Mfanyabiashara afa akihojiwa na TRA

Selous

JF-Expert Member
Jan 13, 2008
1,325
144
MFANYABIASHARA maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Amri Amir, amefariki dunia ghafla wakati akihojiwa na maofisa wa Mamlaka ya Kodi ya Mapato nchini (TRA).

Tukio hilo lililoteka hisia za wananchi wengi wa mkoani Kagera, hususan wilayani Karagwe, lilitokea juzi wakati maofisa hao wa kodi kutoka Mwanza, walipofika ofisini kwake kwa ajili ya kuangalia kiasi cha kodi anachodaiwa mfanyabiashara huyo.

Kwa mujibu wa habari zilizothibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kagera, Henry Salewi, zilisema kuwa, Amir alifariki dunia wakati akiwa katikati ya mahojiano na maofisa hao wa TRA, ambao waliamua kutimka mara baada ya kifo hicho.

"Ni kweli Amir alifariki wakati akihojiwa na maofisa wa TRA. Wakati akiwa katikati ya mazungumzo ambayo bado hatujui yalisema nini, mfanyabiashara huyo alianguka ghafla, wengi wakihisi kuwa ni presha na baadaye alifariki dunia papo hapo. Naomba uweke sawa kwamba hakupigwa, bali alianguka ghafla na kufa," alisema Kamanda Salewi.

Alisema kutokana na utata wa kifo hicho, kamanda huyo kwa kushirikiana na ndugu wa marehemu, walikubali kutofanya mazishi jana ili kupisha uchunguzi uliofanyika jana.

Kamanda huyo alisema aliamuru kufanyika kwa uchunguzi wa mwili huo ili kuondoa wasiwasi ulioenezwa kuwa huenda alipigwa au amelishwa kitu chenye sumu.

"Bahati nzuri uchunguzi umefanyika leo (jana) na mazishi yamefanyika kijijini kwake, ila sijapata matokeo ya majibu kwa vile niko nje ya ofisi, tukiwasiliana kesho, nitakupa," alisema kamanda huyo.

Hata hivyo Kamanda Salewi hakuweza kutaja majina ya maofisa hao wa TRA kwa madai kuwa bado wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.

Habari zaidi kutoka Karagwe, zinasema kuwa mfanyabiashara huyo ambaye pia alikuwa mweka hazina wa CCM, wilaya, alikuwa mfadhili mkubwa wa CCM wilayani humo na kifo chake ni pigo kwa chama hicho tawala.

Mfanyabiashara huyo anayemiliki vituo vya mafuta mkoani Kagera na Mwanza, amekuwa mfadhili mkubwa wa chama hicho, kutokana na michango yake aliyoitoa mara kadhaa katika kukiwezesha, hasa wakati wa uchaguzi.

Hii inakuwa ni mara ya pili kwa tukio la kuanguka na kisha kufariki dunia akiwa anahojiwa, baada ya jambo kama hilo kutokea mwishoni mwa miaka ya 1990, wakati aliyepata kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Horace Kolimba, alipofikwa na mauti wakati akihojiwa na Kamati Kuu ya chama hicho tawala mjini Dodoma.

Source: Tanzania Daima
 
Inasikitisha! Ila nahisi pengine LABDA alikuwa na malimbikizo makubwa ya kodi ndio maana akapata presha!
 
Ninakubaliana na wewe mkuu Masaki,inavyoonyesha marehemu alikuwa haweki wazi hesabu zake hivyo watu wa TRA walivyofanya assessment akaonekana anatakiwa kulipa kodi kubwa sana pengine hilo ndilo lililopelekea mauti yake. Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Amri.
 
Alikuwa mfanyabiashara maarufu na kada wa sisiemu......... Amekufa wakati akihojiwa na maafisa wa TRA.... Akaanguka ghafla na kufariki.... Maafisa wakatimka mbio!!.. Kwa nini wakimbie kama hawajafanya kitu au walihofia kuhusiswa na kifo?.
PIP Amir Amir na poleni familia ya marehemu
 
Rest in peace Amir, ila hao maofisa nini kiliwafanya wakimbie? si walikuwa kwenye ukaguzi!!!!!!
 
Wakati kwa kawaida unapokimbia kitu kama hukukifanya ndio unaamsha hisia kuwa umehusika .... sasa walipokimbia ina maana walimwacha akiwa ofisini peke yake au walitoa taarifa then ndo wakakimbia?.. mh hata siwezipata majibu hapa.

Poleni wanaccm wa Kagera
 
shinikizo la damu...alikuwa anadaiwa kiasi gani?

Hawa jamaa walikwenda huko waka inflate hiyo kodi ili wamtoe upepo maana hizi ndiyo zao hasa wakati mwaka unakaribia kwisha na siku kuu zinakuwa nyingi. Ni victim wa mafisadi nadni ya TRA.
 
Too bad!Hao TRA officers badala wamkimbize hospitali wanakimbia?very stupid people!Lazima wahusishwe na hicho kifo probably walimuhoji under too much pressure ila na yeye alipaswa awaonye kama ana matatizo ya kiafya maana mtu haanguki tu just from no where!
 
