cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 85,628
- 137,329
Duuuuuh hii hatareeeh sana lol.
Hii ilikuwa ni promo ya mahojiano ya MARTIN CHEGERE.
Sasa haya ni mahojiano ya MARTIN CHEGERE kwenye kipindi cha MKASI kilichokuwa kinaratibiwa na SALAMA JABIR na kurushwa hewani na kituo cha televisheni cha Channel 5.
Nadhani pia, ni muda mrefu umepita tangu kipindi hiki kirushwe hewani.
Kipindi hicho, yaani mwaka 2017 - mimi sikuwepo TANZANIA , lakini sasa hivi nimepata fursa ya kutizama mahojiano yake yote.
Lakini kuna maswali ya kujiuliza kama mtazamaji na mfuatiliaji wa mambo yanayoendelea TANZANIA .
[ Sorry ] Hivi huyu SALAMA JABIR amesomea taaluma ya UHANDISHI WA HABARI au ni UJANJA UJANJA tu?
Kwa sababu tunaamini kabla ya mahojiano, kuna ile hali ya kujiridhisha na kile kitakachoenda kujadiliwa, kama kuwa na taarifa sahihi za mhusika, yaani mgeni wa kipindi.
Na kulingana na taarifa za MARTIN CHEGERE, hakuwahi kuwa mwanafunzi bora - iwe kwa shule ya msingi! Kidato cha nne! Na kidato cha sita!
Sasa sijafahamu ni kwanini huyu mtangazaji, SALAMA JABIR alipata wasaa wa kumhoji MARTIN CHEGERE kama mwanafunzi bora wa kidato cha sita, mwaka 2007. Wakati hakuna jina la mwanafunzi kama MARTIN CHEGERE kwenye orodha ya wanafunzi bora wa kidato cha sita, mwaka 2007.
Inabidi siku nyingine, hivi vituo vyetu vya habari kama vituo vya redio na televisheni viwe na utaratibu wa kufuatilia mambo kwa kina kabla ya kurusha vipindi hewani.
Maana mahojiano kama haya yanabaki milele halafu aibu na hadhi inashuka kwa mhusika, mwandishi wa habari na hata kituo cha habari kinapoteza ule uhalali na uthamani mbele ya jamii.
Hii kasumba ya kujiita mwanafunzi bora wakati sio, inapatikana sana Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam [ UDSM ].
Yaani pale MLIMANI, kila mhadhiri alifanya vizuri shule ya sekondari! Kila mhadhiri ana rekodi yake kwa shule ya sekondari! Wakati hamna kitu hicho.
Na kwa upande wa wanafunzi, hali ni ile ile! Yaani pale MLIMANI kila mwaka, wao wanaamini huwa wanachukua mwanafunzi bora kitaifa! Kila mwaka wao wanaamini pale COET kuna mwanafunzi bora kitaifa! Wakati hamna kitu hicho.
Taasisi ya elimu kama CHUO KIKUU haipaswi kuwa na majigambo na tambo kama za wanasiasa. Mafanikio na wasifu wa kitaaluma ndio vitu vinavyotakiwa kutangaza taasisi za VYUO VIKUU na sio vinginevyo.
Sasa tukiwauliza maswali - kulingana na wasifu wa kitaaluma wa mwanafunzi anayeitwa MANDELA CHARLES aliyemaliza elimu yake ya msingi mwaka 2003, elimu yake ya kidato cha nne mwaka 2007 na elimu yake ya kidato cha sita mwaka 2010. Je, kuna mwanafunzi au mhadhiri yoyote wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam [ UDSM ] anayemzidi MANDELA CHARLES? Pitia Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia au NECTA | Home kwa taarifa za ukweli na uhakika.
Huyu mwanafunzi MANDELA CHARLES, ndio aliyeongoza somo la HISABATI kwa shule ya msingi, mwaka 2003.
Huyu mwanafunzi MANDELA CHARLES, ndio aliyeongoza baadhi ya masomo na kidato cha nne kwa ujumla, mwaka 2007.
Huyu mwanafunzi MANDELA CHARLES, ndio aliyeongoza masomo ya PHYSICS na DEVELOPMENT STUDIES kwa kidato cha sita, mwaka 2010.
Huyu mwanafunzi MANDELA CHARLES alichukua shahada ya kwanza ya METALLURGY & MINERAL PROCESSING ENGINEERING pale COES, Chuo Kikuu Cha Dodoma [ UDOM ] na ndiye aliyekuwa Rais wa Serikali ya Wanafunzi katika College of Humanity & Social Sciences, CoHSS mwaka 2012/13.
Sasa kwa upande wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam [ UDSM ] na VYUO VIKUU vingine, kuna mwanafunzi mwenye wasifu wa kitaaluma kama huyu? Kama yupo tuonesheni taarifa zake!.