Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,462
- 154,332
- Thread starter
- #441
Wimbo wa mchakamchakaEti mzee mwanjisi alimfanya best yake mtu aliepigwa kiwanja chake we sema ulilipia x 2
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wimbo wa mchakamchakaEti mzee mwanjisi alimfanya best yake mtu aliepigwa kiwanja chake we sema ulilipia x 2
Mimi naona ni mda sana zaidi ya miaka kumi,maana nna kachalii nilizaaga huko kapo darasa la tano nowMbona naona kama juzi tu?
Mimi naona ni mda sana zaidi ya miaka kumi,maana nna kachalii nilizaaga huko kapo darasa la tano nowMbona naona kama juzi tu?
Umewahi kuyasikia majina haya? Chiba, Kajole, Mfike, Ngwisa, Butwa, Yesu, Shetani, Nico Mkinga, Chipweta, Gerald Hongoli, Magonza, Kambosonic, Murad Mbewa, Shommy Bigga, Gill Biz, Adili, Isanga Family, Mkavenga, Veda kala Veda?Bujibuji kumbe gwakukaja wewe aiseee nimecheka kinouma amamoma aiseee mara iposolo
Bato na David watoto wa Mwanjisi, wapo?Mzee wa mwanjisi amefariki mwaka juzi kwa tatizo la mapafu, mpaka uzeeni mwake alikuwa anapiga sana sigara..
Nilimfahamu kwasababu kuna maza aliniuzia kiwanja, kumbe kiwanja sio chake ni cha mwanjisi, basi baada ya kukutana na Mwanjisi akawa mshikaji wangu kwa story zake ..
WtF?Mbeyaaa... haikuishiwa matukio miaka ya 80..
Kuna mtu akijiita mungumtu akiishi pale mafiati... kama sikosei akiitwa Mwalwago ikisemekana alikuwa na udugu na Daudi Mwakawago
Hiyo style ya mazishi inaitwa ASWILE (GODWIN) KOMA KUMWANYA
😀😀 gwee mkamu kangi ikufwana gwa ngonde uju bhule?
Kabila langu.Natafuta kabila ambalo halina wachawi na watu wenye nguvu za ajabu
Ndagha Mwaisa kwa stori nzuri!Ukifika Mbeya Mjini kuna eneo linaitwa Forest Mpya.
Siku za nyuma eneo hilo lilijulikana tu kama Forest kwa kuwa kulikuwa na msitu mkubwa sana wa miti ya milingoti ambayo Kama huijui ni miti inayozalisha nguzo za umeme na za TTCL.
Huu msitu ndio Jaili aliutumia kuchinja watu ambao alikuwa akiwapiga kwanza na nyundo, Kisha huwapakia kwenye gari na kwenda kuwachinja Forest.
Mama yake Jaili alikuwa ni mchawi sana na alikufa na kufufuka Mara tatu kwenye uhai wake. Na alipokuja Mara ya nne haraka haraka wakaenda kumzika kwenye makaburi ya Nonde.
Mara ya kwanza alifia katika Hospital ya Rufaa Mbeya, enzi hizo ikiitwa Gredi Wani. Alipokufa wakampeleka mortuary, sasa Kuna watu walikuwa na maiti ya ndugu yao kafa kwa ajali, wakati mhudumu anavutavuta mafriji, mama yake Jaili akanyanyuka, na kutembea kwa miguu hadi kwa mwanae mitaa ya Ghana.
Mara ya pili alifia nyumbani kwa mwanae, na akapelekwa mortuary ambako alikaa, na siku walipoenda kumuandaa kwa ajili ya maziko, aliamka na kurudi kuwa hai, watu wakatoka nduki vibaya Sana.
Baada ya siku chache huyu Bibi mwenye mauzauza ambayo USER=98741]Mshana Jr[/USER] hajawahi kuyaona maishani mwake, alifariki Tena, ila Safari hii nimesahau alifufukaje.
Sasa alipokuja kufa Mara ya nne, hawakumchelewesha, Wananzengo fasta wakakimbilia kwenye makaburi ya Nonde, wakachimba kaburi refu sana, ngazi ya zimamoto inazama, wakaandaa na trip ya mawe, jiwe la chuma sio mamoma.
Maiti fasta ikawekwa kwenye jeneza lililotengenezwa kwa mti wa Mkambokambo, ile miti ambayo zamani wakati wa Christmas ilikuwa inauzwa Namanga na Kariakoo Cyprus tree.
Fasta wakaitwa Mchungaji Mwamlima na Mwinjilisti Mwaibofu wa wa kanisa la Moravian. Mwili wa marehemu hakuingizwa kanisani kwa ajili ya kufanyiwa ibada ya mwisho. Moja kwa moja ikapelekwa Nonde, Mwamimwa akaendesha ibada huko. Ibada ilikuwa fupi Sana kuokoa muda ili asifufuke Tena.
Jeneza likashushwa huko kaburini, kwa namna ya kuvurumushwa.
Lile tipper ambalo lilikuwa na trip ya mawe, likabenua mawe yote Ndani ya kaburi.
Baada ya hapo vijana wakapiga posolo /chepe za kutosha kumfukia marehemu.
Huu msiba ulisisimua sana, watu wa Ghana, Mbata, Majengo, Nonde, Mabatini na hata Mwanjelwa walifika kuona mazishi hayo ya kigagula. Huyu Mama ndiye aliyekuwa anafanya mwanawe Jaili asikamatwe, na hata akikamatwa alikuwa anatoroka jela. Jaili alikufa miaka ya 1998/99 na kuzikwa Nonde.
Jaili ameishi maisha ya uzee kwa mateso makubwa, alikuwa anashinda Uhindini kwa Wahindi akiwaomba hela, wakimnyima anatishia kutoa Siri zao.
Mtoto wake aitwaye Manyenye alikuwa tishio Sana, naye alikufa siku chache baada ya kifo Cha baba Yake.
Kwahiyo mzee mwanjisi alifurahi kiwanja chake kuuzwà bila idhini yake hili tango haliliki.
Bato na David watoto wa Mwanjisi, wapo?
Asante kwa kunijuza. Baba yao alikuwa anawavutisha bangi tangu wakiwa na miaka mitanoDavid ni mwanasheria na ndiye aliyekuwa anampambania baba yake kwenye hiyo kesi yetu, Bato sijabahatika kumjua..
Zilikuwa Imani tu,huu mto kuna sehemu nime uruka Sana.Karibu na chuo cha magereza kule.Tulikuwa tunaenda kufanya mazoezi.Ni kama wanavyosema kwenye bwawa la "kisiba" kule Tukuyu njia ya kwenda Lwanga.Alikuwa ni Mmanyafu, kabila dogo sana linalopatikana kwenye mpaka wa wilaya ya Rungwe na Ileje Kijiji Cha Ikuti.
Kijijini hapo unapita mto Songwe/Kiwira. Kijiji chote ni wachawi sana na mto huu mkubwa ukifika kijijini hapo, huwa mdogo kabisa, kiasi cha kuweza kuruka kwa miguu.
Ukiruka mto hupanuka na wewe kudumbukia Ndani na kupoteza maisha. Kitendo hicho huitwa na wenyeji ATINYELITE BUKOMU kwamba hajaruka vizuri.
Nyinyi ndio mlikuwa mnaenda Kula "dawa" Kwa "Chadog"Daaah Lumbila.
Mkuu umenikumbusha hiyo mitaa back then wakati nasoma Iyunga ndo tulikuwa tunaenda kufata mademu hiyo mitaa .Pamoja nakule juu Ikuti.
Hahahaha Mwanjisi hakuwa mchawi bali mbabe alikuwa anafunga "kilemba".Kuna route moja aliianzisha, Airport - Sokomatola,basi akikuona unapeleka hiace njia hiyo,ujue ni vita.Na gari yake ikikamatwa tu,alikuwa anabeba familia yake anaipeleka central police waihudumie wao polisi.Kuna mzee mmoja naye alikuwa anaitwa Mwanjisi alifanya biashara ya Hiace, sifa ya gari ya ni ilikuwa imechoka sana naye alikuwa na stori za mauza uza. Hivi bado yu hai?
Sent using Jamii Forums mobile app