Meya wa Kinondoni afanya ufisadi

Mwafrika wa Kike

JF-Expert Member
Jul 5, 2007
5,185
56
Naona gazeti la fisadi Rostam Azizi limeanza kuanika ufisadi wa mafisadi watoto. Ufisadi huanza kidogo kidogo na baadaye kufikia hatua ya kuiba mabilioni na kuanza kuua watu.

Masahihisho tu kwa nyie waandishi, hakuna kitu kinaitwa jiji la Florida hapa Marekani.

na masyaga matinyi

MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Kinondoni Alhaji Salum Londa, anatuhumiwa kughushi nyaraka ili kumuwezesha binti yake kwenda Marekani, Julai mwaka jana.

Uchunguzi uliofanywa na MTANZANIA umebaini kuwa, Londa alitumia

vibaya madaraka yake kumjumuisha Amina Salehe Londa, katika orodha ya madiwani vijana, ili aweze kwenda Marekani.

Madiwani vijana kutoka Manispaa ya Kinondoni walikuwa wamealikwa nchini jijini Florida, Marekani, mwezi Julai mwaka jana na Taasisi ya Sister City International.

Lakini jitihada za Londa kumpeleka mtoto wake, ziligonga ukuta, baada ya Ubalozi wa Marekani kumnyima kibali cha kuingia nchini humo (VISA), tarehe 11 ya mwezi huo.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa, kabla ya kufanyika kwa safari hiyo, mtoto huyo tayari alikuwa ameshalipwa fedha za safari kiasi cha Sh milioni 6, na manispaa hiyo.

Katika orodha ya madiwani vijana walioteuliwa kutoka kata 27 za Manispaa ya Kinondoni Julai 2005, ambapo kila kata ilitoa wawili, katika Kata ya Kawe ambayo Londa ni diwani wake, nafasi zote mbili zilichukuliwa na watoto wake.

Watoto hao ni Haji Londa, na Amina Salehe, ambaye katika orodha hiyo ameandikishwa kama Amina Abdallah. Majina ya Meya huyo ni Salum Saleh Londa.

Katika safari hiyo ambayo Alhaji Londa naye alikwenda Marekani, pia anatuhumiwa kurejea nchini na kompyuta ndongo (laptop) 20, na kuziuza kwa manispaa.

Mstahiki Meya huyo aliuza kompyuta hizo kwa Sh milioni 3 kila moja, bei ambayo inalalamikiwa kuwa ni kubwa, kulinganisha na bei ya soko.

Mwanzoni mwa wiki hii, madiwani katika manispaa hiyo walielezea kutokuwa na imani na kiongozi huyo kutokana na kutuhumiwa kwa vitendo mbali mbali vya ufisadi katika utekelezaji wa majukumu yake.

Walisema kuwa kuna mpasuko mkubwa miongoni mwao, kiasi cha kukwamisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Madiwani hao pia wanamtuhumu Londa kwa kujaribu kuupa sura ya udini mgogoro wa kiwanja namba 965, kilichopo Kata ya Kawe, katika manispaa hiyo.

Katika sakata hilo la kiwanja, Londa ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kawe, anatuhumiwa kukiuka Sheria ya Ardhi Mijini ya mwaka 1999, kifungu namba 4.

Kwa mujibu wa sheria hiyo, mwekezaji yeyote kabla ya kumilikishwa eneo, anapaswa kulipa fidia kwa mujibu wa bei ya soko kwa wakati husika.

Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanyika, kiwanja hicho chenye ukubwa wa mita za mraba 36,667, kilipaswa kulipiwa fedha zisizopungua Sh milioni 200, lakini malipo hayo hayajawahi kufanyika.

Kiwanja hicho kwa sasa kinamilikiwa na Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Masjid Qiblatain, na tayari kimezungushiwa ukuta, huku ujenzi wa msikiti, shule, na majengo mengine ukiendelea.

