Afrika Furaha
JF-Expert Member
- Dec 16, 2010
- 329
- 9
Messi kwa kweli anaitafuna La Liga kama vile ni Ligi Kuu ya Shangazi yake, kila mwisho wa wiki ana mabao mawili au matatu, na Barca hawapitishi wiki bila kupiga mtu 4 au zaidi. Nadhani Messi aende kucheza England ajaribu kukabwa na mabeki wenye ROHO MBAYA wa English Premier League, tuone kama kweli anaweza kuchomoza na mabao kila wiki akicheza viwanja vya White Hart Lane, Old Trafford, Goodson Park, Stamford Brigde n.k. Mwenzie Ronaldo ameshakomazwa na Ligi hiyo kiboko duniani