Meya wa jiji la mbeya ATTANAS KAPUNGA akalia kuti kavu.

ferre.g

JF-Expert Member
Mar 3, 2013
2,215
327
Ndugu zangu habari za mwaka mpya.

Ni wazi shahiri kuwa meya huyu kauanza mwaka vibaya sana.

Ni ktk kikao cha WDC ambacho huwa cha wazi ilimbidi avunje kikao ili kuruhusu wananchi kutolewa nje.

Agenda ilokuwa inafuatia ni ya matumizi ya tshs 95 ml alizotumia kwenda China kama nauli ilihali nauli halisi ni tshs 3.ml go and return.

Ni madiwani wa chadema wapatao 16 walouwasha moto hadi kufikia na wa ccm kuungana pamoja kuwa arejeshe haraka pesa hizo.

Meya huyu wa STD 7 aligoma akidai zilitumika zote kwenye matumizi ya maradhi.... hapa akaamsha hasira za madiwani walioamka kwa pamoja na kumwagia maji mwili mzima.

Alikuwa ni Abbas kandoro alie mnusuru na kipogo kwa kushirikiana na na wana usalama hawa walituliza munkali ya madiwani.

Kandoro amemtaka meya huyo arejeshe fedha hizo kabla madiwani wa cdm hawajaenda kuutangazia umma na kuandamana jambo ambalo litashusha hadhi yake make chama chake kutokomea.

Nawasilisha

NB; Haya ni baadhi tu mengine nayaficha.
 
Nyongeza madiwani wanaandaa mkakati wa kumng'oa ktk kiti hicho.

Tungoje ntawajuza zaidi.
 
na bado makapuni ya pepsi cocacola tbl na mengineyo ya iyunga viwandani yanatoa kodi ya jiji milion 40 kila baada ya miezi mitatu na hawasemi zinatumikaje ni zaidi ya bilion moja kwa mwaka.
 
Huyu Meya wa Mbeya ni CCM, hivyo anadhani hicho ni kitu kidogo tu kulingana na wenzake wanavyokwiba hii nchi, CDM wekeni kidedea mpaka apigwe chini
 
hiyo ndio dawa yao wamwagiwe tindikali wafie mbali, maana wameshao pesa za walalao ni kama shamba la bibi wa kambo, ml 95/ml 3 hainiingii akilini, nanikampitishia pesa zote hizo? na huwa wanazichota wapi?.ameniharibia new year yangu, najuta kwaninimefungua hii kitu.
 
hiyo ndio dawa yao wamwagiwe tindikali wafie mbali, maana wameshao pesa za walalao ni kama shamba la bibi wa kambo, ml 95/ml 3 hainiingii akilini, nanikampitishia pesa zote hizo? na huwa wanazichota wapi?.ameniharibia new year yangu, najuta kwaninimefungua hii kitu.

Punguza munkali kaka... hawa ndo viongoz wetu
 
Hayo malalamiko ni ya siku nyingi juu ya meya Kapunga. Apigwe chini tu
 
hiyo ndio dawa yao wamwagiwe tindikali wafie mbali, maana wameshao pesa za walalao ni kama shamba la bibi wa kambo, ml 95/ml 3 hainiingii akilini, nanikampitishia pesa zote hizo? na huwa wanazichota wapi?.ameniharibia new year yangu, najuta kwaninimefungua hii kitu.

pole mkuu usijali tutafika tu........
 
Ndugu zangu habari za mwaka mpya.

Ni wazi shahiri kuwa meya huyu kauanza mwaka vibaya sana.

Ni ktk kikao cha WDC ambacho huwa cha wazi ilimbidi avunje kikao ili kuruhusu wananchi kutolewa nje.

Agenda ilokuwa inafuatia ni ya matumizi ya tshs 95 ml alizotumia kwenda China kama nauli ilihali nauli halisi ni tshs 3.ml go and return.

Ni madiwani wa chadema wapatao 16 walouwasha moto hadi kufikia na wa ccm kuungana pamoja kuwa arejeshe haraka pesa hizo.

Meya huyu wa STD 7 aligoma akidai zilitumika zote kwenye matumizi ya maradhi.... hapa akaamsha hasira za madiwani walioamka kwa pamoja na kumwagia maji mwili mzima.








Kapunga kwa wanaomfahau vizuri hajaanza wizi leo. Ufisadi ameuanza muda mrefu yeye na Kabwe ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na ndiyo maana kila mkurugenzi mzuri anayepelekwa Mbeya ni lazima amjengee fitina aondoke ili aendelee kufanya ufisadi.Anapenda kuwa na mkurugenzi ambaye anachotaka yeye iwe hivyo.Pia tatizo lipo kwa wanahabari je wanaweza wakaandika habari hiyo ya meya.Namkumbuka mwandishi mmoja wa NIPASHE anaitwa Thobias Mwanakatwe angekuwepo mbeya angeliandika. Huyu meya ni fisadi wa kutupa ana madepo ya kuuza bia kila kona katika jiji la mbeya na mjini mbalizi fedha zote za kifisadi. madiwani chadema kazeni butu hadi ang'oke huyo fisadi.amenunua viongozi wote wa CCM wa wilaya na mkoa hawawezi kukohoa kwake hata akijamba wanasema ndiyo mheshimiwa unasemaje.
 