Poleni wafiwa....Kwa nini hao maofisa wa TRA walikimbia sasa baada ya huyo bwana kuanguka na kufa??? Hawaononi inaweza kuwafanya watu wajenge hisia mbaya hata kama kweli alikuwa amepata pressure may be kutokana na kuonekana ana deni kubwa la kodi??
 
Nawapa pole sana wafiwa. Lakini itakuwaje sasa, huo uchunguzi wa TRA ndo utakuwa umefikia ukomo?
 
hawa jamaa walikwenda huko waka inflate hiyo kodi ili wamtoe upepo maana hizi ndiyo zao hasa wakati mwaka unakaribia kwisha na siku kuu zinakuwa nyingi. Ni victim wa mafisadi nadni ya tra.

haswa, nakubuliana na wewe mia kwa mia. You have just hit a nail on the head
 
Too bad!Hao TRA officers badala wamkimbize hospitali wanakimbia?very stupid people!Lazima wahusishwe na hicho kifo probably walimuhoji under too much pressure ila na yeye alipaswa awaonye kama ana matatizo ya kiafya maana mtu haanguki tu just from no where!
Kevo! Unaamini kwamba maafisa wa TRA wanaweza kumhoji Mfadhili na kada mkubwa wa CCM under too much pressure? Labda huijui vema nchi hii.
Katika Tanzania hii ya sasa kutumia madaraka yako kumhoji MFADHILI wa CCM kwa undani juu ya fedha zake na kwa nini halipi kodi, unakata tiketi ya kwenda kulima kwenu kijijini. Habari ndio hiyo.
Mungu amlaze pema.
 
Inasikitisha! Ila nahisi pengine LABDA alikuwa na malimbikizo makubwa ya kodi ndio maana akapata presha!


Kusikitisha inasikitisha sana si kwa huyo aliye kufa tu kwa Watanzania wote kwa ujumla. Naamini kabisa huyo Mfanya biashara amekufa kutokana na mshituko alioupata baada ya kuwa threaten na hao jamaa wa TRA. Majuzi nilikuwa nikimjibu mzee mwanakijiji moja ya maswali yake kuhusu Serikali iweje?
mchango wangu mkuba ulikuwa kwenye mfumo wetu wa kodi. Watanzania wengi wanakwepa kodi kwa sababu ni kubwa na zisizolipika na zenye kuua biashara. Bila kukwepa kodi biashara yako haiwezi kuwa "of going concern" lazima itakufa!Nilipendekeza viwango vya kodi vipunguzwe ili kila mmoja wetu amudu kulipa na kutokulipa kodi iwe aibu kubwa! Kodi ikiwa kubwa walipaji wanakuwa kidogo na wakwepaji wanakuwa wengi na ikiwa ndogo inakuwa kinyume chake! Mwisho napenda kutoa angalizo kuhusu hawa mabwana kodi hususan kile kitengo cha elimu kwa walipa kodi chini ya Protas Mmanda. Sidhani kama Mmanda anafanya kazi yake ipasavyo maana jamii inatakiwa ijue jinsi ya kukokotoa kodi na sio kutishiwa na mabwana kodi waonyeshe unadaiwa pesa nyingi ili uwape hongo ufutiwe au upunguziwe kodi. Pesa nyingi wanahongwa mabwana kodi,mawaziri wa fedha na wahusika wenye mamlaka ya kodi kuliko makusanyo ya mwezi ya TRA ni kwakuwa hatuna books of records tu ya hizo zinazohongwa.
 
Kevo! Unaamini kwamba maafisa wa TRA wanaweza kumhoji Mfadhili na kada mkubwa wa CCM under too much pressure? Labda huijui vema nchi hii.
Katika Tanzania hii ya sasa kutumia madaraka yako kumhoji MFADHILI wa CCM kwa undani juu ya fedha zake na kwa nini halipi kodi, unakata tiketi ya kwenda kulima kwenu kijijini. Habari ndio hiyo.
Mungu amlaze pema.

Kumbuka huko CCM kuna makundi na la mafisadi ndilo limeshika hatamu isije kuwa marehemu alikuwa mwiba kwa mafisadi wakaamua kumtumia jamaa wa TRA wamkomoe!Lolote linawezekana ikiwa Spka anatukanwa na kuzushiwa na kwenye rank Spika anaweza kuongoza nchi ikiwa wakuu wapo safarini sembuse kada na mfadhili wa CCM?
 
Hawa jamaa wa TRA ni wahuni, wao badala ya kumpa huyu ndugu huduma ya kwanza wakakimbia? Tungekuwa makini wanapaswa kujibu kesi ya kuua bila kukusudia!!
 
Hawa jamaa wa TRA ni wahuni, wao badala ya kumpa huyu ndugu huduma ya kwanza wakakimbia? Tungekuwa makini wanapaswa kujibu kesi ya kuua bila kukusudia!!
KM labda walishajua sababu ya kifo ni vitisho vyao hivyo dhamira zao chafu zikawatuma 'kulala mbele'
 
Back
Top Bottom