Meremeta, Randgold,Tangold & The Jersey Connection: Jeshi liliingizwaje hapa?

Bill

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
8,251
8,456
Kwa Uchache: Ya Meremeta, Tangold, JWTZ na Signatories

Waziri akizima hoja ya Slaa kuhusu Ukaguzi wa Meremeta/Tangold alisema haiwezi kujadiliwa hadharani kwa kuwa inahusu mambo nyeti ya usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi Tanzania - JWTZ.

Ilishadhihirika kuwa Meremeta ilirithisha shughuli zake kwa Tangold, na kwamba Serikali kupitia BOT iliilipia deni kubwa kupitia benki ya SA zaidi ya TZS 155 bn. Tangold ikachukua kazi za Meremeta.

Kwa maana hiyo Tangold ni mali ya usalama wa Taifa kupitia JWTZ. Na kwa maana hiyo pia CHENGE mtia saini mkuu wa akaunti za Tangold ndiye Signatories wa JWTZ.

Ni akaunti ngapi za JWTZ ambazo Chenge na wenzake ni lazima waanguke sahihi zao ndio hela zitoke.

Kwa nini jeshi la nchi yetu linadhalilishwa katika wizi huu limekaa kimya, linatakiwa kuja na kutoa ufafanuzi ikibidi kuichukulia hatua za kinidhamu Serikali.

Leteni michango yenu kwa ufupi
 
Kwa Uchache: Ya Meremeta, Tangold, JWTZ na Signatories

Kwa nini jeshi la nchi yetu linadhalilishwa katika wizi huu limekaa kimya, linatakiwa kuja na kutoa ufafanuzi ikibidi kuichukulia hatua za kinidhamu Serikali.
Leteni michango yenu kwa ufupi

Kama hatua ipi kwa mfano?
 
Huu mjadala unazimwa kwa lipi haswa ? Je ni kwa maslahi ya watawala au maslahi ya taifa? Je usalama wa taifa upo kwa ajili ya nani kama si raia ????
 
Kuna jamaa hapo juu wanaanza kudiscuss the spelings! Nadhani nao wana nia ya kuuzima huu mjadala hapa JF. So wapo wengi pia hapa JF wenye nia hiyo.

Otherwise Bill umetoa mchanganuo mzuri sana. Ni kitu ambacho tunahitaji majibu na si majibu OVYO OVYO.
 
Mzee Bill, nadhani ulimaanisha "Signatories".

Wenye jukumu la kutia saini ktk cheki za kampuni ya Tangold, ili bank inayoweka fedha zake iweze kumlipa mteja yeyote, waliteuliwa, kama ilivyo kawaida, na bodi ya kampuni. Andrew Chenge, akiwa Attorney General wa Tanzania wakati wa kampuni kuundwa alikuwa Member wa Bodi. Kwa usahihi kabisa akateuliwa ni mmoja wa signatories.

ULAJI ulipoamza kwa nguvu miongoni mwa watumishi wa umma, (baada ya Muasisi wa Taifa kuondoka) inaonekana Chenge aliruhusiwa "kununua" hisa ktk hii kampuni, kwa bei tusiyofahamu.

Sina hakika kama ni wakati huo alipofungua akaunti ktk Bank ya kule Jersey Islands, Uingereza, na kuanza kulundika "vijisenti" huko. Waingereza wametuarifu kwamba ktk mgao wa ile commission ya 30 percent ya ununuzi wa Radar, US$ 600,000 zilizolipwa bwana Vijisenti, ziliwekwa huko.

Waingereza wanajua. Sisi Tanzania tumearifiwa. Pia tunajua kwamba ile bei ya radar ilikuwa ya kuruka sana, kiasi cha Waziri mmoja wa Uingereza (?Judith Short) kutusemea ktk Bunge lao kwamba kampuni yao ilitudanganya. Sisi wenyewe tunatambua commission ya 30 percent ni kufuru na wizi wa hadharani. Lakini "Uchunguzi" wetu bado haujakamilika, licha ya madokezo na madondoo yote hayo.

Viongozi wazalendo jasiri, wakiongozwa na Dk. Willibrod Slaa Bungeni, wakauliza "kulikoni?". Mheshimiwa Jeremiah Sumari, Naibu Waziri wetu wa Fedha tunayemlipa mshahara, akasema maswali hayo yanahusu viongozi wa JWTZ na kwamba hayazungumzwi! Hapa akiimanisha kwamba ukiteuliwa kiongozi ktk Jeshi, basi hata aliyekuteuwa, yaani Serikali inayosimamiwa na Bunge, haiwezi kukuhoji unapokwiba fedha za umma.

Swali lilikuwa Controller and Auditor General aanze kazi mapema kukagua makampuni haya yenye hisa nyingi za Serikali ili Bunge lijue ni nini kilifanyika. Ni jukumu lao.

Mhe. Sumari sio tu alijibu utumbo, bali alimalizia kumwambia Mhe. Slaa abuni hoja nyingine kuleta Bungeni!

Siku iliyofuata, Mhe. Zitto Kabwe akielezea masikitiko yake kuhusu majibu ya Mhe. Sumari, ambayo kwa kila muelewa aliyeyasikia aliona ni ya "hovyo hovyo" akaamuriwa na kiongozi wa Bunge eti ayafute maneno hayo. Sasa tujiulize "Je Tutafika?"

Mimi naona Bunge hili la sasa likiwa na majority ya wana-CCM, limefikia kikomo ktk kupuuza maslahi halisi ya WaTz. Na Serikali yenyewe inaonekana kuwa ni jumuiya ya watu wasioelewa au wasiojali maovu yanayofanyiwa nchi yao, yanayosababisha kutokufikia malengo ya kujikwamua ktk ujinga, umaskini na maradhi yanayotuangamiza.
 
Hili wazo la kwanini JWTZ haitoi tamko hata mimi limenijia wakati kazaa kichwani, serikali inalipaka matope jeshi hapa, na sisi wananchi tutalichukia jeshi kwa namna hii...mana kumbe hata lenyewe linajihusisha na ufisadi...kama sio kweli, JWTZ mko wapi mkipakwa matope...??
 
Bill,
Hao askari wanaoifahamu hiyo Meremeta ni asilimia ndogo sana ya jeshi letu. Hapo ndipo utakubali kuwa ile kauli ya Chiligati kule Busanda kuhusu uwezo wa wananchi kusoma magazeti na vyombo vya habari kwa ujumla haikutoka kwa bahati mbaya. Kwao hizi ni kelele za mlango!
 
Mzee Bill, nadhani ulimaanisha "Signatories".

Wenye jukumu la kutia saini ktk cheki za kampuni ya Tangold, ili bank inayoweka fedha zake iweze kumlipa mteja yeyote, waliteuliwa, kama ilivyo kawaida, na bodi ya kampuni. Andrew Chenge, akiwa Attorney General wa Tanzania wakati wa kampuni kuundwa alikuwa Member wa Bodi. Kwa usahihi kabisa akateuliwa ni mmoja wa signatories.

ULAJI ulipoamza kwa nguvu miongoni mwa watumishi wa umma, (baada ya Muasisi wa Taifa kuondoka) inaonekana Chenge aliruhusiwa "kununua" hisa ktk hii kampuni, kwa bei tusiyofahamu.

Sina hakika kama ni wakati huo alipofungua akaunti ktk Bank ya kule Jersey Islands, Uingereza, na kuanza kulundika "vijisenti" huko. Waingereza wametuarifu kwamba ktk mgao wa ile commission ya 30 percent ya ununuzi wa Radar, US$ 600,000 zilizolipwa bwana Vijisenti, ziliwekwa huko.

Waingereza wanajua. Sisi Tanzania tumearifiwa. Pia tunajua kwamba ile bei ya radar ilikuwa ya kuruka sana, kiasi cha Waziri mmoja wa Uingereza (?Judith Short) kutusemea ktk Bunge lao kwamba kampuni yao ilitudanganya. Sisi wenyewe tunatambua commission ya 30 percent ni kufuru na wizi wa hadharani. Lakini "Uchunguzi" wetu bado haujakamilika, licha ya madokezo na madondoo yote hayo.

Viongozi wazalendo jasiri, wakiongozwa na Dk. Willibrod Slaa Bungeni, wakauliza "kulikoni?". Mheshimiwa Jeremiah Sumari, Naibu Waziri wetu wa Fedha tunayemlipa mshahara, akasema maswali hayo yanahusu viongozi wa JWTZ na kwamba hayazungumzwi! Hapa akiimanisha kwamba ukiteuliwa kiongozi ktk Jeshi, basi hata aliyekuteuwa, yaani Serikali inayosimamiwa na Bunge, haiwezi kukuhoji unapokwiba fedha za umma.

Swali lilikuwa Controller and Auditor General aanze kazi mapema kukagua makampuni haya yenye hisa nyingi za Serikali ili Bunge lijue ni nini kilifanyika. Ni jukumu lao.

Mhe. Sumari sio tu alijibu utumbo, bali alimalizia kumwambia Mhe. Slaa abuni hoja nyingine kuleta Bungeni!

Siku iliyofuata, Mhe. Zitto Kabwe akielezea masikitiko yake kuhusu majibu ya Mhe. Sumari, ambayo kwa kila muelewa aliyeyasikia aliona ni ya "hovyo hovyo" akaamuriwa na kiongozi wa Bunge eti ayafute maneno hayo. Sasa tujiulize "Je Tutafika?"

Mimi naona Bunge hili la sasa likiwa na majority ya wana-CCM, limefikia kikomo ktk kupuuza maslahi halisi ya WaTz. Na Serikali yenyewe inaonekana kuwa ni jumuiya ya watu wasioelewa au wasiojali maovu yanayofanyiwa nchi yao, yanayosababisha kutokufikia malengo ya kujikwamua ktk ujinga, umaskini na maradhi yanayotuangamiza.


Hakika kwa bunge la majority ya wana CCM hakuna uzingatiaji wa maslahi ya nchi. Hayo yanaongelewa hadharani tena LIVE kila mTZ anasikia, watu wanapuuzwa na kuambiwa wafute hoja, wabunge wamenyamaza tuu, Je inakuwaje kwenye vikao vya ndani vya wabunge wa CCM?

Nadhani huwa wanashaauriana "Msiwastue hawa walala bongo ili tuendelee kuila nchi"

Haiingii akili kuona kuwa nchi yenye utajiri wa rasilimali kila pemebe iko taabani kwa umaskini kiasi kwamba wananchi wake wanashindwa kumudu hata mlo mmoja.

Hatujawahi kutawaliwa na chama kingine zaidi ya CCM, kwa maana hiyo basi umaskini huu umeletwa na CCM. Ili kuuondoa umaskini ni lazima kwanza kwenda kwenye source na kuiondoa. Na source yenyewe ni CCM

Ondoa CCM ondoa Umaskini
progress.gif
 
JWTZ lenyewe linaendeshwa kisiasa, Hata siku moja usitegemee kwamba watasema chochote. Unadhani wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ni wanajeshi wastaafu wanateuliwa kwa bahati mbaya???

JWTZ na CCM ni mtu na Mjomba wake tusitegeme Tamko lolote.
 
Hii ya kusema miradi hii ina uhusiano na usalama wa Nchi naona ni kutishana ,ukiangalia miradi yote ya serikali inaweza kuhatarisha usalama wa Nchi au inahusika moja kwa moja na usalama wa Nchi.
Au tuseme wanamaanisha bajeti ya vyombo vya ulinzi haimo katika na haijadiliwi katika Vikao vya Bajeti ya Nchi , kwa kuwa vyombo hivyo vina vitega uchumi vyao na mapato na matumizi yanayopatikana huko yanakuwa ni siri kwa walioko au waliomo humo. Hapa panakuja hoja ya mishahara na mafao ya wanaohusika na mapato ya huko ,viwango vya mishahara ya vyombo hivyo havihusiani na viwango vya mishahara ya wafanyakazi wa serikali ,kwa maana hiyo panapojadiliwa viwango vya mishahara pale bungeni vyombo vya ulinzi na usalama vinakuwa havimo ,na ndipo kunakopelekea wafanyakazi wa vyombo hivi kulipana kwa upendeleo na wachini kabisa anakuwa kama mtumwa na hana mtetezi na inaonekana pale wanapopelekwa mstari wa mbele na wengine kufariki na wengine kurudi vilema huwa inakuwa mbinde kulipwa na na mara nyingi huwa hawalipwi kabisa ,nakumbuka nilihangaishwa sana kudai malipo niliporejea kutoka kwenye mapambano ya kumng'oa nduli na sikulipwa ,wisho wake niliambiwa niende kwa Nyerere kwenda kudai kwa kuwa yeye ndie aliesema vijana wajitokeze kulinda Nchi yao sio kitengo cha Jeshi. Sikupata kitu.
Labda kama mpo mnaofahamu bajeti ya matumizi ya vyombo vya ulinzi kama huwa inajadiliwa bungeni na kujaziwa fedha kutoka serikalini, mtueleze.
 
logo_new.jpg

RANDGOLD RESOURCES IN JV WITH TANZANIAN GOVERNMENT

24 August 2005
2005-08-23

Dar es Salaam, 24 August 2005 (LSE:RRS)(Nasdaq:GOLD) - London and Nasdaq listed gold miner Randgold Resources announced today that it had signed a joint-venture agreement with the government of Tanzania to develop new mineral deposits in that country.
Known as the Tangold agreement, it relates to a specific area of interest, the Kiabakari Maji-Moto region, which covers 2 692 km2 around the Buhemba mine but not the mine itself. Included in the agreement are the Buhemba South prospecting licence and the Kiabakari prospecting licence, which incorporates the old Kiabakari mine. The Kiabakari deposit was discovered in 1893 and when closed in 1966 was the third-largest gold mine in Tanzania.
In terms of the Tangold agreement, Randgold Resources will fund all exploration and feasibility study costs related to the joint venture. The government retains a free and carried stake of 10% in the area of interest and in any special purpose company which may develop a mine there. On the completion of a Type IV feasibility study, the government will have a one-time right to buy an additional 15% participating interest in the specific discovery.
"The Tangold agreement marks a significant milestone in the evolution of our Tanzanian strategy and is in line with our overall strategy of developing gold opportunities in close partnership with the host country," Randgold Resources chief executive Dr Mark Bristow said today.
Randgold Resources is an international gold mining and exploration business focused on Africa. Its mission is to discover, develop and manage gold projects.
Wana JF, Randgold inaishia wapi na Tangold inaanzia wapi ? Waendeshaji wa Tangold wana accounts zao Visiwa vya Jersey - zinakofichwa hela zetu walizotuibia. Sasa Serikali imepiga marufuku kuzungumzia Meremeta , Deep Green na Tangold. Hebu tujikumbushe kidogo yaliyotokea 2007:-

Energy and Minerals minister Nazir Karamagi told the House yesterday that Meremeta was set up in 1997 purposely to buy minerals from small-scale miners in the Lake Victoria zone and is jointly owned by Trinnex (pty) Ltd and the government on a 50-50 per cent shareholding.

As gold mining and trading became more competitive after the liberalisation of the mining sector, Karamagi explained, Meremeta failed to attain its target of buying 300 kg of gold monthly.

He said in 2000 it established Buhemba Gold Mine but that also failed to meet its commercial targets because of financial constraints and the government was forced to intervene.

`In 2003 Meremeta stopped buying gold from small-scale miners and instead decided to establish a completely new company known as RandGold/Tangold ?, which was wholly state-owned,` noted the minister.
Kweli njia ya mwongo ni fupi - Pinda amekubali kupindishwa na pamoja na kwamba ukipanda mchele huwezi kuvuna chungwa, haya kwa hakika yanasikitisha. Nawasilisha.
 
Halafu kinachotatanisha zaidi - Randgold Resources baadaye walitoa taarifa hii:-

Our strategy in Tanzania has paid off with the awarding of the Kiabakari exploration license and the conclusion of the joint venture with Tangold. We now dominate the land position in the Musoma Greenstone Belt. Drill rigs are booked to start a preliminary reconnaissance phase of drilling at Kiabakari and continue testing conceptual models beneath complex regolith cover.
Hivi JV ilikuwa kati ya Randgold Resources na Serikali ya Tanzania au ilikuwa kati yake na Tangold - kitendawili kinakua. Lakini Kulingana na Mizengo Pinda
''The Meremeta issue involves the Tanzania People's Defence Forces (TPDF). It is an issue closely related to our own national defence and security. We must protect our country,'' he said without any further elaboration.
Kaaazi kweli kweli..........maanake na Meremeta hiyo hiyo ilikuwa JV kati ya Trinnex (Pty) Limited ya Afrika Kusini na serikali ya Tanzania !!!
 
Mjadala wa DECI utazimwa kwa maslahi ya "watawala", na mjadala wa Tangold/Meremeta, nao pia utazimwa kwa namna hiyo hiyo.

Mungu ibariki Tanzania!

2010 tutajua moja, kama tutaendelea kukuubali ufisadi (kwa staili ile ya zimwi likujualo...) ama tutataka uongozi (si utawala) mbadala.

Nani anastahili kuongoza? Mtapima wenyewe. Kama kweli demokrasia ipo nchi hii!

./Mwana wa Haki
 
Back
Top Bottom