Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Mhe. Charles Kuyeko Jana alimtembelea na kumjulia hali Mstahiki Meya mstaafu wa Jiji la Dar es salaam, Dkt. Didas Massaburi ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kuyeko alikutana na Mhe. Diwani wa Chanika (CCM), ndugu Ojambi Massaburi ambaye ndiye anamuuguza Babake.
Mbali na kumjulia hali Dkt. Massaburi, Mhe. Kuyeko pia alimtembelea Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) MKoa wa Geita, Kamanda Mwita Mhere aliyepata ajali wiki Jana Mkoani Dodoma. Mhere amelazwa katika hospitali ya taifa Muhimbili kitengo cha MOI akitibiwa majeraha yaliyokana na ajali alisema kuwa kwa sasa anaendelea vizuri. Mhere pia alimshukru Mhe. Kuyeko kwa kuweza kutenga muda wake na kwenda kumuona hospitalini.
Aidha, Mhe. Kuyeko aliwapa pole wagonjwa hao aliowatembelea kwa kuwaombea kwa Mungu ili awaponye haraka na walejee kwenye majukumu yao ya kawaida ili tuendelee kulijenga taifa.
Mbali na kumjulia hali Dkt. Massaburi, Mhe. Kuyeko pia alimtembelea Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) MKoa wa Geita, Kamanda Mwita Mhere aliyepata ajali wiki Jana Mkoani Dodoma. Mhere amelazwa katika hospitali ya taifa Muhimbili kitengo cha MOI akitibiwa majeraha yaliyokana na ajali alisema kuwa kwa sasa anaendelea vizuri. Mhere pia alimshukru Mhe. Kuyeko kwa kuweza kutenga muda wake na kwenda kumuona hospitalini.
Aidha, Mhe. Kuyeko aliwapa pole wagonjwa hao aliowatembelea kwa kuwaombea kwa Mungu ili awaponye haraka na walejee kwenye majukumu yao ya kawaida ili tuendelee kulijenga taifa.