Duduvwili
JF-Expert Member
- Jan 31, 2015
- 3,884
- 3,805
Nafikiri labda ni vile Idara TZ ilihusika ku mlink kum introduce PKAcha kuandika vitu usivyokua na uhakika navyo jomba na kama ni hio documentary ya Kabarebe iliyoko youtube nimeshaiona zaidi ya mara 4 mkuu.
Kagame alisema kama Congo itaendelea kuwapa hifadhi waasi wa serikali iliyopinduliwa/interahamwe ataivuruga Congo na hio ni 1995 na akasema wazi wazi kabisa kuivuruga Congo ni rahisi tu kwa ku train waasi na kuwapa support na ukitaka nitakuwekea hapa gazeti la US likiripoti hio habari.
Na Kagame akatoka hapo akaenda ziara US akawaeleza khs hatari ya inayomkabili kwawaasi kuhifadhiwa Congo na kupewa Support na serikali ya Mobutu,serikali ya US ikampuuza ikaona ka nchi kenyewe kadogo na ka kidwanzi kametoka kuchinjana kataiwezaje kijeshi nchi kama Congo ambayo ni kubwa mara 90 ya ka Rwanda ukitaka pia ntakuwekea hapa washngton post ikiripoti ziara hio ya PK na alichokisema PK.
Khs Kabila senior usichokijua ni kua Kabila alishajaribu kuipindua serikali ya Congo tangu 1967 kupitia chama chake cha People's Revolution Party na akashindwa miaka yote hio lkn kupitia ADFL iliyotengenezwa na wakina Kagame ndipo aliweza kushika nchi(1st congo war),Kabila alikua anaishi Dar so ni kweli M7 alim-link Kabila(nae M7 aliunganishwa na Kabila kupitia usalama wa Taifa wa Tz) kwa kina PK na wakina PK walihitaji mtu ambae wananchi wa Congo watam support kwa kuona ni Mkongo mwenzao kuliko kuona wanyamlenge ndio waliokamata nchi ya Congo.
So kusema mchongo wa kuivuruga Congo ulipangwa Tz sio kweli hata kwa 1%.