Meya Raibu atoa Mashine ya Photocopy, Printer na Magunia ya mahindi Kwa shule zisizokuwa na uwezo

Aug 21, 2021
16
20
MEYA MOSHI ATOA MASHINE YA PHOTOCOPY PRINTER NA
MAGUNIA YA MAHINDI

Leo Mstahiki Meya Manispaa Ya
Moshi Ameshiriki Kikao Cha Wazazi Shule Ya Msingi Mandela Iliyoko Manispaa Ya Moshi,Ambapo Katika Kikao Hicho Mstahiki Meya Amewapongeza Wazazi Na Waalimu Wa Shule Hiyo Kwa Ufaulu Mzuri Wa Wanafunzi Kuwa Wa Pili Katika Shule Za Serikali Na Wa 9 Shule zote ikiwemo Zikiwemo Shule Binafsi.

Mstahiki Meya Mh.Juma Raib Amekubali Maombi Yao Na Kuwapatia Mashine Ya Photocopy,Printer Pamoja Na Magunia Kumi ya Mahindi Kwa Wanafunzi Wasio Na Uwezo,Mh.Meya Pia Amekabidhi Sh. Laki Moja Kwa Ajili Ya Motisha Kwa Waalimu Ili Waongeze ari Katika Ufundishaji.


Vilevile Mh.Mstahiki Meya Ameahidi Kuendelea Kuleta Maendeleo Katika Shule Zote Za Manispaa ya Moshi Ili Kukuza Ufaulu.Mh.Meya Pia Amewataka Wazazi Kuendelea Kuchangia Fedha Za Chakula Shuleni Kwani Ni Jukumu Lao Ili Kukuza Elimu Ya Msingi.

Mwisho Mh.Meya Ametoa Maelekezo Kuwa Ni Marufuku Kumrudisha Mwanafunzi Kwa Mchango Yoyote Shuleni.View attachment 2037404View attachment 2037405View attachment 2037406
IMG-20211208-WA0002.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Meya anatakiwa kutoa tani za mahindi na maharage
Mamea wa nchi hizi nao ni waganga njaa
Meya lazima uwe na cheda ukitoa msaada unakuwa msaada kweli
 
Zile hela alizoiba na Power Sabaya sasa anaona hazina kazi bora ahonge wanyonge kuosha dhambi.
Hata Yuda alitupa vile vipande 30 vya fedha hekaluni baada ya kuona Yesu amehukumiwa. Raibu is just doing the same. Arudishe hela za Limo.
 
Back
Top Bottom