Mfanyabiashara ahukumiwa kunyongwa Dar, alimuua mdai wake aliyempa hela amuagizie Fuso

Kwa hiyo, marehemu aliuwawa kwa sababu alidai chake?

Na kwamba hela aliyokuwa anadai marehemu ilinunulia nyumba Magomeni badala ya kununulia Fuso kama marehemu alivyokubaliana na mshtakiwa/muuaj...
Tatizo kuna watu wanadaigi kwa jazba kejeli na matusi tena hadharani. Sasa hii inapelekea kumpa nafasi shetani atawale nafsi na akili ya mdaiwa nakusababisha sintomfaham kupelekea kufanya mauaji bila kujijua.

Mnakumbuka kisa cha uriah aluvyokuwa anadai chake mke wake kwa Daudi? Alikomaa hadi akakataa kwenda nyumbani. Daudi alimaindi kichiz akaamua tu kumpoteza.

Dawa ya deni ni kulipa. Tusiwe wachoyo na tamaa zembe. Dhulma ni mbaya inasababisha mdaiwa kuwa na hasira za kijinga akidaiwa nakupelekea kuua nafsi isiyokuwa na hatia.

Saa zingine ukimdai mtu anakukwepa na kukudhulumu muachie Mungu tu. Jamaa angemuachia Mungu asingeuwawa.

Acha anyongwe tu.
 
Inasemekana japo niliipata miaka mingi huko nyuma.

Aliyeuliwa (baba feisari) alikuwa anafanya kazi ubungo kwenye mabus ya muuaji.

Wakachanga na muuaji ili wanunue gari lao.

Marehemu siku hiyo ameenda job na alikuwa na tabia ya kumpigia mke wake cm kila saa nne au saa kumi, cm hakupiga siku hiyo.

Hapo ndugu wakaanza kutafuta.

Baadae sana inasemekana aliyepanga pale alipofukiwa marehemu, akipaki gari nje usiku anasikia linawashwa, mwisho mpangaji kafanya kisomo.

Ndo ikawa mwanzo wa marehemu kujulikana, ni mengi mno,

Ila ninayo hii strory full, nawahi job.
 
Kwa hiyo, marehemu aliuwawa kwa sababu alidai chake?

Na kwamba hela aliyokuwa anadai marehemu ilinunulia nyumba Magomeni badala ya kununulia Fuso kama marehemu alivyokubaliana na mshtakiwa/muuaji?

Kwa hiyo Marehemu na Muuaji walikuwa wanaaminiana kiasi cha marehemu kumpa hela muuaji akamwagizie Fuso?

Hivyo basi, bwana muuaji aliingia tamaa na kumdhulumu marehemu pesa na roho yake?

Kikulacho ki nguoni mwako!
Hpn muuaji ndie aliye mpa pesa jamaa amuagizie gari Aina ya fuso ikapita muda bila kuletewa gari ndipo muuaji akamuita jamaa na Kisha kuja kumuua nyumbni kwake aliko panga bean muuaji
 
Dah, hiii kesi nakumbuka hii,

Jamaa alipohama na kuhamia kusikojulikana,

Mpangaji aliyehamia baadae ndiye aliyegundua shimo ambalo lilikuwa linatitia,

Ikabidi aitwe mwenye nyumba kukiwa na Mjumbe na polisi,

Hapo ndiyo waligunduwa mabaki ya mwili wa marehemu.
Mimi nakumbuka mke wa Marehemu alienda kuripoti polisi kupotea Kwa Mumewe na kuulizwa NI Nani anaemshuku ndio akamtaja mtuhumiwa Kwa sababu alipoondoka aliaga anaenda Kwa Mtuhumiwa kuchukua gari yake.
Ndipo polisi wakamshika Mtuhumiwa baada msago kidogo akakiri na kuwapeleka polisi alipofanya tukio
 
Wabongo wana Roho mbaya sana aisee duuh yaani kamuua mtu kamfukia na inawezekana kafukia wengi ajaanza kwa huyo tuu...daah huyo inatakiwa anyongwe haraka asipewe hata nafasi ya kuvuta sigara..yaani ilikua akitoka mahakani ni kwenye kitanzi sio mambo ya kusubiri rufaa kwa makatili..
 
Mfanyabiashara Hemed Ally amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa kukusudia Farihani Maluni.

Habari inaeleza Farihani alimpa milioni 30 Hemed amuagizie lori aina ya fuso na baada ya muda mrefu kupita bila ya lori kufika na mdai kulidai, Ally alimuita Farihani nyumbani kwake alipopanga eneo la Sharif Shamba, Ilala.

Hamjat Nassoro wakati akitoa ushahidi wake ambae ndie mmiliki wa nyumba hiyo alisema Ally hakumaliza kodi yake ya mwaka wa pili na alikaa miezi mitano pekee akidai amenunua nyumba Magomeni hivyo anahama.

Hamjat amesema wakati Ally akiishi kwenye nyumba hiyo alimuomba ruhusa aende kwa mjumbe ili achimbe shimo nje ya nyumba atapishe maji kutokana na shimo kujaa majitaka hata hivyo mjumbe hakutoa ruhusa.

Ally alirudi kwa Hamjat akimwomba amruhusu achimbe shimo kwa ndani ya uzio wa nyumba ambapo alimruhusu kwa maelekezo afukie vizuri kama kulivyokuwa, shimo hilo lilitumika kumfukia marehemu Juni 12, 2014.

Februari 9, 2015 Hamjat alipokea simu kutoka kwa polisi wakimtaka aende katika nyumba yake kuna tukio mshtakiwa alilifanya naye akaenda na baada ya kufukua walikuta mabaki ya mwili wa Farihani ukiwa umefungwa kamba mikononi na plasta maeneo ya fuvu(Daktari alihisi ilitumika kumziba mdomo na kumsababishia akose pumzi).

Kama ushahidi umetimia na hakuna rushwa iliyotolewa auliwe na kusiwe na watetezi wa haki za binadamu.
 
Mfanyabiashara Hemed Ally amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa kukusudia Farihani Maluni.

Habari inaeleza Farihani alimpa milioni 30 Hemed amuagizie lori aina ya fuso na baada ya muda mrefu kupita bila ya lori kufika na mdai kulidai, Ally alimuita Farihani nyumbani kwake alipopanga eneo la Sharif Shamba, Ilala.

Hamjat Nassoro wakati akitoa ushahidi wake ambae ndie mmiliki wa nyumba hiyo alisema Ally hakumaliza kodi yake ya mwaka wa pili na alikaa miezi mitano pekee akidai amenunua nyumba Magomeni hivyo anahama.

Hamjat amesema wakati Ally akiishi kwenye nyumba hiyo alimuomba ruhusa aende kwa mjumbe ili achimbe shimo nje ya nyumba atapishe maji kutokana na shimo kujaa majitaka hata hivyo mjumbe hakutoa ruhusa.

Ally alirudi kwa Hamjat akimwomba amruhusu achimbe shimo kwa ndani ya uzio wa nyumba ambapo alimruhusu kwa maelekezo afukie vizuri kama kulivyokuwa, shimo hilo lilitumika kumfukia marehemu Juni 12, 2014.

Februari 9, 2015 Hamjat alipokea simu kutoka kwa polisi wakimtaka aende katika nyumba yake kuna tukio mshtakiwa alilifanya naye akaenda na baada ya kufukua walikuta mabaki ya mwili wa Farihani ukiwa umefungwa kamba mikononi na plasta maeneo ya fuvu(Daktari alihisi ilitumika kumziba mdomo na kumsababishia akose pumzi).

Ama kweli waarabu wa pemba hujuana kwa vilemba vyao
 
Back
Top Bottom