Mfahamu Ngamia! Mnyama mstahimilivu sana katika mazingira ya ukame

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,435
19511485_1579670962051771_3757839397810016373_n.jpg

Ngamia ni mnyama anayekula majani tuu, ni mrefu na mwenye ufanano na twiga kwa kiasi fulani, tofauti yao ni kwamba wakati twiga akiwa mrefu zaidi, ngamia ni mnene zaidi, pia twiga makazi yake ni mbugani lakini ngamia ni mnyama anayefugwa, kwa uzito hawaachani sana pia, mnyama huyu hubeba mimba kati ya miezi 12 mpaka 14 na huzaa mtoto mmoja au pacha kwa bahati sana, na mtoto huwa na kilo zipatazo 50 huku mgongoni akiwa hana Nundu kabisa.

Kwa Kimombo Ngamia anaitwa Camel, lakini neno hilo asili yake ni Latin likibeba maana ya respectively, ukiondoa jina hilo pia anafahamika kwa jina la Meli ya jangwani, ni mnyama mwenye faida lukuki sana, kwanza maziwa yake hutumiwa na binadamu, mnyama yake pia, wakati vinyweleo vyake na ngozi hutumika kuzalisha bidhaa kadha wa kadha, lakini kama haitoshi Ngamia pia ni usafiri, kwa ambao wamefika Sudan au Misri jambo hili wala halitawashangaza.

Maisha yao ni kati ya miaka 40 mpaka 50, kimsingi ngamia wapo wa aina Mbili, mwenye nundu moja ndio maarufu sana hapa Africa, wakati aina ya pili ambao hubeba nundu mbili na vinyweleo vingi wakipatikana huko Asia, waone na miili yao vile vile na mwendo wao wa taratibu lakini ukitaka kumuharakisha yawezekana pia, akishika njia haswaa hukimbia km 40 na zaidi kwa saa moja tuu.

Kwa urefu huwa na futi 6 mpaka 7, na uzito wao ukicheza kati ya kg 300 mpaka 1000 endapo matunzo mazuri atapewa, mtoto wa ngamia hupevuka anapotimiza miaka 7, Ngamia jike ni kiumbe ambaye kwa mapozi na malingo amebobea, humzungusha sana dume pindi anapotaka wastarehe, mpaka jike akubali na kujilaza chini dume hutumia mbinu nyingi sana, ikiwa ni pamoja na kumlamba, kumchezea shingo, kumkuna na anapokuwa mkaidi dume huchukia na kumuuma kabisa, hapo jike ndio kidogo atamfikiria fikiria kuwa jamaaa alipofikia sasa hakuna namna ! Na apewe tuu huduma !

Na kwa usumbufu huo jike akipitisha tuu jambo hilo, Dume hufidia akiingia hatoki mpaka afanye ejaculation zaidi ya mara tatu, ndipo aanze kutafuta pumzi ya round nyingine, hapo ndio atatoka huku jike wake akimkwepeshea macho kwa aibu ya usumbufu alioufanya !

Ukiondoa hayo Ngamia ni mstahimilivu sana katika mazingira ya ukame, anaweza akadumu kwa muda mrefu sana pasina ya kula wala kunywa, Na siri ya kuwa hivyo ni ile Nundu aliyonayo pale juu, huweza kubeba kiasi kingi cha wanga kinachomsaidia kujimudu anapokuwa katika mazingira kama hayo, hunywa maji zaidi ya lita 110 na si mwepesi kupata kiu .

SIFA ZAKE ZA UPEKEE.

1. Ni mnyama msikivu, mtulivu na mwenye nidhamu.

2. Ni mnyama mtii.
Huko uarabuni nasikia akisomea dua tuu analala tayari kwa kuchinjwa.

3.ukiwatumia kama usafiri we muharakishe jike tuu, dume atafanya haraka huwa hapendi kushindwa kwa jike.

4.madume huwa wakubwa na warefu kidogo kwa majike.

5. Ni mnyama mwenye heshima yake Uarabuni, kama ilivyo twiga Tanzania au Kangaroo kwa Australia.

6.hupendelea kuishi kifamilia

7. Ukiwa naye jangwani na kukiwa na uhaba wa maji anaweza kukuongoza mpaka sehemu mtayopata maji.

8. Ngamia jike hutoa maziwa kuanzia Lita 15 na zaidi.

8. Ni mnyama mpenda amani na rafiki sana kwa binadamu.

Wakati hapa Tanzania wajasiriamali wakihamasishwa kufuga kuku kwa ajili ya chakula na biashara, huko Sudan mwaka Jana walikuwa wanafanya campaign ya kufuga ngamia kwa sababu kama za sisi kufuga kuku.

Hata hivyo imefahamika kwamba wanyama ambao huwa hawapatikani katika jamii fulani, kitoweo chao ukipeleka katika jamii hiyo watu wake hupata tabu sana katika matumizi, sasa nakuacha na swali je waweza kunywa maziwa ya ngamia na kuila nyama yake !



Wasalaam !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom