Mfahamu Mgunduzi wa kampuni ya Apple Steve Jobs

plan z

JF-Expert Member
Jun 10, 2019
1,381
1,414
Steve Jobs.jpg

Steve Jobs ni mfanyabiashara, mwekezaji, na mgunduzi wa kampuni kubwa dunia ya APPLE na alizaliwa mnamo February 24, 1955 huko San Francisco, California nchini Marekani ambapo "aliasiliwa"( ADOPTED) na Clara and Paul Jobs kipindi ambacho anazaliwa na hii ilitokana na wazazi wake halisi ambao ni Joanne Schieble na Abdulfattah Jandali kushindwa kuoana sababu ya mvutano uliokuwepo wa kifamilia yaani kati ya familia ya baba yake na Mama yake. Hivyo Steven alilelewa na wazazi hao wakufikia ambao hawakuwa na kipato kikubwa (a lower-middle-class couple)

Baba yake yaani Paul Jobs alikua akifanya kazi katika karakana ya familia ambapo ilikua ikihusika na mambo ya kielekroniki na hapo Steven ndipo alipokua akifanya kazi na baba yake kwa kipindi chote akiwa mdogo. Huko ndipo Steven alipoanza kuvutiwa na maswala ya Kielectroniki.

Steven alipokua alipelekwa shule na alipofika grade ya nne Steven alipewa mtihani kwa ajili ya kujiunga na high-school na alifanikiwa kupasi na akachagua kusoma katika chuo chaReed ambacho kilikua cha gharama mno kwa wazazi wake hao wakufikia kushindwa kumudu gharama za ada. Hivyo wazazi wake hao waliamua kua Steven asome kwa mhula mmoja tuu kisha aache masomo.

Baada ya kuacha masomo chuoni hapo, Steven alibaki chuoni hapo ili ajifunze baadhi vitu ambavyo alikua akivutiwa navyo na alikua akilala sakafuni mwa vyumba vya rafiki zake chuoni hapo. Calligraphy ndilo darasa alilokuwa akivutiwa nalo.

Mnamo mwaka 1970 Steven alikutana na rafiki yake Steve Wozniak ambaye alikua na miaka mitano zaidi yake na pia kukutana na Bob Dylan ambapo wote hao walikua wakivutiwa na electronics na ndipo walipoamua kufanya kazi katika karakana ya electronics nyumbani kwa kina Steven na hapo ndipo walipoamua kutengeneza kompyuta ya Apple I na Apple II. Wozniak alikuwa akijihusisha na maswala ya kielektroniki ilhali Steven yeye alikua akijihusisha na mambo ya design tofauti tofauti.

LOGO/NEMBO ya kwanza iliyptumika ilikua ni picha ya mwanasayansi maarufu duniani aliefahamika kwa jina la Sir Isaac Newton akiwa amekaa chini ya mti wa Apple. Baadae ikafuata nembo ya Upinde wa mvua (rainbow) kisha Apple ambalo lilikua limeng'atwa kwa pembeni na hadi hapo Nembo hiyo ikawa ikitumika na kubadilishwa rangi tu.

Mnamo mwanzoni mwa mika ya 1980, Steven alitembelea kituo cha utafiti cha computer kilichokua kikiitwa Xerox PARC na ikumbukwe kabla ya hapo aligundua computer aina ya Lisa ambapo ilikua ni toleo lingine la computer ya Apple. Na jina Lisa lilitokana na jina la mtoto wa kike wa Ex-girlfriend wake ambaye walikua wapenzi kipindi wakiwa high school na mtoto huyo watu wengi walikua wakiamini ni mtoto wa Steven na hata hivyo Steven alikataa kulipa fedha kwa ajiili ya kumtunza mtoto huyo licha ya kuwa na mamilioni ya fedha alizotengeneza kupitia mauzo ya Apple, hivyo Steven aliamua kuiita computer hiyo jina la Lisa.

Alipokuwa Xerox PARC, alijenga hisia kubwa mno kwani wanasayansi waliokua katika kituo hicho,walikua wamewekeza katika namba kubwa ya teknolojia ambazo zinekuja kuwa na faida kipindi cha miongo iliyokua mbele yao (jambo ambalo tunaona matunda yake kwa sasa) ikiwa ni pamoja na graphical user interface (GUI) and the mouse, Ethernet, laser printing and object oriented programming.
Try to check full History here, ilikuwaje Apple ikawa maarufu? Iphone zilianzaje?



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom