Mfalme Mzee Yusuph amethibitisha kurudi kwenye taarabu

Dini ya kweli utaijiua kwa matunda yake
Kama angekuwa anapata kitu huko alipoenda asingeona umuhimu wa kurudi kuho ambako alikuwa anakuita haramu

Kwa YESU kunalipa (watanielewa wale tu waliomchukulia kwa uzito)
 
Mungu hadhihakiwi kabisa. Ukisema umeacha ya duniani naye anakuondolea yote uliyopata duniani ili uanze na MUNGU upya.
Sasa jombaa kaona hali si hali arudi mule mule.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hata yesu alikuwa anaruhusu wanafunzi wake wakavue samaki Coz bila kufanya kazi atakula juzuu?

Kumbuka ana familia, ndugu wanaomtegemea, sasa afanye nn na kipaji ambacho akiimba anajua atapata pesa
 
Ila any way njoo utupe burudani tulikumiss taarabu ilikufa kabisa kweli we mfalme wa taarab


Hapo ulipomalizia nimepapenda!

Yeye ni mfalme wa taarabu.
Ufalme wa mungu awaachie wengine!"mumewanguu,

Sent using Redmi Y2
 
Hata yesu alikuwa anaruhusu wanafunzi wake wakavue samaki Coz bila kufanya kazi atakula juzuu?

Kumbuka ana familia, ndugu wanaomtegemea, sasa afanye nn na kipaji ambacho akiimba anajua atapata pesa
Ni sawa unayosema ila unakumbuka aliuitaje huo mziki? Hadi akakataza watu wasipige kwenye vituo vya redio na tv! Kwamba watakuwa wanazidi kumkosea Allah!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebo mnataka afe njaa afu siku ya msiba mpike pilau?

Katika dini ya kiislamu mbona hakuna maandiko yanayosema muumini akiishiwa unga ndani sheikh anapaswa kubeba majukumu ya muumini wake?

Kama waislamu wote ni ndugu na muislamu ndugu yake muislamu, kwanini undugu huo usiwe katika kusaidiana hususani kwenye maswala ya kiuchumi kama haya?

Dini yaki yenye kujenga mshikamano miongoni mwa waumini wake ilitakiwa iwe na dhana hii

Sitaki kuamini kua hamjui sababu ya jamaa kufanya sub mapema hata kabla ya kipindi cha pili hakijaanza.

It's Scars
 
Ni uamuzi wake na ana kila haki ya kufanya au kubadilisha anachofanya wakati wowote ule..., ingawa maamuzi yake ya kuacha yanaleta mapungufu kwa mashabiki wake kukosa burudani.
 
mumewanguu,
Mungu hayupo, narudia, Mungu hayupo. Ni upuuzi ulioletwa na wagni kwa maslahi ya kutupumbaza.... watutawale na kweli wameweza!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom