kokote maana hata rais wako anajua.

Wakishakufukuza wanaleta Makaburu kushikilia nafasi hizi.

HOWEVER HII STORY YA ADELINA NADHANI HATA TAMWA WANAITAMBUA.
 
Nilipoona Hii Comment yako mkuu, mpaka machozi yamenitoka.

Mi si mwandishi mzuri, Lakini huwa kuna wakt natamani nikutane na rais nimuulize hili swali.. "KWA NINI UMEAMUA KUIUZA NCHI YETU KWA WAGENI, NCHI AMBAYO BABA WA TAIFA AMEPAMBANA VILIVYO KUIPA UHURU?"

Nahisi kuna watu wanaokaa mbali na migodi wanashangaa hali hii kutokea lakini mtu aliyeandika story nimependa sana.

Hili tukio wakt linatokea mi nilikuwepo live. Na haya matukio huku kwetu yamezoeleka kabisa. Wazungu wanafanya kila wanachotaka na hakuna wa kubisha.

Wengine wanafanya haya halafu wanakwambia nenda mahakamni kama unaona umeonewa. Ni kama wafanyakazi wa migodini ni watumwa ndani ya nchi yao. Ukienda mahakamni nako Hakimu either ataomba rushwa ama ataanza kuiskiliza kesi yako huko mtaani ili ajue ni jinsi gani atapata pesa kutoka kwa hao wazungu. Ukitaka kufanya kazi kwa amani inabidi uwe mnafiki kwa wazungu ndo uatishi kwa raha mstarehe. Kuna matukio mengi ya kutisha ambayo kama nikamua kuyaeleza hapa yote kila mtu hatisoma hii thread kwa kuwa nimmengi mno.

Wazungu wanatufanya sie kama vifaa vya kazi na si binadamu.

Kuna Boss wangu ni mzungu mgeni amabaye alikuwa kama na miaka miwili tu hapa Tz. Lakini alikuwa anawasimulia wafanyakazi wenzangu kuwa.." Hapa TZ ukitaka kuishi kwa amani inabidi uwe na pesa halafu uelwane na wahindi basi.. in Tanznia there is no law. If you have money and good communication with Indian you get VISA and you live comfotably even if its the whole family of yours. Juzi watanzania wenzetu wamefia mgodini chini ya ardhi lakini wanaokuja kufanya uchunguzi ni wazungu wenzao, wataalam wa nchi yetu mko wapi.

Mheshimiwa Slaa baba uko wapi. Njoo huku migodini angalau uongee na watanzania uone wanvyoteseka.
Ahh yaani nchi inakatisha tamaa. Sasa hivi watanzania wanfukuzwa kazi kwa visingizio vya wizi halafu wanakwambia nenda kokote maana hata rais wako anajua.

Wakishakufukuza wanaleta Makaburu kushikilia nafasi hizi.

HOWEVER HII STORY YA ADELINA NADHANI HATA TAMWA WANAITAMBUA.

Wewe ndo umenitia uchungu zaidi kuliko hata taarifa ya Adeline. Kuhusu Adeline nafikiri huo mfumo wa uandishi siyo mzuri. Ni wa kudhalilisha, mbona huwa tuna tafsida nyingi tu, au huyu mwandishi alikimbia somo la kiswahili?
Joloe, Tanzania hatuna viongozi ujue!!! Hivi ulishawahi kujua kwamba hii nchi inaongozwe na genge fulani la majambazi ambao wapo madarakani kwa ajili ya manufaa yao binafsi na si maisha ya watanzania? Angalia wakenya wanavyochezea uchumi wa tanzania, angalia waarabu wanavyovuna maliasili zetu na kuzipeleka kwao, angalia hao Geita, barrick na wangineo wanavyovuna dhahabu zetu na kutokomea nazo kwao, halafu wazalendo wananyanyasika, ili hali hata kodi tu hao wazungu wanakwepa kulipa. Uliza hizo dhahabu na almasi zinazochimbuliwa zinachangia kiasi gani cha uchumi wa taifa.
Nenda mipakani hata mpaka wa namanga tu kuingia Kenya, halafu ulinganishe hali ilivyo kwa bidhaa zinazotoka tanzania kuingia kenya, siku ya pili urudi kwa njia hiyohiyo kutoka kenya kuja Tanzania uone tofauti. Angalia wakenya wanavyojizolea watalii kupitia mlima kilimanjaro na mbuga ya serengeti. sisi tunang'aa macho tu. Wahindi ndiyo wanaoendesha nchi yetu na kujipangia kila wanachotaka bila kujali hali za maisha ya watanzania wazelendo. Hii hali ina mwisho wake, nilishawahi kusema hili na ninalirudia. Siku inakuja hapo ambapo watanzania watachoka na watasema liwalo na liwe.
 
Wewe ndo umenitia uchungu zaidi kuliko hata taarifa ya Adeline. Kuhusu Adeline nafikiri huo mfumo wa uandishi siyo mzuri. Ni wa kudhalilisha, mbona huwa tuna tafsida nyingi tu, au huyu mwandishi alikimbia somo la kiswahili?
Joloe, Tanzania hatuna viongozi ujue!!! Hivi ulishawahi kujua kwamba hii nchi inaongozwe na genge fulani la majambazi ambao wapo madarakani kwa ajili ya manufaa yao binafsi na si maisha ya watanzania? Angalia wakenya wanavyochezea uchumi wa tanzania, angalia waarabu wanavyovuna maliasili zetu na kuzipeleka kwao, angalia hao Geita, barrick na wangineo wanavyovuna dhahabu zetu na kutokomea nazo kwao, halafu wazalendo wananyanyasika, ili hali hata kodi tu hao wazungu wanakwepa kulipa. Uliza hizo dhahabu na almasi zinazochimbuliwa zinachangia kiasi gani cha uchumi wa taifa.
Nenda mipakani hata mpaka wa namanga tu kuingia Kenya, halafu ulinganishe hali ilivyo kwa bidhaa zinazotoka tanzania kuingia kenya, siku ya pili urudi kwa njia hiyohiyo kutoka kenya kuja Tanzania uone tofauti. Angalia wakenya wanavyojizolea watalii kupitia mlima kilimanjaro na mbuga ya serengeti. sisi tunang'aa macho tu. Wahindi ndiyo wanaoendesha nchi yetu na kujipangia kila wanachotaka bila kujali hali za maisha ya watanzania wazelendo. Hii hali ina mwisho wake, nilishawahi kusema hili na ninalirudia. Siku inakuja hapo ambapo watanzania watachoka na watasema liwalo na liwe.

Ndg yangu kuna wakati huwa natamani ningezaliwa kenya. Nawapenda kenya sababu ni watu wa KU DARE. Siku zote huwa naamini hii nchi yetu ina mazezeta wengi. Na kila siku rais wa nchi utamsikia anasema eti " nitapata ushindi wa kishindo' Swali langu ni hivi huyu rais nani huwa anampigia kura.???
Tangu vyama vingi vianze sijawahi hata siku moja kumpa KURA yangu mtu wa CCM. Mwaka 2000 kuna mmoja wa wabunge wa CCM ni babu yangu lakini bado kwa jinsi ninavoichukia CCM hakuipata kura yangu.
Waislam wana kifungu fulani cha kwenye quran kinasema " Kitu kikikukera basi kiondoe kwa mkono wako, la basi kikanye kwa mdomo na hili likikushinda basi Nuna uonyeshe umekereka"
I hate every person suppoting this majambazi wa tanzania
 
kashikwa nyeti?hahaaaa mambo haya bana yanatia raha sana na kusikitisha as well
 
Duh,so sad!!!
Ki ukweli jamaani - mtu anaefanya kazi mgodi ni mtumwa!!!!!!
Atakaebisha na abishe kwa kiasi kikubwa lakini mwisho wa siku atakiri ni utumwa maana ni ajira rahisi kupata na rahisi kuipoteza na kwa kusingiziwa lolote,na kama kweli makaburu ndo viongozi wa migodi hii,utasikia mengi zaidi ya hayooo!!
Hapa ndipo tunapoweza kulia kwa uchungu kumkumbuka baba wa taifa - alituasa juu ya ukaburu, nasikitika sana viongozi tulionao wengi wao wana roho za ukaburu sio wote ila wengi wao!!!
Maana kama mtu anakufanya unyama wa namna hii afu hata hakukamatwa na polisi!basi ukaburu utaimaliza tz yetu , eeh Mungu tusaidie sisi na watoto wetu,Amen.
 
Sijafurahia Lugha ya mwandishi. Angeweza tumia maneno mbadala (sijui wanaita tafsida) ili kuwakilisha taarifa yake. Otherwise sijui huyu jamaa alisoma wapi...
 
Duh,so sad!!!
Ki ukweli jamaani - mtu anaefanya kazi mgodi ni mtumwa!!!!!!
Atakaebisha na abishe kwa kiasi kikubwa lakini mwisho wa siku atakiri ni utumwa maana ni ajira rahisi kupata na rahisi kuipoteza na kwa kusingiziwa lolote,na kama kweli makaburu ndo viongozi wa migodi hii,utasikia mengi zaidi ya hayooo!!
Hapa ndipo tunapoweza kulia kwa uchungu kumkumbuka baba wa taifa - alituasa juu ya ukaburu, nasikitika sana viongozi tulionao wengi wao wana roho za ukaburu sio wote ila wengi wao!!!
Maana kama mtu anakufanya unyama wa namna hii afu hata hakukamatwa na polisi!basi ukaburu utaimaliza tz yetu , eeh Mungu tusaidie sisi na watoto wetu,Amen.

Kwani wewe umewahi kufanya migodini( mambo ya The Deep?
 
Nilipoona Hii Comment yako mkuu, mpaka machozi yamenitoka.

Mi si mwandishi mzuri, Lakini huwa kuna wakt natamani nikutane na rais nimuulize hili swali.. "KWA NINI UMEAMUA KUIUZA NCHI YETU KWA WAGENI, NCHI AMBAYO BABA WA TAIFA AMEPAMBANA VILIVYO KUIPA UHURU?"

Nahisi kuna watu wanaokaa mbali na migodi wanashangaa hali hii kutokea lakini mtu aliyeandika story nimependa sana.

Hili tukio wakt linatokea mi nilikuwepo live. Na haya matukio huku kwetu yamezoeleka kabisa. Wazungu wanafanya kila wanachotaka na hakuna wa kubisha.

Wengine wanafanya haya halafu wanakwambia nenda mahakamni kama unaona umeonewa. Ni kama wafanyakazi wa migodini ni watumwa ndani ya nchi yao. Ukienda mahakamni nako Hakimu either ataomba rushwa ama ataanza kuiskiliza kesi yako huko mtaani ili ajue ni jinsi gani atapata pesa kutoka kwa hao wazungu. Ukitaka kufanya kazi kwa amani inabidi uwe mnafiki kwa wazungu ndo uatishi kwa raha mstarehe. Kuna matukio mengi ya kutisha ambayo kama nikamua kuyaeleza hapa yote kila mtu hatisoma hii thread kwa kuwa nimmengi mno.

Wazungu wanatufanya sie kama vifaa vya kazi na si binadamu.

Kuna Boss wangu ni mzungu mgeni amabaye alikuwa kama na miaka miwili tu hapa Tz. Lakini alikuwa anawasimulia wafanyakazi wenzangu kuwa.." Hapa TZ ukitaka kuishi kwa amani inabidi uwe na pesa halafu uelwane na wahindi basi.. in Tanznia there is no law. If you have money and good communication with Indian you get VISA and you live comfotably even if its the whole family of yours. Juzi watanzania wenzetu wamefia mgodini chini ya ardhi lakini wanaokuja kufanya uchunguzi ni wazungu wenzao, wataalam wa nchi yetu mko wapi.

Mheshimiwa Slaa baba uko wapi. Njoo huku migodini angalau uongee na watanzania uone wanvyoteseka.
Ahh yaani nchi inakatisha tamaa. Sasa hivi watanzania wanfukuzwa kazi kwa visingizio vya wizi halafu wanakwambia nenda kokote maana hata rais wako anajua.

Wakishakufukuza wanaleta Makaburu kushikilia nafasi hizi.

HOWEVER HII STORY YA ADELINA NADHANI HATA TAMWA WANAITAMBUA.


F@#$%uck everything...wazungu na sanaaa watanzania wote hasa nyie mnaofanya kazi migodini.....HIVI BILA MIGODI HAMUWEZI KUISHI???...au ndio utumwa wa fikra uliowajaa watanzania mlio wengi kuwa ni lazima muajiriwe na mulipwe as if hamna akili za kufikiria na kufanya mambo yenu mengine???...UTUMWA WA FIKRA...viongozi wenu wanafikiria ili nchi iendelee lazma kuwa na wawekezaji wazungu, nyie nao mnafikiiria ili muendelee lazma muajiriwe....watoto wenu nao wakitoka vyuoni wanawazia kuajiriwa..na wajukuu zenu viunoni mwa watoto wenu wanafikiria kuajiriwa...mpaka vifo vyenu ...MTALIA NA KUSAGA MENO...suluhisho ni kubadilika KIFIKIRA NA KUAMINI KUWA SIO LAZMA MUENDELEE KUWA WATUMWA NA KUWATEGEMEA WAZUNGU NA MIGODI....nchi ngapi hazina migodi na maisha yanaendelea???...WAKE UP TANZANIANS...THINK OUT OF A BOX...watumwa nyie...pu$%^&&&mbafuuuuuu....

NI MAONI TUU WADAU SEMA YAMEJAA HASIRA NA CHEMBECHEMBE ZA UTAIFA ZILIZOELEMEA KWENYE MITAZAMO YA SHUJAA WETU Mwl. J.K. NYERERE
 
F@#$%uck everything...wazungu na sanaaa watanzania wote hasa nyie mnaofanya kazi migodini.....HIVI BILA MIGODI HAMUWEZI KUISHI???...au ndio utumwa wa fikra uliowajaa watanzania mlio wengi kuwa ni lazima muajiriwe na mulipwe as if hamna akili za kufikiria na kufanya mambo yenu mengine???...UTUMWA WA FIKRA...viongozi wenu wanafikiria ili nchi iendelee lazma kuwa na wawekezaji wazungu, nyie nao mnafikiiria ili muendelee lazma muajiriwe....watoto wenu nao wakitoka vyuoni wanawazia kuajiriwa..na wajukuu zenu viunoni mwa watoto wenu wanafikiria kuajiriwa...mpaka vifo vyenu ...MTALIA NA KUSAGA MENO...suluhisho ni kubadilika KIFIKIRA NA KUAMINI KUWA SIO LAZMA MUENDELEE KUWA WATUMWA NA KUWATEGEMEA WAZUNGU NA MIGODI....nchi ngapi hazina migodi na maisha yanaendelea???...WAKE UP TANZANIANS...THINK OUT OF A BOX...watumwa nyie...pu$%^&&&mbafuuuuuu....

NI MAONI TUU WADAU SEMA YAMEJAA HASIRA NA CHEMBECHEMBE ZA UTAIFA ZILIZOELEMEA KWENYE MITAZAMO YA SHUJAA WETU Mwl. J.K. NYERERE

Kila uanpotaka kuandika punguza hasira ndg yangu. uatakuwa si msaada tena.
Hakuna mtu dunian mwenye ujasiri wa kufa nja wakti chakula anakiona.
Ukiona mtu aina hiyo basi si binadamu wa kawaida. Nchi yetu imejaa ufisadi kote. auatenda wapi hebu fikiria jinsi familia zetu zilivyo maskini. Kuna watu wangapi mama zao ni wajane na wadogo zao wanawategemea hao kaka ama dada zao ili waende shule. Ukiacha kazi kesho yake unaambia na mama yako ile nyumba alikyokuwa akiishi imeenda na mafuriko. Wakati huo sehemu pekee ya wewe kupata ajira ni huko kwa makburu. Utafanya nini.
Ni watu wangapi wanfanya kazi ili familia zao zipaate hata mlo wa siku moja.
hAYO MANENO YAKO YANANIFANYA NIAMINI KUWA WEWE HUISHI TZ NADHANI UKO ULAYA AMA USA NDO MAANA UNATHUBUTU KUONGEA MANENO HAYO. Naomba usiwalaumu watanzania ila jaribu kutumia mwanga uliyonao kuwapa mbinu ni nini cha kufanya na sio kutukana. Unawakosea watanzania wanaokufa njaa na mafuriko ya kila siku.
 
Back
Top Bottom