Kiwanja hicho kinapakana na kingine kilichouzwa na manispaa hiyo mwaka juzi, na kuzua tafrani kubwa kati ya wakazi wa eneo hilo, na mwekezaji aliyekusudia kujenga shule.

Katika sakata hilo la awali lililohusisha wakazi wa eneo hilo, ambapo walifikia hatua ya kuvunja ukuta uliokuwa ukijengwa na mwekezaji aliyeuziwa eneo, Meya Londa, alilaumiwa kuhusika na uuzwaji wa kiwanja hicho, ambacho ni mali ya manispaa.

Wakizungumza zaidi, wadiwani hao walisema imefikia hatua hata maamuzi yanayopitishwa na Baraza la Madiwani hayatekelezwi, yakiwamo malipo ya zabuni mbali mbali, ambayo yamekuwa yakizidishwa kwa malengo ya ubadhirifu wa fedha za walipa kodi.

Source Mtanzania;


http://www.newhabari.com/mtanzania/habari.php?id=2238&section=kitaifa
 
Kama kweli huyu ni kiongozi mwadilifu, angejiuzulu mara moja. Sababu ziko nyingi lakini kubwa zaidi ni kutumia vibaya madaraka yake kwa sababu binafsi (kuuza viwanja, kuwafagilia wanawe kwenda Marekani kwa fedha za serikali pasipo na ustahili, kutumia safari ya kiserikali kibiashara). Yaani ni kweli, ufisadi huanza kidogo kidogo kama hivi na Londa afanzwe fundisho!!
 
Hii inchi inanuka rushwa in all departments!

Inaelekew Watz sasa wanaanza kuzoea wala rushwa!

Kwa nini huyu jamaa asijiuzulu?
 
Kama kweli huyu ni kiongozi mwadilifu, angejiuzulu mara moja. Sababu ziko nyingi lakini kubwa zaidi ni kutumia vibaya madaraka yake kwa sababu binafsi (kuuza viwanja, kuwafagilia wanawe kwenda Marekani kwa fedha za serikali pasipo na ustahili, kutumia safari ya kiserikali kibiashara). Yaani ni kweli, ufisadi huanza kidogo kidogo kama hivi na Londa afanzwe fundisho!!

Wewe kama Kikwete mwenyewe anafanya wizi na ufisadi hadharani basi unategemea mameya wake wafanye nini!
 
PCCB wanasubiri nini? kupewa amri na Kikwete ya kuunda tume ya uchunguzi? TZ inachosha kwa kweli!
 
Meya anachaguliwa na wananchi. Huyo sio Meya wa Kikwete ni Meya wa wakazi wa Kinondoni.

Richard alishinda big brother na ccm wakamuandalia maandamano na kusema ni matokeo ya "uongozi bora wa ccm" the same thing kwa meya wa kinondoni kuwa meya wa ccm na meya wa Kikwete at the same time - LOGIC 101
 
Richard alishinda big brother na ccm wakamuandalia maandamano na kusema ni matokeo ya "uongozi bora wa ccm" the same thing kwa meya wa kinondoni kuwa meya wa ccm na meya wa Kikwete at the same time - LOGIC 101

Aunt hivi watu huko nyumbani uwa wanakula kweli ukiwa umekasirika?
 
This is the power of ICT... kila aliyekula atajulikana tu... muda muafaka ukifika
 
Aunt hivi watu huko nyumbani uwa wanakula kweli ukiwa umekasirika?

Mmarekani mtarajiwa. Naombea hukumaanisha nilivyokuelewa. Kama ni hivyo kwa mwendo huu utaishia lupango huko unakoishi. Naomba naomba unifahamishe hasa ulikuwa na maana gani au umwombe msamaha huyu dada yetu. Kama ni mimi mwenye mawazo mabaya naomba unisamehe.
 
Jamani hapa ni watu wako kazini . Ia Londa ana historia kubwa ya ufisadi , udini na uchafu kibao. Londa nilimuona na wana CCM wenzake pale kwenye msiba wa Marehemu Chifupa huwezi kuamini . Nilishangaa msiba ulikiwa kama kampeni. Londa ni mchafu sana sana .Lakini nani wa kumweleza ? CCM ndiyo hivyo tulivyo .Kujuana na tunajuana bwana na kubebana .
 
Jamani hapa ni watu wako kazini . Ia Londa ana historia kubwa ya ufisadi , udini na uchafu kibao. Londa nilimuona na wana CCM wenzake pale kwenye msiba wa Marehemu Chifupa huwezi kuamini . Nilishangaa msiba ulikiwa kama kampeni. Londa ni mchafu sana sana .Lakini nani wa kumweleza ? CCM ndiyo hivyo tulivyo .Kujuana na tunajuana bwana na kubebana .


Ina wenyewe hiyo......
 
Swala la Londa lina utata kiasi cha mwezi mmoja gazeti hili hili la Mtanzania liliandika habari mbaya ya Londa kuwa kawapa kiwanja Qiblatain.

wakati huo huo Londa ana kesi ya muda mrefu kashitakiwa na waislam kuwa kawadhulumu kiwanja, jengo na msikiti wa waislam na kukifanya kuwa soko na stendi ya bus.wasilam walikwenda hadi kwa Ritta Mlaki kupeleka kilio chao. vipi haya hayasemwi?

kiwanja hicho kiko TEGETA. kwa waislam wanamshutumu kwa kuwadhulumu mali zao na MTanzania linamshutumu kuwa mdini.hapa kuna vita ya kisiasa wilaya ya Kinondoni ambako kuna Mhaya anatumia mtandao wa Kihaya kumshambulia LONDA na gazeti la Mtanzania lina Ukagera.

cha ajabu makala zote amekuwa akiandikwa kama ALHAJI LONDA kwenye issue hizi mbili.
 
Swala la Londa lina utata kiasi cha mwezi mmoja gazeti hili hili la Mtanzania liliandika habari mbaya ya Londa kuwa kawapa kiwanja Qiblatain.

wakati huo huo Londa ana kesi ya muda mrefu kashitakiwa na waislam kuwa kawadhulumu kiwanja, jengo na msikiti wa waislam na kukifanya kuwa soko na stendi ya bus.wasilam walikwenda hadi kwa Ritta Mlaki kupeleka kilio chao. vipi haya hayasemwi?

kiwanja hicho kiko TEGETA. kwa waislam wanamshutumu kwa kuwadhulumu mali zao na MTanzania linamshutumu kuwa mdini.hapa kuna vita ya kisiasa wilaya ya Kinondoni ambako kuna Mhaya anatumia mtandao wa Kihaya kumshambulia LONDA na gazeti la Mtanzania lina Ukagera.

cha ajabu makala zote amekuwa akiandikwa kama ALHAJI LONDA kwenye issue hizi mbili.


Mtalii:

Waislam na watanzania wengine mmeliwa. Na hayo mambo ya dini ni huku mitaani lakin mafisadi hawana dini na wanacheza show tu. Hii ni story:

Londa kachaguliwa diwani mpaka Meya na hakuwa na hakuwepo kwenye mzunguko wa mafisadi lakini na yeye akataka kunyonya. Kujitafutia ujiko, wanaCCM wakamwalika Ben Mkapa huko kwenye mkutano wa wanaCCM Kinondoni. Kwenye mkutano akamwambia rais na mwenyekiti wa CCM kuwa leo tunakuletea zawadi kutoka chama cha upinzani. Zawadi alikuwa Dr. Masumbuko Lamwai.

Mzee Mkapa akapata wazo zuri la kumtumia Mkereketwa Alhaji. Wakati wa uchaguzi Alhaji akapewa kazi na Ben. Kazi yenyewe ni lazima Mama Mlaki ashinde uchaguzi. Mama akashinda na chati ya Alhaji ikapanda na mirija ya kunyonya akapewa tena kutoka Ikulu.

Mnaolalamika na kwenda kumshitaki kwa mama Mlaki mnazunguka tu. Watu wale ni kundi moja.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom