Mfanyabiashara aua majambazi watatu

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Mfanyabiashara aua majambazi watatu
Hellen Mlacky, Moshi
Daily News; Tuesday,June 24, 2008 @00:03

Majambazi watatu, akiwamo raia wa Kenya wameuawa kwa kupigwa risasi na mfanyabiashara waliyekuwa wakipora katika baa yake juzi usiku. Kwa mujibu wa Polisi majambazi wengine watatu walikimbia na fedha walizokuwa wamepora na kutokomea pasipojulikana na kutelekeza mali nyingine walizokuwa wameiba baada ya kushambuliwa.

Wanadaiwa walikuwa tishio kwa kuwavamia wateja katika baa mbalimbali na nyumba za kulala wageni katika maeneo ya Marangu na kuwapora mali zikiwamo simu za mkononi na fedha.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Ramadhani Baruti, aliwaambia waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa tatu usiku katika eneo la Mamba Kiria, wilayani Moshi Vijijini.

Alisema kuwa usiku wa tukio hilo majambazi sita wakiwa na bastola walivamia baa ya Market View mali ya Erick Shayo (40) na kuwaweka wateja chini ya ulinzi huku wakifyatua risasi hewani.

Wateja walitii amri na kuamriwa kutoa mali walizokuwa nazo, wakapora kaunta na baadaye katika vyumba vitatu vya wageni. Baruti alisema kuwa baada ya majambazi hao kutekeleza azma yao kwa nusu saa waliondoka kwenye baa hiyo na kwenda baa ya Egbert Maleko ambako mauti yaliwakuta.

Kaimu Kamanda huyo alisema kuwa wakati majambazi hao walipowaweka wateja chini ya ulinzi, Maleko alipata upenyo na kukimbia nyumbani na kuchukua bunduki yake aina ya shotgun yenye risasi nane na kuwashambulia majambazi, kwanza kwa kumpiga risasi ya shingoni aliyekuwa na bastola aliyeanguka chini na kuiachia, akampiga mwingine usoni hadi akadondoka nje ya baa na wa tatu alipigwa risasi makalio.

Alisema kuwa baada ya majambazi hao kupekuliwa mmoja alikutwa na kitambulisho cha Kenya chenye namba 4899725 kilichotolewa Machi 27 mwaka 2001 huko Uasingishu, Loitoktok. Polisi wanasema alikutwa na bastola aina ya Beretta yenye namba 642206 ikiwa na risasi sita.

Majambazi wengine hawakutambuliwa majina wala uraia wao na wanakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30 na 40. Polisi inamshikilia Honest Fares Moshi (29), mkazi wa Mamba Marangu kwa mahojiano zaidi kwa kuhusishwa na tuhuma za tukio hilo na kuendelea kuwasaka wengine waliokimbia.
 
Haya majambawazi yalikuwa yamekufa sasa yameanza kufufuka chonde chonde tuyapigie kura kuyafichua mbona tutakwisha?????????
 
Let this serve as a lesson to the others .... huyo mfanyabiashara anastahili pongezi
 
Ombi la kumrudisha kamanda Tossi Kilimanjaro ili amani irejee

Tusizungumzie Kilimanjaro tuu. Hebu tuangalie Arusha pia. Huu mkoa umekuwa na matukio mabaya sana ya wizi wa kutumia silaha, matukio yake hayaandikwi sijui kwanini??? Wizi unatokea hata jirani na makazi ya askari ila wao wanakuja baada ya jamaa kuondoka. Shall we think there is something behind??? Tunamkumbuka sana Kamanda Kombe, Mungu amuongezee maisha, wakati wa utawala wake tulisahau kama kuna watu wanaitwa wezi hapa Arusha, pia wana usalama barabarani waliacha tabia zao za kujifanya magari yote yapitayo barabarani wana hisa nayo, kwani kuomba rushwa kuliisha, amani ilikuwepo. Sasa ukitoka na gari lazima uwe na senti za kuchunga gari,. If possible, Kamanda Mwema anatakiwa aangalie hii Mikoa upya.

Kasi aliyoanza nayo imepungua na watendaji wake wasio waaminifu wanachukua nafasi ya kuliharibu jeshi la Polisi. Bado muda upo wa kulisahihisha.
 
Let this serve as a lesson to the others .... huyo mfanyabiashara anastahili pongezi


...naam, anastahili na ulinzi pia, kuna hao watatu 'waliokimbia!', namatumaini pia kwa hizo serial numbers, watafuatiliwa wanaozimiliki, iwe ni Tanzania au Kenya, hata kama ni toka polisi au jeshini.
 
tossi uko wapi jamani mashemeji zako wameshaanza kazi?????
 
Mboana sehemu kuwa ya matukio ya ujambazi yamekuwa yanawahusisha raia wa Kenya?
 
Halafu huyo mangi katambaa hadi kufuata bastola..duh!! mchagga kwa pesa!! Sasa yeye ndo angepigwa risasi ya makalio?
 
Mboana sehemu kuwa ya matukio ya ujambazi yamekuwa yanawahusisha raia wa Kenya?
Kichuguu Mkuu,
Walishaambizana kuwa TZ ndio njia ya mkato kupata kile unachokitafuta maana hata Polisi wenyewe wakivua Uniform wanakuwa wenzao katika purukushani
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom