Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
WAFANYABIASHARA watano wamefikishwa mahakamani na kusomewa mashitaka ya kuiibia Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) mamilioni ya fedha akiwemo mfanyabiashara Maarufu Nassor Said Nassir (Bopar) anayemiliki maduka kadhaa ya bidhaa mbali mbali visiwani Zanzibar.
Mfanyabiashara huyo maarufu Zanzibar Mkaazi wa Kiembe samaki Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja anadaiwa kuiibia Benki ya Watu wa Zanzibar dola 880,000 kwa kushirikiana na mwenzake Sleyum Mbaraka.
Mwendesha mashitaka katika kesi hiyo iliyosomwa katika mahakama ya Mkoa Vuga Mjini, Khamis Suwedi alisema wafanyabiashara hao wawili walitenda kosa hilo mnamo Machi 11 mwaka huu baada ya kula njama na kuiba fedha hizo kinyume na sheria.
Bopar ni mfanyabiashara maarufu Zanzibar mwenye asili ya Asia aliyekuwa akiingiza bidhaa za mchele, unga wa ngano, na bidhaa nyenginezo katika soko la ndani la Zanzibar ikiwemo mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku na serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Waliofikishwa mahakamani jana na kusomewa shitaka la kuiba fedha za Benki ya Taifa ni Juma Abass Juma (44) mkaazi wa Amani anayetuhumiwa kuiibia PBZ dola za Marekani 341,220,000 mwengine ni mfanyabiashara Ramadhan Issa Jecha (47) mkaazi wa Mwanakwerekwe ambaye anatuhumiwa kuiibia Benki hiyo fedha taslimu milioni 379, 240,000.
Akisoma mashitaka hayo mwendesha mashitaka huyo alisema washitakiwa kwa nyakati tofauti walifanikiwa kuiibia benki hiyo kwa njia za udanganyifu vitendo ambavyo ni kinyume na sheria ya makosa ya jinai
Mwendesha mashitaka Khamis Suwedi alieleza mahakamani hapo kwamba wafanyabiashara hao Juma Abbas Othman na Zahor Mbaraka Salum kwa kushirikiana walifanikiwa kuiibia PBZ dola za Marekani 340,000,000
Akisoma hati ya mashitaka alisema kitendo hicho kimefanyika kati ya Machi 11 na 19 bada ya wahusika kutenda kosa la wizi na kufikishwa mahakamani hapo ambapo mshtakiwa Sleyum Mbaraka naye alidaiwa kuiibia benki hiyo kati ya Machi 12 ba 19 dola za Marekani 1,220,000
Washitakiwa wamerejeshwa rumande katika gereza la Kiinua Miguu Kilimani Mjini Unguja, baada ya upande wa mashitaka kupinga maoni ya dhamana kwa vile kiwango cha fedha kilichoibwa ni kikubwa ba kuwepo kwao nje kunaweza kuathiri hatua za uchunguzi za kesi hiyo.
Hata hivyo Hakimu Mkusa Issac Sepetu alisema suala la dhamana kwa washitakiwa hao atalitolea uamuzi Julai 28 mwaka huu.
Awali wakili anaemtetea mshitakiwa Bopar Hamid Mbwezeleni aliitaka mahakama kumuangalia mteja wake kumpatia dhamana ili kuepusha shughuli zake za biashara kuathirika katika kipindi atakachokuwepo ndani.
Benki ya Watu wa Zanzibar ndio inayotumiwa na idadi kubwa ya wakulima na wafanyabiashara kuhifadhi fedha zao lakini hivi karibuni kumekuwepo na matukio ya kupotea fedha katika akiba za wateja ambapo hivi karibuni zaidi ya milini 200 ziliibwa katika mazingira ya kutatanisha kutoka katika akaunti ya mfuko wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa kambi ya upinzani waliofungua katika Benki hiyo.
SOURCE: ZANZIBAR YETU.
Mfanyabiashara huyo maarufu Zanzibar Mkaazi wa Kiembe samaki Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja anadaiwa kuiibia Benki ya Watu wa Zanzibar dola 880,000 kwa kushirikiana na mwenzake Sleyum Mbaraka.
Mwendesha mashitaka katika kesi hiyo iliyosomwa katika mahakama ya Mkoa Vuga Mjini, Khamis Suwedi alisema wafanyabiashara hao wawili walitenda kosa hilo mnamo Machi 11 mwaka huu baada ya kula njama na kuiba fedha hizo kinyume na sheria.
Bopar ni mfanyabiashara maarufu Zanzibar mwenye asili ya Asia aliyekuwa akiingiza bidhaa za mchele, unga wa ngano, na bidhaa nyenginezo katika soko la ndani la Zanzibar ikiwemo mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku na serikali ya mapinduzi Zanzibar.
Waliofikishwa mahakamani jana na kusomewa shitaka la kuiba fedha za Benki ya Taifa ni Juma Abass Juma (44) mkaazi wa Amani anayetuhumiwa kuiibia PBZ dola za Marekani 341,220,000 mwengine ni mfanyabiashara Ramadhan Issa Jecha (47) mkaazi wa Mwanakwerekwe ambaye anatuhumiwa kuiibia Benki hiyo fedha taslimu milioni 379, 240,000.
Akisoma mashitaka hayo mwendesha mashitaka huyo alisema washitakiwa kwa nyakati tofauti walifanikiwa kuiibia benki hiyo kwa njia za udanganyifu vitendo ambavyo ni kinyume na sheria ya makosa ya jinai
Mwendesha mashitaka Khamis Suwedi alieleza mahakamani hapo kwamba wafanyabiashara hao Juma Abbas Othman na Zahor Mbaraka Salum kwa kushirikiana walifanikiwa kuiibia PBZ dola za Marekani 340,000,000
Akisoma hati ya mashitaka alisema kitendo hicho kimefanyika kati ya Machi 11 na 19 bada ya wahusika kutenda kosa la wizi na kufikishwa mahakamani hapo ambapo mshtakiwa Sleyum Mbaraka naye alidaiwa kuiibia benki hiyo kati ya Machi 12 ba 19 dola za Marekani 1,220,000
Washitakiwa wamerejeshwa rumande katika gereza la Kiinua Miguu Kilimani Mjini Unguja, baada ya upande wa mashitaka kupinga maoni ya dhamana kwa vile kiwango cha fedha kilichoibwa ni kikubwa ba kuwepo kwao nje kunaweza kuathiri hatua za uchunguzi za kesi hiyo.
Hata hivyo Hakimu Mkusa Issac Sepetu alisema suala la dhamana kwa washitakiwa hao atalitolea uamuzi Julai 28 mwaka huu.
Awali wakili anaemtetea mshitakiwa Bopar Hamid Mbwezeleni aliitaka mahakama kumuangalia mteja wake kumpatia dhamana ili kuepusha shughuli zake za biashara kuathirika katika kipindi atakachokuwepo ndani.
Benki ya Watu wa Zanzibar ndio inayotumiwa na idadi kubwa ya wakulima na wafanyabiashara kuhifadhi fedha zao lakini hivi karibuni kumekuwepo na matukio ya kupotea fedha katika akiba za wateja ambapo hivi karibuni zaidi ya milini 200 ziliibwa katika mazingira ya kutatanisha kutoka katika akaunti ya mfuko wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa kambi ya upinzani waliofungua katika Benki hiyo.
SOURCE: ZANZIBAR YETU.