kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 235
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mwanza, Francis Mkambenga, alisema hali ilikuwa tete na kwamba operesheni hiyo ilikuwa imepangwa kwa ajili ya kuwaondoa machinga katika eneo hilo la msikiti na shule eneo la Makoroboi.
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Mkambenga, alisema operesheni hiyo ilikuwa na baraka zote za jiji huku Meya wa jiji hilo, Josephat Manyerere, alisema hana taarifa kutoka ofisi ya mkurugenzi.
Mkurugenzi ana dharau fulani, pengine ana nia ya kunikomoa mimi na chama changu cha CHADEMA, alisema Manyerere.
Manyerere alisema wakati yeye akifichwa taarifa za kuwapo kwa operesheni hiyo, taarifa hizo zilipelekwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa.
Aliongeza kuwa ofisi za wabunge wa Jiji la Mwanza, Ilemela na Nyamagana nazo zilinyimwa taarifa hizo kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji.
Ninalaani operesheni hii haramu, maana imefanywa bila kujulishwa ofisi yangu ya meya. Hapa inaonekana mkurugenzi anataka kunikomoa mimi kama meya na chama changu cha CHADEMA tunaoongoza jiji hili. Hii ni dharau inayofanywa na ofisi ya mkurugenzi kuninyima taarifa muhimu kama hizi, alisema Meya Manyerere. Meya huyo aliwataja watu waliojeruhiwa na kulazwa katika hospitali za Sekou Toure na Bugando kuwa ni Omari Abdallah, Juma Machumu, Calvin Jeremiah, Brayen Pastori, Kulwa John (amepigwa risasi kichwani), Medard Benard na Dotto Thomas, na kwamba majeruhi wawili kati ya hao wamelazwa chumba cha uangalizi maalumu (ICU), katika Hospitali ya Bugando (BMC).
Source. Tanzania Daima
Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza, Mkambenga, alisema operesheni hiyo ilikuwa na baraka zote za jiji huku Meya wa jiji hilo, Josephat Manyerere, alisema hana taarifa kutoka ofisi ya mkurugenzi.
Mkurugenzi ana dharau fulani, pengine ana nia ya kunikomoa mimi na chama changu cha CHADEMA, alisema Manyerere.
Manyerere alisema wakati yeye akifichwa taarifa za kuwapo kwa operesheni hiyo, taarifa hizo zilipelekwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa.
Aliongeza kuwa ofisi za wabunge wa Jiji la Mwanza, Ilemela na Nyamagana nazo zilinyimwa taarifa hizo kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji.
Ninalaani operesheni hii haramu, maana imefanywa bila kujulishwa ofisi yangu ya meya. Hapa inaonekana mkurugenzi anataka kunikomoa mimi kama meya na chama changu cha CHADEMA tunaoongoza jiji hili. Hii ni dharau inayofanywa na ofisi ya mkurugenzi kuninyima taarifa muhimu kama hizi, alisema Meya Manyerere. Meya huyo aliwataja watu waliojeruhiwa na kulazwa katika hospitali za Sekou Toure na Bugando kuwa ni Omari Abdallah, Juma Machumu, Calvin Jeremiah, Brayen Pastori, Kulwa John (amepigwa risasi kichwani), Medard Benard na Dotto Thomas, na kwamba majeruhi wawili kati ya hao wamelazwa chumba cha uangalizi maalumu (ICU), katika Hospitali ya Bugando (BMC).
Source. Tanzania Daima