Meya Arusha ataka RC Gambo afungwe kwa kukaidi mahakama

Jembe Jembe

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
749
1,797
MKUU wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ametakiwa kujitathimini iwapo anastahili kuendelea kuwa mtumishi wa umma katika nafasi aliyonayo baada ya kutiwa hatiani na mahakama kuu mkoa wa Tanga na kutakiwa kulipa kiasi cha shilingi milioni 20 kwa kosa la kumdhalilisha mtumishi mwenzake kwa matusi.


Kesi hiyo namba 4 ya mwaka 2015,Gambo alikata rufaa mahakama kuu ,kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama za chini,katika kesi ya madai iliyofunguliwa na mlalamikaji ,Najum Tekka ambaye ni mwanasheria wa halmashauri wilaya ya Korogwe aliyekuwa akimlalamikia Gambo kumtolea lugha ya kumdhalilisha kuwa anadigrii ya nguo ya ndani(chupi).


Kwa mujibu wa hukumu hiyo nakala tunayo, iliyotolewa, Septemba 9 mwaka 2016 na jaji Amour Khamis wa mahakama kuu,mkoani humo,meya wa jiji la Arusha, Kalisti Lazaro alisema kuwa Gambo amekaidi kulipa kiasi hicho cha fedha kilichoamuriwa na mahakama na kuitaka mahakama itoe amri akamatwe na kufilisiwa Mali zake na afungwe.
ab29aaca6844bedd42e89253bb22f42c.jpg
 
Wanasheria tunaomba msaada hapa...iwapo serikali ikikaidi amri ya mahakama nini kinafuata???

Au kama hivi Gambo anapokaidi mahakama inatakiwa ifanye nini?
 
Huyo RC anafanya madudu mengi sana.....

Lakini kiburi chote hiko anakipata toka kwa Bwana yule ambaye alishaapa kuwa hakuna mTz yeyote anayepaswa kumpangia la kufanya!

Huyo RC wa Arusha hana tofauti na Bashite, hao maRC wawili wana kiburi cha kupindukia kutokana na kubebwa na mbeleko ya Mkulu.

Imekuwa vyema mahakama imetoa uamuzi wa aina hiyo, bila kujali kuwa huyo jamaa ni 'untouchable'

Sasa tusubiri kauli ya yule Bwana ambaye huwa anatamba hadharani kuwa mhimili wake ni zaidi, kwa kuwa umejichimbia zaidi chini!
 
Kama hayo ni ya kweli RC Gambo anatakiwa kuwajibishwa. Sheria lazima ichukue mkondo wake, tena haraka. Hiyo ndiyo haki!
Unategemea huyu huyu Magu amwajibishe?

Hebu jiulize swali dogo tu hivi scandal zote alizozifanya Bashite, alistahili kuendelea kuwa RC?

Lakini anaendelea kuwa RC kutokana na mbeleko ya Bwana mkubwa......

Vivyo hivyo kwa Gambo.

Kwa scandal moja tu ya 'kutafuna' rambirambi za wafiwa wa St Vincent, hivi bado angeendelea kuwa RC wa Arusha?

Lakini anaendelea kuwa RC kwa kuwa anaendelea 'kubebwa' na Bwana mkubwa!
 
Hizi tabia za kutumia madaraka vibaya Gambo ameanza kitambo tangu akiwa DC.Kwa hukumu hii ambayo tayari ni sheria iwe funzo kwa wenzanke wanaotumia madaraka vibaya,wajue kuna siku watasimama mahakamani na kujibu waliyotenda,tena watasimamishwa kwa capacity yao wenyewe!
 
MKUU wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo ametakiwa kujitathimini iwapo anastahili kuendelea kuwa mtumishi wa umma katika nafasi aliyonayo baada ya kutiwa hatiani na mahakama kuu mkoa wa Tanga na kutakiwa kulipa kiasi cha shilingi milioni 20 kwa kosa la kumdhalilisha mtumishi mwenzake kwa matusi.


Kesi hiyo namba 4 ya mwaka 2015,Gambo alikata rufaa mahakama kuu ,kupinga hukumu iliyotolewa na mahakama za chini,katika kesi ya madai iliyofunguliwa na mlalamikaji ,Najum Tekka ambaye ni mwanasheria wa halmashauri wilaya ya Korogwe aliyekuwa akimlalamikia Gambo kumtolea lugha ya kumdhalilisha kuwa anadigrii ya nguo ya ndani(chupi).


Kwa mujibu wa hukumu hiyo nakala tunayo, iliyotolewa, Septemba 9 mwaka 2016 na jaji Amour Khamis wa mahakama kuu,mkoani humo,meya wa jiji la Arusha, Kalisti Lazaro alisema kuwa Gambo amekaidi kulipa kiasi hicho cha fedha kilichoamuriwa na mahakama na kuitaka mahakama itoe amri akamatwe na kufilisiwa Mali zake na afungwe.
ab29aaca6844bedd42e89253bb22f42c.jpg

Inaonekana ni kesi ya madai ya kuchafuliwa jina kwa hiyo mdai anatakiwa akaze hukumu ili mali za mdaiwa zikamatwe na kama hana au amezificha mdai aiombe mahakama imfunge jela ya madai(civil prison) mpaka alipe kwani serikali haihusiki kwa kesi binafsi za viongozi.
 
Yaani watu mnavyojadili utafikiri kweli... Kweli watanzania wawekee topic yoyote hata ya uongo then.....
 
Back
Top Bottom