Mfalme wa Mwisho wa Zanzibar Jamshid atua Oman kwa mara ya kwanza

Alwaz

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
6,827
10,356
Mtawala wa mwisho wa Zanzibar kwa mfumo wa ufalme ambaye alichukuliwa Uiengereza kwa madai ya kupinduliwa leo ametua nchini Oman kutokea London ikiwa ni mara yake ya mwanzo tangu azaliwe miaka 91 iliyopita.
Ametua nchini humo kama wazanzibari wengine wanavyofika kuitembelea nchi hiyo yenye historia kubwa na ukanda ya Afrika Mashariki na kati.
1600188475070.png

1600188596191.png


1600188912061.png
 
Mtawala wa mwisho wa Zanzibar kwa mfumo wa ufalme ambaye alichukuliwa Uiengereza kwa madai ya kupinduliwa leo ametua nchini Oman kutokea London ikiwa ni mara yake ya mwanzo tangu azaliwe miaka 91 iliyopita.
Ametua nchini humo kama wazanzibari wengine wanavyofika kuitembelea nchi hiyo yenye historia kubwa na ukanda ya Afrika Mashariki na kati.
View attachment 1570802
View attachment 1570805

View attachment 1570808

Huyu ndio aliyepinduliwa? Kakubali yaishe au ndio Maalimu anamuwakilisha?
 
Waliwauza Babu zetu Kama bidhaa,shame on him,
Wazungu ndio wahusika wakuu wa biashara ya utumwa unaouzungumzia ambao hasa biashara hii ilifanyika Afrika Magharibi. Kwa hapa kwetu mambo yalipowaendea kombo wakajitia kuwasingizia waarabu na kwa aibu wakajenga kanisa pale walipokuwa wakiwatesa mababu zako.
Waarabu enzi hizo walijikita kwenye biashara za viungo na vito kutoka Afrika ya kati.Wale waliokuwa wakiwabebea mizigo waliwalipa kijiji baada ya kijiji.
 
Wazanzibari mnanishangaza.mnaona fahari kutawaliwa na warabu wa Oman kuliko kujitawala wenyewe. Shame on You.
Ilikuwa ni historia tu alipofikia huyo Jamshid kwani ilikuwa watawala ni wazanzibari wenye asili tofauti.Haikuwa tatizo mpaka walipofitinishwa. Mtu mwenye asili ya Oman akitawala Zanzibar tatizo liko wapi.Mbona Tanzania imewahi kutawaliwa na maraisi wenye asili ya Kenya na Msumbiji.Marekani imetawaliwa na mtu mwenye asili ya Uiengereza.Si rahisi kuwatenganisha viumbe vya Mwenyezi Mungu kwa matakwa ya kibinadamu.
Kama kuna mtu anaona ubaya ni kutawaliwa na mtu mwenye asili ya Oman basi ana dalili ya chuki za kidini.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom