Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Madiwani Mbeya wamweka Meya njia panda
Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, amewekwa njia panda na Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, baada ya kutakiwa kujibu tuhuma nane zinazomkabili ndani ya siku saba, ikiwemo ya matumizi mabaya ya fedha za halmashauri.
Meya huyo anatuhumiwa kutumia Sh. 5, 760,000 kama nauli ya ndege kwenda na kurudi nchini China kwa safari isiyokuwa rasmi ya kikazi.
Alidai sababu nyingine zinazoonyesha kuwa Meya wa Jiji la Mbeya, alihusika katika vurugu hizo ni kwamba, siku Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Mr. Sugu alipokwenda kuzungumza na wananchi kuwatuliza akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Evance Balama na Mkurugenzi wa Jiji, Idd Juma katika hali ya kushangaza Meya huyo ambaye alikuwa katika msafara huo aliingia mitini.
Mwabulanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema, alisema Meya huyo bila idhini ya Baraza la Halmashauri ya Mbeya Mjini, aliidhinisha matumizi ya mamilioni ya fedha za halmashauri kwa ajili ya matumizi ya tume aliyoiunda kuchunguza madiwani wawili kinyume cha kanuni za kudumu za halmashauri ya jiji hilo za mwaka 2004 sehemu ya nne kifungu Na.40, 2 (C) ..........
Meya huyo pia anadaiwa kutumia madaraka yake vibaya kwa kuwaahidi watu viwanja na hivyo kujipatia mamilioni ya fedha, huku akishindwa kuwapatia viwanja hivyo, na kwamba pia ameamuru Diwani wa Kata ya Itende kuvunja daraja lililojengwa kwa fedha za Mbunge wa Mbeya Mjini, Mbilinyi ......
Mara baada ya kusomwa kwa tuhuma hizo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Juma, alitoa ufafanunuzi kuwa, Meya huyo hawezi akazijibu tuhuma katika kikao hicho na badala yake zinatakiwa ziwasilishwe kwa Mkurugenzi ili Meya akabidhiwe na kuzijibu ndani ya siku saba na baadaye zijadiliwe katika kikao cha Baraza la Madiwani kitakachopangwa.........
Meya huyo anatuhumiwa kutumia Sh. 5, 760,000 kama nauli ya ndege kwenda na kurudi nchini China kwa safari isiyokuwa rasmi ya kikazi.
Alidai sababu nyingine zinazoonyesha kuwa Meya wa Jiji la Mbeya, alihusika katika vurugu hizo ni kwamba, siku Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Mr. Sugu alipokwenda kuzungumza na wananchi kuwatuliza akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Evance Balama na Mkurugenzi wa Jiji, Idd Juma katika hali ya kushangaza Meya huyo ambaye alikuwa katika msafara huo aliingia mitini.
Mwabulanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema, alisema Meya huyo bila idhini ya Baraza la Halmashauri ya Mbeya Mjini, aliidhinisha matumizi ya mamilioni ya fedha za halmashauri kwa ajili ya matumizi ya tume aliyoiunda kuchunguza madiwani wawili kinyume cha kanuni za kudumu za halmashauri ya jiji hilo za mwaka 2004 sehemu ya nne kifungu Na.40, 2 (C) ..........
Meya huyo pia anadaiwa kutumia madaraka yake vibaya kwa kuwaahidi watu viwanja na hivyo kujipatia mamilioni ya fedha, huku akishindwa kuwapatia viwanja hivyo, na kwamba pia ameamuru Diwani wa Kata ya Itende kuvunja daraja lililojengwa kwa fedha za Mbunge wa Mbeya Mjini, Mbilinyi ......
Mara baada ya kusomwa kwa tuhuma hizo, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Juma, alitoa ufafanunuzi kuwa, Meya huyo hawezi akazijibu tuhuma katika kikao hicho na badala yake zinatakiwa ziwasilishwe kwa Mkurugenzi ili Meya akabidhiwe na kuzijibu ndani ya siku saba na baadaye zijadiliwe katika kikao cha Baraza la Madiwani kitakachopangwa.........