Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,000
- 9,861
Mauaji yamefikia viwango vya hali ya juu nchini Mexico, huku watu 95 wakiuawa kila siku nchini humo - hii ikimaanisha kuwa mtu mmoja huuawa kila baada ya dakika 15.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi, kulikuwa na mauaji ya watu 34,582 mwaka 2019, ikiwa ni idadi ya juu zaidi ikilinganishwa na wakati rekodi za mauaji hayo zilipoanza kuchukuliwa mnamo mwaka 1997.
Idadi hiyo ikilinganishwa na mauaji ya mataifa mengine, wapiganaji wapatao 11,000 na raia waliuawa katika vita vilivyotokea nchini Syria mwaka 2019, kwa mujibu wa taasisi ya uangalizi ya Haki za binadamu nchini Syria.
Mitandao ya wauzaji wa madawa ya kulevya nchini Mexico imekuwa ikilaumiwa kwa kuchafua sura ya nchi inayoifanya kuwa moja ya mahala hatari zaidi duniani.
Mapema mwezi huu, wanamuziki wazawa walipigwa risasi na kuchomwa moto magharibi mwa Mexico katika shambulio ambalo linaaminiwa kufanywa na mtandao wa walanguzi wa dawa za kulevya.
Waathiriwa, walikua na umri wa kati ya miaka 15 na 42, walikua wakirudi kutoka katika sherehe wakati waliposhambuliwa katika mji wa Chilapa katika jimbo la Guerrero.
Mwezi Novemba watu tisa wa familia ya yenye asili ya Mexico na Marekani kutoka dini ya Mormon - akina mama watatu na watoto sita - waliuawa katika shambulio lililofanywa na mtandao wa magenge yenye silaha- jambo lililoibua hisia kali na raia wa nchi hiyo wa ndani na nje walitoa wito wa kufanyika kwa mageuzi.
Kufuatia tukio hilo, wanaharakati wawili maarufu - Javier Sicilia na Julian LeBaron - walitoa wito wa kufanyika kwa matembezi ya amani siku ya Alhamisi tarehe 23 katika mji wa Merelos na kuendelea kwa siku tatubaadae katika mji mkuu , Mexico City.
Chanzo: BBC
Kwa mujibu wa taarifa rasmi, kulikuwa na mauaji ya watu 34,582 mwaka 2019, ikiwa ni idadi ya juu zaidi ikilinganishwa na wakati rekodi za mauaji hayo zilipoanza kuchukuliwa mnamo mwaka 1997.
Idadi hiyo ikilinganishwa na mauaji ya mataifa mengine, wapiganaji wapatao 11,000 na raia waliuawa katika vita vilivyotokea nchini Syria mwaka 2019, kwa mujibu wa taasisi ya uangalizi ya Haki za binadamu nchini Syria.
Mitandao ya wauzaji wa madawa ya kulevya nchini Mexico imekuwa ikilaumiwa kwa kuchafua sura ya nchi inayoifanya kuwa moja ya mahala hatari zaidi duniani.
Mapema mwezi huu, wanamuziki wazawa walipigwa risasi na kuchomwa moto magharibi mwa Mexico katika shambulio ambalo linaaminiwa kufanywa na mtandao wa walanguzi wa dawa za kulevya.
Waathiriwa, walikua na umri wa kati ya miaka 15 na 42, walikua wakirudi kutoka katika sherehe wakati waliposhambuliwa katika mji wa Chilapa katika jimbo la Guerrero.
Mwezi Novemba watu tisa wa familia ya yenye asili ya Mexico na Marekani kutoka dini ya Mormon - akina mama watatu na watoto sita - waliuawa katika shambulio lililofanywa na mtandao wa magenge yenye silaha- jambo lililoibua hisia kali na raia wa nchi hiyo wa ndani na nje walitoa wito wa kufanyika kwa mageuzi.
Kufuatia tukio hilo, wanaharakati wawili maarufu - Javier Sicilia na Julian LeBaron - walitoa wito wa kufanyika kwa matembezi ya amani siku ya Alhamisi tarehe 23 katika mji wa Merelos na kuendelea kwa siku tatubaadae katika mji mkuu , Mexico City.
Chanzo: BBC