JalfMoney
JF-Expert Member
- Feb 19, 2019
- 739
- 1,147
Mpuuzi weweUmeshauriwa kuacha ulevi lakini hutaki kusikia haya ndio madhara yake!
Mpuuzi weweUmeshauriwa kuacha ulevi lakini hutaki kusikia haya ndio madhara yake!
Mayor hajui Sheria
Kwanza aliomba mahakama arudishiwe umeya Ina maana alikuwa anajua kuwa yeye Sio meya.Sasa alisema yeye Ni meya kivipi?
Hiyo akidi ya theluthi mbili Ni ya wajumbe waliohudhuria kikao haihesabu hata wale waliosusa kikao
Akidi ilitimia ya kumwondoa
Mayor Issaya Mwita anaandika...
Na Issaya Mwita.
Mayor wa Jiji la DSM.
Marafiki zangu nawashukuru kwa maombi na dua zenu
Kuna watu wengi hawakumuelewa hakimu kwa maamuzi yake ile jana
Nilifungua kesi 6/01/2020... Siku ya Jumatatu, katika maombi yangu nilimtaka hakimu anipe mambo mawili
1. Kwanza anipe zuio la muda na kwamba mimi Isaya Mwita niendelee kuwa Mayor Mpaka pale mahakama itakaposikiliza kesi yangu ya Msingi
Na nikaieleza mahakama kwamba tayari kuna procedure mbalimbali za kuniondoa katika nafasi yangu
Maombi yangu ya pili ilikuwa ni muda wa kudumu mpaka nitakapoipata haki yangu
Kwa kuwa maombi yangu niliyapeleka kwa hati ya dharura tulipangiwa kusikiliza 8/1/2020.
Tarehe 7 jioni wajumbe wa baraza tulipata barua ya kuitwa kwenye kikao na kwamba kikao kitakuwa 9/01/2020... Alhamisi saa 4 asubuhi ...
Kwa hiyo nikaipeleka barua ile ya wito mahakamani asubuhi ya 8/01 ambayo ndiyo ilikuwa siku ya kusikiliza kesi hiyo ...
Barua ile wa wito haikupokelewa ...kwa mizengwe tuu ...na mawakili wa serikali wakiongozwa na Naibu wa mwanasheria Mkuu ndugu Malata ... wakasema barua hiyo ilipaswa kufailiwa kabla ya samansi kuwafikia
Kesi yetu ikaendelea siku hiyo ya tarehe 8 na tulitegemea kupewa status quo...lakini hakimu hakutoa siku ile ..akapanga Siku ya 9... mchana
Kumbuka kwamba wito wa kikao cha baraza ni saa 4 hiyo hiyo 9/01/2020
Ikanilazimu kuhudhuria baraza siku hiyo ...na kama mlivyosoma kwenye vyombo vya habari .... Marafiki zangu hawa wakapiga kura na kupata 16 votes ...
Ikumbukwe kwamba baraza la jiji la Dar es salaam lina wajumbe 26
Wabunge 5... kila mbunge anaiwakilisha wilaya (Halmashauri)
Mameya 6
Na madiwani 15 ...kila Halmashauri inaleta madiwani watatu watatu ... hivyo basi idadi yetu inakamilika kwa kuwa na wajumbe 26
Sasa marafiki zangu kutafuta 2/3 ya 26 unaweza kuona ni 17.3 ...
Kanuni zetu za kudumu ..Toleo la 1982 kama lilivyotangwa na gazeti la serikali ...
Kanuni 12... unaonesha kwamba ...ili kumuondoa Mayor..2/3 ya wajumbe watasaini ili kupata uhalali wa kuitisha mkutano Maalum wa kumuondoa meya ...Kigezo hicho madiwani walikikidhi
Sasa utata ulikuja pale ambapo ..marafiki zangu hawa walimtegemea yule Diwani aliye wasainia kutotokea kwenye kikao ...wakabaki wamepigwa butwaa... Mara wakafanya maamuzi ya haraka .."Tumsainie jina lake" kweli walifanya hivyo ...mimi na baadhi ya wajumbe tulichelea kuingia ... nilipoingia ndiyo nikagundua jina la Diwani yule limekuwa fojali...
Hapo ndipo kizaa zaa kipoanza
Lakini baadae tulikubaliana tukaendelea tukapiga Kura CCM wakapata 16 na sisi tumebaki na kura 2 tu
Kanuni ya 84 (1) inasema Meya ataondolewa madarakani kwa 2/3 ya wajumbe wa Halimashauri hapo ndipo walipokwama.
Wakaanza maigizo kwamba ni 2/3 ya wajumbe waliohudhuria kikao wakasahau kwamba ni 2/3 ya wajumbe ndiyo iliyoitisha kikao kile
Turudi sasa kwa Maamuzi ya Mahakama ...
Kwangu mimi sioni kama Hakimu amekosea kwani hatukupeleka barua ile kwa muda ...
Hivyo alikuwa sawa kuninyima struts quo ...
Lakini pia maamuzi hayo wangekuwa na maana sana ile siku ya 8/01/2020 au 9/01
Maamuzi ya jana hayana athari yoyote kwangu kwa kuwa tayari kile nilichotaka kukizuia kilishafanyika 9/01/2020 ... na kwamba sasa Azimio la kutaka kuniondoa limekosa uhalali wa kikanuni
Asanteni sana.
Yana mwisho haya View attachment 1319222
Naomba ufafanuzi wa haya.
1. Theluthi mbili ya akidi ya wajumbe wa kumtoa Meya haikufika kikanuni , sasa ni kwa nini kikao kikaendelea?
2. Ni kwa nini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi hajatoa tamko lolote hadi sasa?
MIMI KADRI YA MAELEZO YA MEYA AKIDI ILIFIKIWA YA WAJUMBE WALIOHUDHURIA ILI KUPIGA KURA YA KUMTOA.WALIFIKIA 18 JUMLISHA NA MEYA MWENYEWE NI 18. Ila wawili walipinga na kulikuwa na mjumbe aliyetegemewa awepo ili theluthi mbili ya wajumbe wakumwondoa ya 17 iseme ndio. WAJUMBE WAHUSIKA WA KUMWONDOA AMEELEZA NI 26. Huko marekani hata ukiwa mgonjwa unafuatwa upige KURA.Naomba ufafanuzi wa haya.
1. Theluthi mbili ya akidi ya wajumbe wa kumtoa Meya haikufika kikanuni , sasa ni kwa nini kikao kikaendelea?
2. Ni kwa nini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi hajatoa tamko lolote hadi sasa?
Mayor hajui Sheria
Kwanza aliomba mahakama arudishiwe umeya Ina maana alikuwa anajua kuwa yeye Sio meya.Sasa alisema yeye Ni meya kivipi?
Hiyo akidi ya theluthi mbili Ni ya wajumbe waliohudhuria kikao haihesabu hata wale waliosusa kikao
Akidi ilitimia ya kumwondoa
Kuandika kwenyewe tu hueleweki sembuse pointless zako
@Kipara kipya nguo za Ccm
ndio bashite kakutuma hivyo??Kama hurakiwi unangangania Nini?
Mimi nikiwa ndani ya kundi la watu kumi sita tu wakionyesha kunichukia nasepa zangu dakika hiyo hiyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Jifunze kuandika kwanzaKama hurakiwi unangangania Nini?
Mimi nikiwa ndani ya kundi la watu kumi sita tu wakionyesha kunichukia nasepa zangu dakika hiyo hiyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Waziri hajatoa tamko kwa sababu Jiwe hajamwambia lakufanyaNaomba ufafanuzi wa haya.
1. Theluthi mbili ya akidi ya wajumbe wa kumtoa Meya haikufika kikanuni , sasa ni kwa nini kikao kikaendelea?
2. Ni kwa nini Waziri mwenye dhamana na Tamisemi hajatoa tamko lolote hadi sasa?
Kama hurakiwi unangangania Nini?
Mimi nikiwa ndani ya kundi la watu kumi sita tu wakionyesha kunichukia nasepa zangu dakika hiyo hiyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio mkuu. Huwezi kulazimisha kukaa na watu wasiokupenda mwisho wa siku wanakufanyia wanavyojisikia.Mpumbavu nini wewe.Kama wewe ungekuwa na duka kariakoo wanaokuzunguka wakawa hawakutaki ungehamisha duka ukauzie Buza?
Sent using Jamii Forums mobile app