Mexico: Watu 95 huuawa kila siku

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,861
Mauaji yamefikia viwango vya hali ya juu nchini Mexico, huku watu 95 wakiuawa kila siku nchini humo - hii ikimaanisha kuwa mtu mmoja huuawa kila baada ya dakika 15.

Kwa mujibu wa taarifa rasmi, kulikuwa na mauaji ya watu 34,582 mwaka 2019, ikiwa ni idadi ya juu zaidi ikilinganishwa na wakati rekodi za mauaji hayo zilipoanza kuchukuliwa mnamo mwaka 1997.

Idadi hiyo ikilinganishwa na mauaji ya mataifa mengine, wapiganaji wapatao 11,000 na raia waliuawa katika vita vilivyotokea nchini Syria mwaka 2019, kwa mujibu wa taasisi ya uangalizi ya Haki za binadamu nchini Syria.

Mitandao ya wauzaji wa madawa ya kulevya nchini Mexico imekuwa ikilaumiwa kwa kuchafua sura ya nchi inayoifanya kuwa moja ya mahala hatari zaidi duniani.

Mapema mwezi huu, wanamuziki wazawa walipigwa risasi na kuchomwa moto magharibi mwa Mexico katika shambulio ambalo linaaminiwa kufanywa na mtandao wa walanguzi wa dawa za kulevya.

Waathiriwa, walikua na umri wa kati ya miaka 15 na 42, walikua wakirudi kutoka katika sherehe wakati waliposhambuliwa katika mji wa Chilapa katika jimbo la Guerrero.

Mwezi Novemba watu tisa wa familia ya yenye asili ya Mexico na Marekani kutoka dini ya Mormon - akina mama watatu na watoto sita - waliuawa katika shambulio lililofanywa na mtandao wa magenge yenye silaha- jambo lililoibua hisia kali na raia wa nchi hiyo wa ndani na nje walitoa wito wa kufanyika kwa mageuzi.

Kufuatia tukio hilo, wanaharakati wawili maarufu - Javier Sicilia na Julian LeBaron - walitoa wito wa kufanyika kwa matembezi ya amani siku ya Alhamisi tarehe 23 katika mji wa Merelos na kuendelea kwa siku tatubaadae katika mji mkuu , Mexico City.

Chanzo: BBC
 
Latin America kuna shida sana ya madawa ya kulevya sishangai kuuana katika scale hii

Nchi ambazo hakuna utumiaji mkubwa wa drugs huwa hakuna homicides katika rate za juu hata siku moja India, China being the case

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dawa ya kuzuia mauaji ni kuruhusu biashara ya unga iwe halali dunia nzima. Mwenye kuutaka anunue na asiye utaka auache. pombe na sigara, zilikuwa hivyo lakini kwa sasa hakuna shida na wapo walevi na ambao sio walevi.

Huko Marekani wameruhusu matumizi ya bangi, siku hizi husikii sijui drug dealer wala nini, na crime imepungua.
Wakiruhusu biashara ya unga hata Mexico patakuwa kama Geneva, Switzerland tu.

Hakuna haja ya kuzuia biashara ya unga iruhusiwe. Watakao penda watatumia,na wasipenda watauacha.

Hapa Tanzania kuna Bar kila kona, wapo walevi na wapo wasiowalevi, na wapo wale seasonal walevi, yani wakizikamata wanalewa. Iwe hivyo kwenye Unga.
 
Dawa ya kuzuia mauaji ni kuruhusu biashara ya unga iwe halali dunia nzima. Mwenye kuutaka anunue na asiye utaka auache. pombe na sigara, zilikuwa hivyo lakini kwa sasa hakuna shida na wapo walevi na ambao sio walevi.

Huko Marekani wameruhusu matumizi ya bangi, siku hizi husikii sijui drug dealer wala nini, na crime imepungua.
Wakiruhusu biashara ya unga hata Mexico patakuwa kama Geneva, Switzerland tu.

Hakuna haja ya kuzuia biashara ya unga iruhusiwe. Watakao penda watatumia,na wasipenda watauacha.

Hapa Tanzania kuna Bar kila kona, wapo walevi na wapo wasiowalevi, na wapo wale seasonal walevi, yani wakizikamata wanalewa. Iwe hivyo kwenye Unga.
Naskia arosto ya unga ni hatari sana mateja wapo tayari kuua ili apate buku tu ya unga. Madawa yakiruhusiwa mateso yataongezeka. Juzi nilisikiliza mahojiano ya aliekuwa demu wa chidbenz anasema mtu mmoja akivuta unga kwenye familia ni sawa na kusema familia nzima inatumia unga kwa mateso watakayopata ikiwa ni pamoja na wizi,hofu,huzuni nk.
 
Naskia arosto ya unga ni hatari sana mateja wapo tayari kuua ili apate buku tu ya unga. Madawa yakiruhusiwa mateso yataongezeka. Juzi nilisikiliza mahojiano ya aliekuwa demu wa chidbenz anasema mtu mmoja akivuta unga kwenye familia ni sawa na kusema familia nzima inatumia unga kwa mateso watakayopata ikiwa ni pamoja na wizi,hofu,huzuni nk.
Hapana hayo unayaona kwasababu haujaruhusiwa, ukiruhusiwa unapatika kwa urahisi kunakua hakuna wizi, unapatikana hadi kwa mkopo.
Ngoja waje waruhusu ndio utaelewa naongelea nini.
 
Sijui yule mdada marichui walimuua....!!,maana simuoni siku hizi.
Mexico wanaizidi Hadi Syria iliyoko vitani
Mexico inateseka na itaendelea kuteseka sana na haya mauaji sababu ipo jirani na nchi yenye soko kubwa la madawa ya kulevya duniani (Marekani).

Hayo mengine ya rushwa, ufisadi ni matokeo ya kuwa karibu na hilo soko (Marekani).
 
Tatizo huko Mexico drug cartels wana hela ndefu kuliko serikali na wana mavifaa ya kivita ya kisasa pengine kuliko ya serkali yao
Hawazidi serikali jeshi la Mexico liko vizuri tu,tatizo Hawa druglord hawana mchezo,yaani wakigundua judge au polise fulani Ni kichomi wanakufuata na kukupa option,pokea pesa uwalegezee ama ufe,na Kama una ulinzi mkali,family yako itakufa,Sasa huwezi weka ulinzi kwa ukoo mzima,
So kabla hawajakufuata wanakuwa na file lako details zote,watoto wanakosoma,address yako,mama yako Yuko wapi etc,,,lazima utalainika tu,
Ndo maana druglord wakikamatwa wanapelekwa USA,,,Askari wanaokamata lazima kuvaa mask
 
Hawazidi serikali jeshi la Mexico liko vizuri tu,tatizo Hawa druglord hawana mchezo,yaani wakigundua judge au polise fulani Ni kichomi wanakufuata na kukupa option,pokea pesa uwalegezee ama ufe,na Kama una ulinzi mkali,family yako itakufa,Sasa huwezi weka ulinzi kwa ukoo mzima,
So kabla hawajakufuata wanakuwa na file lako details zote,watoto wanakosoma,address yako,mama yako Yuko wapi etc,,,lazima utalainika tu,
Ndo maana druglord wakikamatwa wanapelekwa USA,,,Askari wanaokamata lazima kuvaa mask
Umenena
 
Dawa ya kuzuia mauaji ni kuruhusu biashara ya unga iwe halali dunia nzima. Mwenye kuutaka anunue na asiye utaka auache. pombe na sigara, zilikuwa hivyo lakini kwa sasa hakuna shida na wapo walevi na ambao sio walevi.

Huko Marekani wameruhusu matumizi ya bangi, siku hizi husikii sijui drug dealer wala nini, na crime imepungua.
Wakiruhusu biashara ya unga hata Mexico patakuwa kama Geneva, Switzerland tu.

Hakuna haja ya kuzuia biashara ya unga iruhusiwe. Watakao penda watatumia,na wasipenda watauacha.

Hapa Tanzania kuna Bar kila kona, wapo walevi na wapo wasiowalevi, na wapo wale seasonal walevi, yani wakizikamata wanalewa. Iwe hivyo kwenye Unga.

Hawawezi kuruhusu kwani hela hizo nyingi ndio zinaendesha asilimia kadhaa katika baadhi za nchi
Unga unaingia sana USA kutoka huko
Angalia sehemu zote panapotikana OIL, DRUGS kama cocaine na pia Madini lazima Kuna machafuko
Jiulize kwanini hawatoki Afghan
wapo sasa mwaka wa 19 na wanajeshi wa kizungu zaidi ya 2500 wamekufa na USA pekee wametumia zaidi ya $1t yes 1Trillion
Yote hiyo wanapata zaidi ya hiyo kwa Poppy
Uarabuni kwa Mafuta, na huko cocaïne africa Madini
Wao (wazungu) hawawezi kuifanya cocaïne iwe kawaida kama bangi itakuwa ni sawa na kusema diamond ziuzwe kama gololi


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Wewe umeongea point ilakwa sasahuwezi kueleweka
Dawa ya kuzuia mauaji ni kuruhusu biashara ya unga iwe halali dunia nzima. Mwenye kuutaka anunue na asiye utaka auache. pombe na sigara, zilikuwa hivyo lakini kwa sasa hakuna shida na wapo walevi na ambao sio walevi.

Huko Marekani wameruhusu matumizi ya bangi, siku hizi husikii sijui drug dealer wala nini, na crime imepungua.
Wakiruhusu biashara ya unga hata Mexico patakuwa kama Geneva, Switzerland tu.

Hakuna haja ya kuzuia biashara ya unga iruhusiwe. Watakao penda watatumia,na wasipenda watauacha.

Hapa Tanzania kuna Bar kila kona, wapo walevi na wapo wasiowalevi, na wapo wale seasonal walevi, yani wakizikamata wanalewa. Iwe hivyo kwenye Unga.
 
Ndo maana druglord wakikamatwa wanapelekwa USA,,,Askari wanaokamata lazima kuvaa mas
USA ndio soko kubwa la madawa ya kulevya (linalolipa vizuri) hii ndio sababu ya raia wa Mexico kuteseka.

Inabidi Mexico ipewe msaada na USA kwenye hiyo Vita dhidi ya madawa kuanzia intellijensia, fedha, mafunzo na silaha bila kusahau miradi ya kijamii kuwahudumia waathirika wa hii vita na sio kujengewa ukuta.
 
Hawawezi kuruhusu kwani hela hizo nyingi ndio zinaendesha asilimia kadhaa katika baadhi za nchi
Unga unaingia sana USA kutoka huko
Angalia sehemu zote panapotikana OIL, DRUGS kama cocaine na pia Madini lazima Kuna machafuko
Jiulize kwanini hawatoki Afghan
wapo sasa mwaka wa 19 na wanajeshi wa kizungu zaidi ya 2500 wamekufa na USA pekee wametumia zaidi ya $1t yes 1Trillion
Yote hiyo wanapata zaidi ya hiyo kwa Poppy
Uarabuni kwa Mafuta, na huko cocaïne africa Madini
Wao (wazungu) hawawezi kuifanya cocaïne iwe kawaida kama bangi itakuwa ni sawa na kusema diamond ziuzwe kama gololi


Sent from my iPhone using Tapatalk
Wanaruhusu tu uone, hutosii machafuko tena.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom