Mfalme Zumaridi: Kujitenga kwako na serikali kumekuponza

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,798
Nmemfahamu huyu mama anaejiita Mfalme Zumaridi miaka 2 iliyopita. Nilivyoiona ibada na tabiri zake tu nikajua huyu ni mpigaji kama ilivyo kwa wapiga wengine. Lakini kabla hatuja mkosoa au kushangaa kwanini serikali imemfungia hebu tujiulize je kwenye makanisa yetu kuko salama?

Achana na akina Mwamposa tuyachunguze haya haya makanisa yanayojiita makubwa na yasioamini sanaa mahubiri ya miujiza ya mitume na manabii. Makanisa ambayo si ya kiroho kwani yale ya Kilokole yanaitwa ni ya Kiroho japo sijui kwanini. Haya ni makanisa ya Katoliki, Moravian, Anglican, Wasabato na KKT. Hawa wanajiona wako sahihi sana.

Mimi kwa mtazamo wangu tena nikiwa mkristo niliewahi kusali kwenye haya madhehebu kuna kutu na ukakasi ambao hausemwi ktk ishu ya upigaji kwa kutumia jina la Yesu.Ukweli ni kwamba makanisa haya yanaendelea kupiga pesa watu kwa kisingizio cha kutoa kuhuma, Kivipi nitaeleza

1. Haya makanisa yanatumia jina la Yesu kufanya biashara kubwa kupitia mashule, vyuo, maduka ya madawa na mahospitali, mashamba n.k Leo hii shule, na hospitali zinazomilikiwa na Wakatoliki, KKK Wasabato n.k ndio zinazoongoza kuwa na gharama kubwa. Wanaosoma kwenye shule za Mission ni wale wenye kipato kikubwa tu na si vinginevyo. Miminilitegemea shule na hospital za dini na madhehebu ziwahudumie watoto, wazee na wajane ambao ni fukara na maskini.

Ule upendo mkuu tulioachiwa na Yesu uko wapi? Njooni wote wenye kuelemewa na mizigo nami nitawapumzisha. ( Mathayo 11:28) . Kwenye kikao chake na viongozi wa dini Mh. Rais Magufuli aliwachana live viongozi wa kanisa Katoliki na kushangaa kwann hospitali zao zina gharama kubwa sn licha ya kuwa na ubia na serikali.

Mnakumbuka elimu ya juu ilivyotaka kuharibiwa na vyuo vikuu vya Dini kabla ya serkali kuingilia kati?Ilikua pesa mbele kuangalia cheti na ufauru wa mtu. Biashara nyingi za makanisa hazipo kwa ajili ya huduma za jamii bali ni biashara km biashara zingine. Mara ngapi tumeona na kusikia kanisa likigombeana Ardhi na wananchi mpaka kupelekana mahakamani.

Kuna makanisa yanafanya biashara ya mabenki kwa kutumia sadaka je hivyo maandiko ya Biblia yameagiza?. Tunaomshangaa Zumaridi tulitakiwa kushangaa yanayoendelea kwenye makanisa yetu. Ujanja wanaoutumia ni kuwa karibu na serikali ndio maana hata mapungufu yao hayakemewi Msiwaone kusifia kila kitu cha serikali lengo ni kuwa salama.Upigaji ni ule ule sema mbinu ndo tofauti. Ukifatilia kiundani zaidi ni makanisa machache sn ambayo kweli yapo kwa ajili ya kusudi la Mungu.

Kama Zumaridi angekua karibu na chama ipo siku mngemuona apiga maombi uwanja ndege akipokea Bombadia.
 
blaza huduma bora na ya uhakika inauzwa.haitolewi bure hata siku moja.

kanisa haliwezi na wala halitokaa liweze kutoa msaada kwa masikini hawa wengi zaidi ya 20mil wanaohitaji msaada hapa tz kielimu,kiafya,na kiimani.kwa kutumia sadaka zenu 50/50.lazima liuze baadhi ya huduma kwa wachache ili litoe msaada kwa wengine.hapa mazungumzia RC.

huu umasikini wetu wa vipato duni ndio unatufanya tuone kulipa ada ya secondary milioni 1 ni gharama sana.ila kimsingi ni bei ya elimi bora ndio inaamua sio wao.

huyu zumaridi ni nani mpaka tumuache achafue imani za wengine?wenye dini hatujakubaliana naye na kwa hilo atafute kazi nyingine.
 
Naona umeyashupalia makanisa ambayo siyo ya "Kiroho" tu!! Vipi kuhusu hayo ya Kiroho unayosali wewe mtoa mada, hayajishughulishi na huo upigaji? Mfano Kanisa la Efatha, halikuwahi kuingia kwenye mgogoro wa ardhi na watu wa Rukwa? Halikuwahi kumiliki benki?

Vipi kuhusu kanisa la Gwajima, Mama Lwakatare, Kakobe, Mzee wa Upako, nk. Unayajua mapato na matumizi yao? Kuwa fair na uachane na ubaguzi wa kiimani!

Baada ya kuondokana na siasa za Ujamaa na Kujitegemea, tuliruhusu watu binafsi kuwekeza kwenye huduma za kijamii kama ujenzi wa shule, hospitali, nk. Wewe kama unaona huna uwezo wa kumpeleka mwanao St. Francis, basi mpeleke kwenye shule za magufuli za elimu bure, St. Kayumba! badala ya kulialia. Siku zote vitu vizuri vina gharama.


Unapoamua kuongelea uozo wa hizo taasisi/madhehebu ya kidini, usijitoe ufahamu na kubagua. Ongelea kwa ujumla wake, sababu hayo madhehebu yote, mpaka Bakwata! yana madhaifu na mazuri yao pia.
 
Zumarid anaonewa nililizungumza Jana ,


 
Inadhihirisha nchi hii haina uhuru wa dini wala dhamiri, sitetei ujinga wowote lakini tendo hili si la haki, na ukiona sasa serikali ina uhuru wa kuingilia mambo ya dini ipo siku hata wewe hutakuwa salama, maana watakaa watu fulani wanaojiita wakuu wa dini au wasomi wa dini, na kuizuia huduma yako. Wamwache tupambane naye kiroho na si kimwili, maana hapo ndipo kama wameuwasha moto kwa wafuasi wake.
 
Nafikiri watu hatujamuelewa mtoa maada ila mimi nimekuelewa kama ifyatavyo, mosi shule nyingi na hospitali za haya makanisa zinaendeshwa kwa sadaka ya waunini then kwe hesabu ya kwawaida tuu kungekuwa angarau na kadsicount kidogo kwa waumini hao pindi watakapohitaji huduma hizo kwa sababu nao ni moja ya wamiliki, lakini cha ajabu hakuna tofauti yoyote kwa aliye muumini na asiye muumini swali ambalo huwa najiuliza kila siku waumini tunanufaikaje na hii miradi mikubwa mikubwa jibu ni hapana.kifupi ni kwamba haya makanisa yote lao ni moja kumkamua muumini ndo maana siku hizi nimebadilisha utaraibu wa kutoa sadaka naangalia nan mwenye uhitaji nampa kimya kimya tuu na kanisani natoa kiduchu au sitoi kabisa
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom