Mere prediction about the future: Yajayo yanafurahisha, upo tayari?

1. Afrika (ukiacha nchi ya Afrika Kusini) bado mno. Kama mtu ananunua gari la 2001 leo hii 2018 halafu akiliingiza nchini analiita jipya ni tatizo.
2. Siasa za Afrika hazitaruhusu hizo teknolojia kwa hofu ya wapiga kura kukosa kazi. Mambo hayo yataishia huko huko Washington.
Mkuu unajidanganya sana.
kama mambo yangekuwa hivyo hadi leo tungekuwa tunatumia Printer za Dot matrix badala ya Laser Jet Printers, au tungekuwa tunakomaa na barua au fax.

Mkuu nani alijua miaka 15 iliyopita hapa bongo matumizi ya smart card kama ya mwendokosi itatumika kwenye usafiri wa umma?

Nani alijua BVR kwenye upigaji kura itakuja haraka hivyo? Na karibuni tu itakuwa rahisi kumtambua mhalifu kwa kutumia fingerprints maana database ndio hiyo tayari tulitoa alama zetu kwenye zoezi la vitambulisho vya Taifa na uchaguzi mkuu.

Kwa taarifa yako matumizi ya digital currency(Hiyo Block chain) nchi masikini ambazo watu hawana vitambulisho vizuri, mabenki kam westunion hakuna huko vijijini watafaidika sana na hizi Bitcoin pale watakapotumiwa pesa na ndugu zao akina Drogba toka Ulaya au Mbwana Samatta toka huko Ulaya wanakotafuta riziki. wanachohitaji ni Smartphone tu ambazo sasa ni gharama nafuu zimeenea hadi vijijini.

Unafikiri yule aliekamatwa Julius Nyerere international Airport (JNIA) na dola kadhaa cash angetumia Bitcoin au digital currency yeyote angekamatwa?
Kwa kutumia banking system iwe swift, Visa, n.k. hizo lazima utakuwa controlled tu lakini sio hizo digital currency(Block chain kama Bitcoin).

NB: Hapa sifundishi watu kukwepa mkono wa sheria au cybercrime au ukwepaji kodi au utakatishaji fedha. Natoa mifano hii kwa lengo la kuelimisha tu(For Educational Purposes).

Tafuta hii documentary mpya kabisa.
magic-money-the-bitcoin-revolution-2017-720p-cover.jpg

Magic Money: The Bitcoin Revolution (2017)
 
USISUMBUE AKILI YAKO NA MANENO YA KUAMBIWA KITU FLANI KINALIPA

MFANO

Ukipata nafasi ya kufika kule Mbozi, Mbeya ukakutana na habari za watu wanaotajirika kutokana na kilimo cha kahawa, kwa kweli unaweza kuwehuka, na kujiona kama mtu uliyechelewa kweli kweli.

Wakati unarudi, kama ukishuka Mafinga, Njombe na kufuatilia stori na kutazama na milionea walioupata umilionea kutokana na biashara ya miti na mbao, unaweza kudhani kwamba hapa duniani fursa inayowatoa watu kiuharaka ni mbao pekee!

Pitia maeneo ya Ruaha Mbuyuni, Iringa kutana na wakulima wa nyanya na vitunguu wakikuonesha coaster walizonunua kwa kilimo cha msimu mmoja pekee. Aisee kama una akiba utanunua shamba muda huo huo na kuachana na ajira kama ulikuwa mwajiriwa.

Ukitoka pale ukaenda mpaka Mang'ula na Ifakara Morogoro, ukakutana na habari za watu wanavyopiga hela kwenye mpunga, kichwa chako kinaweza kuwaka moto. Unaweza kujizaba vibao na kujimaindi, afu utajiuliza, "Nilikua wapi siku, zote hizi?"

Ukitoka kule jisogeze mdogo mdogo hadi kariakoo, Dsm kisha kutana na wafanyabiashara wa maduka pale ambao wana gepu la kufuata bidhaa kule China, Uingereza na Dubai. Utapigwa na butwaa utakapoona watu wakiongelea milioni mia tatu, milioni mia saba, bilioni mbili kama vile wanaongelea elfu kumi kumi. Usipokua na utulivu unaweza kuamini kwamba biashara zinazolipa ni maduka na unaweza kuanza kufight kupata fremu pale!

Usiende kwanza Zanzibar, bali chukua hata bus au Fastjet uende chapchap kule Arusha. Hapo kutana na stori za mabilionea wa madini wanaotikisa jiji. Ukisimuliwa ABC za madini na namna ya kucheza nayo, unaweza kuacha kila kitu na kuanza kuhangaika na biashara ya madini. Hapo sijakutajia jeuri utakayoiona kwa watu wanaofanya biashara ya utalii. Nakwambia hela ulizozisikia Kariakoo utaziona ni cha mtoto sana!

Unapoendelea kutafakari, rudi mtandaoni. Kama ukibahatika kukutana na watu wanaoitwa Network Marketing utakoma kuchagua. Wakikuelezea stori zao, wakikusimulia walivyonunua mavouge yao, wakikuonesha picha zao walizokua wanakula bata Dubai, Paris, Madagascar na Uamerikani, nakwambia korosho utaziona takataka.

Mbao utazihesabu kama biashara ya utumwa, maduka ya Kariakoo utayaona kama michosho na mipunga ya Ifakara utaiona kama madudu flani ya walugaluga waliochelewa! Sasa mara kumi hata ya Network Marketing wa bidhaa, usiombe ukutane na fursa ya digital currency, hakika nakwambia utatembea kifua mbele ukiamini kutajirika ni ishu ya kufumba na kufumbua. Na huku ndiko Ontario anapowapeleka mark my words

Hapo sijaamua kusafiri na wewe kwenda kwa wale tunaokinadi kilimo kama dhahabu inayoelea. Ukisikiliza wafuasi wa kilimo, ukasikiliza hesabu wanazokupatia unaweza kusema wanaohangaika na madini wanapoteza muda! Ngoja niuchune kukupeleka kwenye fursa ya samaki kuzitoa Mwanza kupeleka Congo, ngoja nisikurushe roho na habari ya korosho, ngoja nikaushie habari ya ufuta!

KUNA MAMBO MATANO YA KUFAHAMU:


1.Usipokua na utulivu wa fikra, hizi habari za fursa za biashara na ujasiriamali zinaweza kugeuka kuwa kama miluzi mingi, na itakupoteza.

2. Mtu yeyote asikudanganye ya kwamba kuna biashara bora kuliko nyingine. Kila biashara, fursa unayoiona huku duniani inao uwezo wa kutengeneza matajiri. Kuna matajiri kutokana na kumiliki shule, wengine kwa kumiliki mabasi, wengine kwa kuwa na vituo vya mafuta, wengine kwa kilimo, wengine kwa udalali n.k. Usisahau kuwa biashara inayomtajirisha mmoja, mwingine akiingia ndio inaweza kumfilisi na kumpoteza kabisa! Kawaulize waliolizwa kwenye kilimo, watakusimulia.

3. Mtu yeyote asikuchanganye na miluzi yake hata ukaamini kwamba kuna fursa inayoweza kumfaa kila mtu. Sio kila fursa inayompa faida John inaweza kukupa faida wewe Ashura. Ukifuatilia kwa umakini utabaini kwamba mafanikio hayakai katika uzuri wa fursa, bali yanatokana na mchukua fursa. Mwingine anaweza kujifunza na kumudu kuifanya network
marketing, lakini mwingine nature ya network marketing haimfai, isipokua akienda kule Mafinga akazamia kwenye mbao, mwaka mmoja mbali unaona ana Semitrela zake mbili na mambo yanaenda.

Kuna watu wanapotea kiuchumi kwa kung'ang'ana na fursa kwa kukariri. Kisa kuna mtu alinunua Range Rover katika network marketing na wewe unaendelea kukomaa, mwaka wa tano sasa hata bodaboda huna, kumbe ungeenda zako Mbozi kwenye Kahawa sasa hivi usikute na nyumba ungekua umejenga. Kisa wanaoenda China wanatoka na wewe unahangaika na biashara za maduka, mwaka wa ishirini bado hakujasomeka na kumbe ungeenda zako kwenye madini huko Mererani muda huu ungekua umeshanunua helkopta yako!

4. Ni kweli kwamba inatakiwa tujifunze fursa mbalimbali, lakini ifike sehemu mtu uchague kukomaa na fursa fulani pasipo kurukaruka. Utajiri hauji kwa mtu kuwa bize na kila fursa inayoingia, bali unakuja kwa kujifunza fursa nyingi na ku-stick na eneo moja, ama maeneo machache ambayo, utajitambulisha nayo na watu watakutambua. Na ukishakua katika kukomaa na maeneo yako (fursa ulizoamua kukomaa nazo), usianze tena kuyumbayumba na kutamani ya wengine.

5. Lazima ifike mahali utambue kwamba kila mtu anahitaji fedha za kutosha lakini hatuhitaji kiwango sawa cha fedha kwa sababu makusudi na malengo yetu hayafanani. Nikisema hivi, sikushauri uhangaike na fursa kwa motive ya hela pekee, bali ufanye vitu kama sehemu ya kuufurahia mchakato wa kazi, na fedha ziwe ni matokeo na sio lengo namba moja
Fursa zipo nyingi kuwa makini katika maamuzi.
nimekuheshimu ghafla....heshima kwako hii comment ni ya tarmac og .kabisa siyo kiwango chake congrat GT!!!
 
Nzuli Sana mkuu, ila ujue tu Binadamu hatuwezi kushindana na wala hatutaweza kushindana na MUNGGU milele daima, maana mawazo yake hayachunguziki.
 
Mkuu kimsingi alichofanya Ontario wala si prediction ameelezea alichosoma kwa kifupi. Na hiyo techonology inayoelezwa hapo haiwezekani Bongo kutokana na massive investment inayohitajika. Kama unataka kuona vijana wa Tanzania wanafanya nini nenda pale Buni Hub au Sahara Sparks.

Na by the way kinachohitajika si watu waliosoma IT, IT ni suala dogo sana hizo research ziko pioneered na watu waliobobea kwenye natural sciences kama quantum physics, thermal dynamics, neural sciences etc.
Ahsante Mkuu
 
Ukomo wa fikra zako ndipo wenzio wanapoendelea kufikiria na kutenda zaidi ya yale uyafikiriayo, uyaonayo na yale uliyo na uwezo nayo. Sky is the limit. If we could live long enough, most of these experiments might be fulfilled.
 
Hii mnayoita AI inatengenezwa na nani kama si binaadamu? How come robort awe na superintelligent kuliko binaadamu wakati huo hiyo superintelligent inatengenezwa na binaadamu halafu inapandikizwa ndani ya huyo robort na kuanza kufanya kazi?
Hakuna futuristic yoyote binaadamu anaweza kucreate akashindwa kuidestroy kwa maana kwamba imzidi uwezo.
 
bro utakua unakosea sanaa kusema hvyo.....ukumbuke technology ndio inatulazimisha kuishi maisha ya miguu mezan na bandle kwnye simu

mfn 1.ww mwenywe sahivi umekaa mahali umetulia umesoma huu uzi na ukatoa maoni yako,isingekua tecnlogy huo muda ungeutumia kwenda shamba au kufanya shughuli zako muhimu

2.sahvivi kuna kiyu kinatumika majumbani kinaitwa kingamuzi kumbuka madishi yetu ya analogy tulikua hatuyalipii na ukishayafunga unaenjy tuu lakini leo technology imetulazimisha kwenda digtal sio hivy tuu bali kuumia kila mwezi kwa kulipia hivyo vingamuzi na bado technology hiyo hiyo itakuja kuua uwepo wa vingamuzi kwa ujio wa SMART TV ambazo nyingi zitatumia ANDROID na IOS

3.Mifano ni mingi lakini nimetoa michache na yakawaida ili nikucritisize kwa unachokisema kwamba Bro Ontario anawapotosha vijana,UKWELI NI KWAMBA ONTARIO HAPOTOSHI VIJANA ILA VIJANA TUNAPOTOKA KWA KUTOKUFATILIA TECHNOLOGY
Inatia huruma sana kuona vijana wakigeuzwa misukule na mirija ya kunufaisha wengine..kwanini unawanyima vijana haki yao ya kutumia akili na nguvu zao za ujanani kutafuta mali na badala yake kuwaaminisha kuwa pesa zinapatikana kwa kuweka miguu mezani na bando la internet...hii ni DHAMBI KUBWA SANA!!

Kijana inabidi UTUBU..wenzetu wanahangaika kuzalisha tangible entrepreneurs wenye biashara zinazoekeweka huku vijana wamegeuzwa misukule na uyu dogo bila kujua..

Aisee TUBUNI iyo dhambi mapema..maana kuna misukule itazeeka inatafuta mali kwenye internet kuja kustuka uko 50's uwezi ata sukuma toroli. TUBUNI HII DHAMBI
 
Hii mnayoita AI inatengenezwa na nani kama si binaadamu? How come robort awe na superintelligent kuliko binaadamu wakati huo hiyo superintelligent inatengenezwa na binaadamu halafu inapandikizwa ndani ya huyo robort na kuanza kufanya kazi?
Hakuna futuristic yoyote binaadamu anaweza kucreate akashindwa kuidestroy kwa maana kwamba imzidi uwezo.
Kama hiyo teknolojia ita izidi akili ya binadamu basi, itatutawala na kutuamrisha cha kufanya.
Teknolojia ikimzidi binadamu basi itatulazimisha tuiabudu na kuitumikia.
Sisi binadamu tutakuwa watumwa wa hiyo tec.
 
Aisee sipendi matapeli!I really hate them with passion!

F**ck'em!

Ukiona mtu anaanza na mbwembwe za "nimesoma vitabu 86...."Majitu yenye grandiosity namna hii hua ni magonjwa ya schizophrenia.

Acha utapeli na ukatubu!

Matapeli ni matapeli tu. Hata yaongee buzz words namna gani!

Ontario you are a pretender.You are trying hard to sound intelligent but you have been debunked to be a fraud in and out!

Majizi bwana

Ndo watanzania tulivo ata sikushangai kwakweli....your too shallow to think deeper
 
Ni very intresting hasa kwa electeonics na macanics ila kwenye swala la Computer kizidi akiri ya binadamu hizo ni chai mkuu. Kuna kitu kinaitwa Gabage in Gabage out, computer haitaweza kifanya kaz ambayo haijaelekezwa na mwanadamu, hata maana y neno machine itakua haina maana. Huyo jamaa alilose ile game kwakuwa vilikaa vichwa vingi tuibrogram computer kuhakikisha inashinda, so yule mwanamichezo alikua anaahindana na akiri nyingi za programers lkn co kweli km computer kuzid mwanadamu. Kwa uwelewa wako mdogo kwenye technology kunakufanya uone mambo hayo ni ya ajabu sana lkn maprograma km akina Mark au Gates hata yachukulia km tunavyoyachukulia sisi. 3rd world countries tuna akiri ndogo huwez linganisha na wenzetu, ss ukisema computer imzidi mtu akiri ni mtu yupi unaemsema? Mzungu? Vyote tutumiavyo ni machinery ambazo mwanadam anatengeneza kwa akiri yake ili kumsaidia kufanya kaz
 
nimesoma yooote nimegundua hii tutawafikia cku c nyingi ngoja tumalize kwanza kuwanunua wabunge na madiwani wa ukawa. shubamiiit.
 
1. Afrika (ukiacha nchi ya Afrika Kusini) bado mno. Kama mtu ananunua gari la 2001 leo hii 2018 halafu akiliingiza nchini analiita jipya ni tatizo.
2. Siasa za Afrika hazitaruhusu hizo teknolojia kwa hofu ya wapiga kura kukosa kazi. Mambo hayo yataishia huko huko Washington.
Tena wasithubutu kutuletea upuuzi huo,wabaki huko huko na ushenzi wao
Dunia ikikaribia ukingoni teknologia itakuwa kubwa kubwa kupindukia ndipo dhiki kuu itakapokuja,,hatari sana tena sana
 
Haya vijana acheni sijui kutafuta credit sijui ukasome HKL mara sijui ualimu, dunia inazidi kutanuka.

Nendeni Veta na vyuo vya Computer Science mkachukue maujuzi ya "IT" maana ndio kozi pekee iliyobaki inayoweza kukusukuma kwa siku za mbeleni ila uwe mjanja mjanja na wa kujiongeza.

Shukrani mkuu.
Ndo kitu kimesalia,yaani nyumba inakuwa printed,Mara ehighway hapa zama za kukariri upuuz wa zamani zmekoma,,computer na sekta ya madini,michezo na burudani ndo watapeta
Eti viwanda vitaleta ajira huo upuuzi hakuna maana tena,nimejifunza kitu hapa
 
Inshort wanaprint parts za kutengeneza nyumba sio nyumba yote kwa pamoja.alafu wana assemble manually
Inawezekana bwana,ukishaset ramani,unaload materials za ujenzi unawasha kitu inasimama maisha yanaendelea,very very possible,kama tunachora mixhora kwa kufeed tools ambazo zipo then unaiprint kwenye 3D paper inatoka nini kitazuia kila tool kufeed material husika?
 
1. Afrika (ukiacha nchi ya Afrika Kusini) bado mno. Kama mtu ananunua gari la 2001 leo hii 2018 halafu akiliingiza nchini analiita jipya ni tatizo.
2. Siasa za Afrika hazitaruhusu hizo teknolojia kwa hofu ya wapiga kura kukosa kazi. Mambo hayo yataishia huko huko Washington.

Sio kweli. Angalia smartphones leo hii tunazitumia. Teknolojia haina mipaka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom