Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
Meya wa jiji la moscow Yuri Luzhkov ametimuliwa leo baada ya kuwa meya wa moscow kwa miaka 18.Rais Medvedev alisaini barua ya kumfukuza meya huyo siku chache tu baada ya meya huyo kusema kuwa hatan'goka madarakani hata kwa mpini.Medvedev ambaye yuko safarini nchini china alinukuliwa akisema kuwa amemfukuza meya huyo kutokana na wananchi na ikulu kutokuwa na imani naye.Meya huyo ambaye mkewe ni billionea na anamiliki makampuni ya ujenzi anatuhumi kuwa chanzo cha mkewe kuwa bilionea,pia meya huyo ameonekana waziwazi kupingana na ikulu ya moscow(kremlin), na alionekana kupata upinzani kutoka kwa wananchi baada ya yeye kwenda mapumzikoni mwezi wa nane ilihali moscow ilikuwa imetandwa na wingu zito na kuungua kwa misitu inayoizunguka.
Baada ya meya huyo kufukuzwa aliandika barua ya kustaafu kwenye chama kikubwa chenye nguvu cha Putin(idinaya rasia) hali ambayo imeleta wasiwasi mkubwa kutokana na kwamba meya huyo ana wafuasi wengi.
Source:jamiiforums.com
Baada ya meya huyo kufukuzwa aliandika barua ya kustaafu kwenye chama kikubwa chenye nguvu cha Putin(idinaya rasia) hali ambayo imeleta wasiwasi mkubwa kutokana na kwamba meya huyo ana wafuasi wengi.
Source:jamiiforums.com