Hiki ndo chama cha Chriss Lukosi. Na leo kakaribisha watu wengi wajiunge nacho.
 
Ndio mana ninaipenda CHADEMA, Vipi Dk; Mbilinyi hakuwepo kuongeza nguvu.???? Kapunga ang'olewe haraka, amezidisha ufisadi.
 
Habari za Kapunga zimeandikwa sana na waandishi wa habari Mbeya, hata hii ya milioni 95 imeshandikwa kwenye Raia Tanzania, tatizo haliko kwa waandishi wa habari bali nyinyi wenyewe mnaomchagua na madiwani wenu wenye kumpa umeya kwa ajili ya chips kuku anazowapa.

Suala lake lilifika kwa JK akawatolea nje akiwaambia hilo ni suala lao wenyewe mliomchagua.

Sakata la safari ya awali ilikuwa sh 5m/ nalo liliandikwa sana, la sasa mbali ya fedha kuwa kubwa pia hazikuwemo kwenye bajeti ya mwaka ya jiji hilo, zimekombwa kutoka mafungu mengine, ndipo Chadema wanahoji aliyewapa hayo mamlaka.

Wanambeya huo mzigo wenu wenyewe mlioulea, mmeletewa Mkurugenzi, aliyeleta nidhamu na ufani wa kazi, akapandisha makusanyo toka bilioni mbili hadi 15, lakini alipotengezewa majungu na huyo meya wenu na DC Sigala hakuna aliyemtetea mlikaa kimya, leo mnapiga domo hapa.

Simamieni jiji lenu, msiwaachie hao vijana wachache wa Chadema wawatatulie matatizo yenu, waungeni mkono kwa kuingia barabarani. Mbunge wenu Sugu hana nguvu yoyote yupo bize na kunfu bungeni, madiwani wa Chadema hapo Mbeya ni vifaa kinachotakiwa ni kuwaunga mkono kwa wananchi kuingia barabarani hadi Kapunga ang'oke, mkisimama pamoja CCM wataogopa, watamtoa

Ndugu zangu habari za mwaka mpya.

Ni wazi shahiri kuwa meya huyu kauanza mwaka vibaya sana.

Ni ktk kikao cha WDC ambacho huwa cha wazi ilimbidi avunje kikao ili kuruhusu wananchi kutolewa nje.

Agenda ilokuwa inafuatia ni ya matumizi ya tshs 95 ml alizotumia kwenda China kama nauli ilihali nauli halisi ni tshs 3.ml go and return.

Ni madiwani wa chadema wapatao 16 walouwasha moto hadi kufikia na wa ccm kuungana pamoja kuwa arejeshe haraka pesa hizo.

Meya huyu wa STD 7 aligoma akidai zilitumika zote kwenye matumizi ya maradhi.... hapa akaamsha hasira za madiwani walioamka kwa pamoja na kumwagia maji mwili mzima.








Kapunga kwa wanaomfahau vizuri hajaanza wizi leo. Ufisadi ameuanza muda mrefu yeye na Kabwe ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam na ndiyo maana kila mkurugenzi mzuri anayepelekwa Mbeya ni lazima amjengee fitina aondoke ili aendelee kufanya ufisadi.Anapenda kuwa na mkurugenzi ambaye anachotaka yeye iwe hivyo.Pia tatizo lipo kwa wanahabari je wanaweza wakaandika habari hiyo ya meya.Namkumbuka mwandishi mmoja wa NIPASHE anaitwa Thobias Mwanakatwe angekuwepo mbeya angeliandika. Huyu meya ni fisadi wa kutupa ana madepo ya kuuza bia kila kona katika jiji la mbeya na mjini mbalizi fedha zote za kifisadi. madiwani chadema kazeni butu hadi ang'oke huyo fisadi.amenunua viongozi wote wa CCM wa wilaya na mkoa hawawezi kukohoa kwake hata akijamba wanasema ndiyo mheshimiwa unasemaje.
 
Halmashauri wanakwiba mpaka visivyoibika kisha wanalazmisha watumish kuchangia tena kwa lazima, maskin wanakamuliwa mpaka inatoka damu lkn wengine wana connect mrija wanavuta kilaini
 
Mzigo mwingine huo Mbeya m95.Chama cha mizigo na mafurushi. Kiongozi sikivu kwa maisha bora kwanza kwake. BRN.
 
Halmashauri wanakwiba mpaka visivyoibika kisha wanalazmisha watumish kuchangia tena kwa lazima, maskin wanakamuliwa mpaka inatoka damu lkn wengine wana connect mrija wanavuta kilaini

wangemtia adabu kama yule Mabina wa Mwanza kwa nini wamchelewesha hivyo
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom