Benson Mramba
JF-Expert Member
- Oct 29, 2013
- 644
- 1,482
Kwanza naomba ifahamike kuwa mimi ni muumini na mfuasi wa siasa na sera za Magufuli na ninaamini ndie kiongozi Bora kuwahi kuwepo Tanzania na Afrika kwa miaka ya karibuni.
Kwa miaka mitano mishahara haikuwahi kupanda ila mfumuko wa bei ulidhibitiwa na watumishi wengi walilipwa malimbikizo yao ya madeni ya likizo, pensheni na kupanda vyeo na uhamisho. Wengi walipandwishwa vyeo kwa kukopwa. Cheo kimepanda ila stahiki zikabaki kuwa madeni. Magufuli alilipa hayo madeni.
Sijui kama Mungu angemjalia uhai mpaka leo ambapo Bwawa la Umeme lingekuwa limekamilika na SGR kipande cha Dar Moro kuanza kazi Je asingepandisha mishahara au angepandisha maana ahadi yake ni kuwa angepandisha mishahara baada ya hii miradi ya kimkakati kukamilika.
Naamini angepandisha mshahara na mfumuko bado ungekuwa chini.
Mama amepandisha mshahara kwa 23.3% Sawa ni jambo zuri je nyongeza hii italeta unafuu wowote kwa mfanyakazi?
Mathalani mtu aliyekuwa akilipwa laki 3 wakati Unga ni tsh 800-1000, mchele 1000-1500, mafuta ya kupikia 3000-4000, nauli ya daladala 300-600 mafuta ya petrol 1800-2000 leo hii atalipwa tsh 360,000+ lakini wakati huo huo Unga ni 1300-1600, mchele ni 2000-2800, mafuta ya kupikia ni 7000-8000, nauli ya daladala ni 500-1200, petrol ni 3100-3500 n.k
Swali ni je kwa mfumuko huu wa bei nyongeza hiyo itamsaidia nini mfanyakazi? Hapa ni Sawa na mtu mwenye presha anakula wali wenye chumvi kwa kusukumia na chai yenye sukari au kunywa pepsi kwa kuichanganya na maji huku ukiamini sukari hainaingia mwilini.
Mama anacheza na akili za wafanyakazi. Kwa gharama za maisha zilivyo sasa hata nyongeza ingekuwa 50% bado uwiano ungekuwa ni ule ule wa miaka 5 iliyopita ambapo hatukuwa na nyongeza.
Kumbukeni mfano wa Mwl Nyerere kuhusu yule zuzu na kipande cha glasi akidhani ni almasi
Wafanyakazi lilieni mfumuko udhibitiwe maana hamjui kesho vitu vitauzwaje na bando litakuwa bei gani. Fungueni macho ili mkiona muone
Kwa miaka mitano mishahara haikuwahi kupanda ila mfumuko wa bei ulidhibitiwa na watumishi wengi walilipwa malimbikizo yao ya madeni ya likizo, pensheni na kupanda vyeo na uhamisho. Wengi walipandwishwa vyeo kwa kukopwa. Cheo kimepanda ila stahiki zikabaki kuwa madeni. Magufuli alilipa hayo madeni.
Sijui kama Mungu angemjalia uhai mpaka leo ambapo Bwawa la Umeme lingekuwa limekamilika na SGR kipande cha Dar Moro kuanza kazi Je asingepandisha mishahara au angepandisha maana ahadi yake ni kuwa angepandisha mishahara baada ya hii miradi ya kimkakati kukamilika.
Naamini angepandisha mshahara na mfumuko bado ungekuwa chini.
Mama amepandisha mshahara kwa 23.3% Sawa ni jambo zuri je nyongeza hii italeta unafuu wowote kwa mfanyakazi?
Mathalani mtu aliyekuwa akilipwa laki 3 wakati Unga ni tsh 800-1000, mchele 1000-1500, mafuta ya kupikia 3000-4000, nauli ya daladala 300-600 mafuta ya petrol 1800-2000 leo hii atalipwa tsh 360,000+ lakini wakati huo huo Unga ni 1300-1600, mchele ni 2000-2800, mafuta ya kupikia ni 7000-8000, nauli ya daladala ni 500-1200, petrol ni 3100-3500 n.k
Swali ni je kwa mfumuko huu wa bei nyongeza hiyo itamsaidia nini mfanyakazi? Hapa ni Sawa na mtu mwenye presha anakula wali wenye chumvi kwa kusukumia na chai yenye sukari au kunywa pepsi kwa kuichanganya na maji huku ukiamini sukari hainaingia mwilini.
Mama anacheza na akili za wafanyakazi. Kwa gharama za maisha zilivyo sasa hata nyongeza ingekuwa 50% bado uwiano ungekuwa ni ule ule wa miaka 5 iliyopita ambapo hatukuwa na nyongeza.
Kumbukeni mfano wa Mwl Nyerere kuhusu yule zuzu na kipande cha glasi akidhani ni almasi
Wafanyakazi lilieni mfumuko udhibitiwe maana hamjui kesho vitu vitauzwaje na bando litakuwa bei gani. Fungueni macho ili mkiona muone