Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
NAMUOMBEA MSAMAHA DC WA UBUNGO KWA WANANCHI
Baada ya kupata wasaa na Muda wa kutosha wa kutafakari, ni muda sahihi wa kuongelea tukio hili la kijinga na Maudhi.
Ni dhahiri kuanzia Jumatano nitoke Mahabusu ya POLISI mpaka leo jumamosi ni kweli hasira zimeisha na busara imetamalaki kichwani kwangu.
Nimeona kupitia vyombo mbalimbali vya Habari na mitandao ya kijamii kila mtu akilaani na kukasirishwa na Matumizi mabaya dhidi ya vyombo vya Dola, hata kupelekea mimi kushikiliwa kituo cha polisi Mbezi(w).
Kwa Masaa 48 mahabusu hata mimi nilikuwa na hasira sana, kwanza nilijiona ninamkosi kwakuwa nilihisi anayafanya haya sababu ya Maswahibu yaliyomkuta ya kuondolewa kuwa Boss ikulu mpaka kuletwa kuwa Dc Ubungo.
Msameheni Dc Ubungo, kwa sababu tatu:
1. Nimepata ujumbe wake kwa walio nifikishia kuwa, anakiri tukio la namna ile si Zuri, na ametoa pole na masikitiko yake kutoka Moyoni.
2. Kwa sababu hao walio na Mamlaka juu yake walitaka afanye vile, asinge fanya kama alivyo agizwa ni dhahiri ingekula kwake Mazima, hivyo alikuwa anatetea Kitumbua chake.
3.Kaonyesha Uungwana mkubwa sana, ingawa amekosa uthubutu wa kuyasema hayo Hadharani, lakini tunapaswa kuyajua mazimgira ya kazi yake na kibarua chake.
Kw sababu tatu nilizo taja hapo juu ADUI wa wana Ubungo siyo DC ni hao waliomuagiza kufanya aliyoyafanya,na waliotoa Amri hiyo sina sababu ya kuwa taja,
Mimi ninawajua...
Wewe unawajua....
Watanzania wanawajua....
Dunia inawajua......
Kulumbana na Dc ni kupoteza lengo katika Halmashauri yetu mpya na nzuri tuliyopewa na Wananchi wakati wa uchaguzi 2015.
Wakati Ubungo kuna kampeni ovu inayoitwa KOMBOA UBUNGO Inayo ongozwa na DSO UBUNGO kwa maana ya kuwarudisha CCM majimboni na kwenye kata.....
Mimii ninawaomba kumpatia ushirikiano DC kwakuwa ni mtu mwelewa kwakiwango fulani, ni jambo hili tu Mabosi zake walilenga kumfitinisha na Viongozi wa Halmashauri.
Aidha nimepokea pole na Hongera za Watanzania nje na ndani ya Ubungo
Masaa 48 polisi Mbezi, yamenifanya nikamilishe "kukaa ndani" Mahabusu zote za Dar, nilisha kaa mahabusu 15 na Magereza manne(4), ilikuwa imebakia mahabusu 1 ya Mbezi polisi, tena kwa makosa ya kisiasa, hivyo nimemuhaidi OCD MBEZI POLISI kupeleka vifaa vya usafi.
MWISHO
Ninapenda kuutarifu Umma wa Watanzania ndani na nje ya Ubungo kuwa Nimeanza safari rasmi ya kutafuta haki dhidi ya sheria hii kandimizi ya ma Dc na ma Rc, haijalishi nitafika au la.
Moyoni nimeweka Nadhiri ya kuwa kiongozi wa Mwisho wa kisiasa aliyechaguliwa kutendewa sivyo kwa kisingizio cha sheria kandamizi na hata kama safari hii kuna nitakao wagusa, basi ni kwa sababu itahitajika mifano tu. Lakini nia ni mimi kuwa muhanga wa mwisho.
Na Boniface Jacob
Mstahiki Meya
Halmashauri ya ubungo
Senior councilor
Baada ya kupata wasaa na Muda wa kutosha wa kutafakari, ni muda sahihi wa kuongelea tukio hili la kijinga na Maudhi.
Ni dhahiri kuanzia Jumatano nitoke Mahabusu ya POLISI mpaka leo jumamosi ni kweli hasira zimeisha na busara imetamalaki kichwani kwangu.
Nimeona kupitia vyombo mbalimbali vya Habari na mitandao ya kijamii kila mtu akilaani na kukasirishwa na Matumizi mabaya dhidi ya vyombo vya Dola, hata kupelekea mimi kushikiliwa kituo cha polisi Mbezi(w).
Kwa Masaa 48 mahabusu hata mimi nilikuwa na hasira sana, kwanza nilijiona ninamkosi kwakuwa nilihisi anayafanya haya sababu ya Maswahibu yaliyomkuta ya kuondolewa kuwa Boss ikulu mpaka kuletwa kuwa Dc Ubungo.
Msameheni Dc Ubungo, kwa sababu tatu:
1. Nimepata ujumbe wake kwa walio nifikishia kuwa, anakiri tukio la namna ile si Zuri, na ametoa pole na masikitiko yake kutoka Moyoni.
2. Kwa sababu hao walio na Mamlaka juu yake walitaka afanye vile, asinge fanya kama alivyo agizwa ni dhahiri ingekula kwake Mazima, hivyo alikuwa anatetea Kitumbua chake.
3.Kaonyesha Uungwana mkubwa sana, ingawa amekosa uthubutu wa kuyasema hayo Hadharani, lakini tunapaswa kuyajua mazimgira ya kazi yake na kibarua chake.
Kw sababu tatu nilizo taja hapo juu ADUI wa wana Ubungo siyo DC ni hao waliomuagiza kufanya aliyoyafanya,na waliotoa Amri hiyo sina sababu ya kuwa taja,
Mimi ninawajua...
Wewe unawajua....
Watanzania wanawajua....
Dunia inawajua......
Kulumbana na Dc ni kupoteza lengo katika Halmashauri yetu mpya na nzuri tuliyopewa na Wananchi wakati wa uchaguzi 2015.
Wakati Ubungo kuna kampeni ovu inayoitwa KOMBOA UBUNGO Inayo ongozwa na DSO UBUNGO kwa maana ya kuwarudisha CCM majimboni na kwenye kata.....
Mimii ninawaomba kumpatia ushirikiano DC kwakuwa ni mtu mwelewa kwakiwango fulani, ni jambo hili tu Mabosi zake walilenga kumfitinisha na Viongozi wa Halmashauri.
Aidha nimepokea pole na Hongera za Watanzania nje na ndani ya Ubungo
Masaa 48 polisi Mbezi, yamenifanya nikamilishe "kukaa ndani" Mahabusu zote za Dar, nilisha kaa mahabusu 15 na Magereza manne(4), ilikuwa imebakia mahabusu 1 ya Mbezi polisi, tena kwa makosa ya kisiasa, hivyo nimemuhaidi OCD MBEZI POLISI kupeleka vifaa vya usafi.
MWISHO
Ninapenda kuutarifu Umma wa Watanzania ndani na nje ya Ubungo kuwa Nimeanza safari rasmi ya kutafuta haki dhidi ya sheria hii kandimizi ya ma Dc na ma Rc, haijalishi nitafika au la.
Moyoni nimeweka Nadhiri ya kuwa kiongozi wa Mwisho wa kisiasa aliyechaguliwa kutendewa sivyo kwa kisingizio cha sheria kandamizi na hata kama safari hii kuna nitakao wagusa, basi ni kwa sababu itahitajika mifano tu. Lakini nia ni mimi kuwa muhanga wa mwisho.
Na Boniface Jacob
Mstahiki Meya
Halmashauri ya ubungo
Senior councilor