Meningitis

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
UVIMBE WA UTANDU WA UBONGO NA UTI MGONGO NI NINI?
Huu ni ugonjwa unaothiri sehemu inayofunika ubongo na uti wa mgongo, yaani utandu. Ubongo unafunikwa na sehemu au tandu tatu nyembamba za seli ili kuitengenisha na fugu la kichwa. Tand hizi zinaweza kuathirika na kusababisha hali inayojulikana kama uvimbe wa utandu wa ubongo na uti wa mgongo.
Kwa sababu tandu zilizoathirika ziko karibu na ubongo, uvimbe wa utandu wa ubongo huwa na athari kwenye ubongo na hata kazi zake kama vile kuona, kusikia, kukumbuka, uwezo wa kutembea, uwezo wa kuzungumza na uwezo wa kukumbuka.

NINI HUSABABISHA UGONJWA HUU?

Aghalabu husababishwa na bacteria, lakini pia huweza kusababishwa na viumbehai kama virusi na fungi Bakteria hii hupumuliwa ndani na hupenya kupitia damu na kuathiri ubongo na uti wa mgongo. Huambukiza haraka sana/husambaa haraka sana katika maeneo ambapo kuna msongamano mkubwa na hii inaweza kugeuka kuwa mlipuko wa magonjwa.

MLIPUKO NI NINI?

Mlipuko ni ugonjwa unaoambukiza haraka na huathiri watu wengi kwa wakati mfupi sana. Mlipuko, aghalabu hutokea katika sehemu/maeneo makubwa ambapo huishi kariby sana hususan karibu na kambi za wanajeshi, kambi za wakimbizi, katika shule za bweni na kadhalika. Milipuko ya magonjwa hutokea mara moja moja miongoni mwa jamii mbalimbali/tofauti tofauti kwa wakati tufauti tofauti kwa mwaka.

NI NANI ALIYE KATIKA HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU?

Kila mtu hupo katika hali ya hatari kuambuwa na kuugua wakati wa mlipuko/mkurupuko huu. Huambuza kirahisi na harka kutoka kwa mtu mmoja hadi mwengine.
Ilivyo kwenye magonjwa yote, ugonjwa wa utandu wa ubongo huathiri sana watoto walio chini ya miaka 5 pamoja na wakongwe. Wale walio na kinga duni k.v wale wanougua ugonjwa wa sukari, saratani, ukimwi, pia wapo katika hali ya kupata ugonjwa wa utandu wa ubongo na uti wa mgongo.

NITAJIZUIA VIPI ILI NISIPATE UGONJWA HUU?

Uzuiaji nzuri ni kupitia chanjo. Lazima watoto wote wachanjwe ili kupunguza hatari ya kuugua ugonjwa wa utandu wa ubongo.
Hata wakati wa mkurupuko wakati mwingine kuna chanjo ya kizuia mamabuzi ya ugonjwa huu.
Kwa sababu ugonjwa huu huambukiza kutoka na kukaribiana kwa watu, ni muhimu kuzingatia usafi na kuwa mbali na waathiriwa wa ugonjwa wakati wa kuwatazama, kuwajulia hali ama kuwaliwaza.
Msongamano wa watu ndicho chanzo muhimu cha kuenea na kusambaa kwa ugonjwa huu kutoka kwa mtu mmoja hadi mwengine. Katika kupunguza msongamano karibu na wewe, pia unahitajika kupunguza uwezo wa kuzuia magonjwa mengine mbali na utandu wa ubongo.

NITATAMBUAJE NINAPOUGUA UGONJWA HUU? (DALILI NA ISHARA)

Ugonjwa huu huwa na joto la hali ya juu, shida ya kuona au kuepuka mwangaza, basi ni bora uende kwenye hospitali iliyo karibu nawe haraka iwezekanavyo. Hii ni muhim sana panapokuwa na mlipuko wa utandu wa ubongo na utu wa ubongo. Hii ni kwa sababu ugonjwa huu huambuza kwa kasi sana.
Usikawie ni vema kuwa na afya badala ya kujuta.

JE KUNA TIBA YA UGONJWA HUU?

Ndiyo: huu ni ugonjwa unaosababishwa na bacteria na kuna dawa za kupambana na magonjwa yababishwayo na hewa katika hospitali zote, ambayo yanaweza kutiba ugonjwa wa utandu wa ubongo kabisa. Dawa hizi hutumiwa kupitia sindano mara nyingi kwa siku na lazima sindano hizi ziendelee kwa kipindi cha wiki/majuma mawili hadi matatu.
Iwapo kuna kukawia kufika hospitalini, dawa hiyo haiwezi kusaidia kutibu mgonjwa ambaye amezidiwa na ugonjwa huu. Haitafanya kazi kwa vyovyote vile. Kwa hivyo ni muhimu kuenda hospitalini kwa wakati unaofaa dalili zinapoonekana.

KUTAKUWA NA UBAYA GANI IWAPO SIPATI MSAADA? (MATATIZO)

Ugonjwa wa utandu wa ubongo huambukiza haraka na kwa sababu ni hatari, husabisha kifo iwapo hautibiwi. Wagonjwa wote wa utandu wa ubongo lazima walazwe hospitalini kwa sababu huzingatiwa kuwa dharura ya kimatibabu. Aghalabu, hili hujiri mgonjwa anapoenda hospitalini akichelewa ili kupata matibabu.
Madhara hufungamana na utendakazi wa ukongo na huhusisha upofu, usiwi na kutoweza kutumia mikono na miguu vizuri, kutozungumza kwa ufasaha and nafuu siyo nzuri.

NITAMTUNZA VIPI MTU AMBAYE ANAUGUA UGONJWA HUU (UTANZAJI WA NYUMBANI)?

Haushauriwi kumtunzia mgonjwa wa utandu wa ubongo nyumbani. Hii ni dharura ya kimatibabu inayostahili kutatuliwa hospitalini kati ya wiki 2-3. Iwapo unashuku kwamba Fulani wanaugua ugonjwa huu, wapeleke hospitalini haraka iwezekanavyo.
Wanapokuwa kwenya matibabu na sasa wamerudi nyumbani, husalia kuwa wanyonge. Kwa Hivyo vema kwao kutunzwa. Sharti chakula chao kiwe chepesi chenye na virutubishi wape kiasi kidogo kila baada ya saa mbili. Hii ni kwa sababu hamu yao ya chakula imerudi chini. Watie moyo wagonjwa ambao wana madhara kutokana na ugonjwa huu.

HOJA MUHIMU KUHUSU UGONJWA WA UTANDU WA UBONGO


  • Utandu ni ugonjwa wa ubongo na uti wa mgongo unaotibika. Husambaa haraka sana katika maeneo palipona msongamano na iwapo hautatibiwa.
  • Huathiri sana sana watoto an wakongwe lakini wakati wa mlipuko/mkumpuko huathiri vijana wanaume na wanawake wape watoto kinga kupitia chanjo.
  • Dalili za ugonjwa wa utandu, joto la hali ya juu, kutapika, kuumwa kichwa na kuepuka mwangaza. Kupitia kwa shingo huwa dalili ya mwisho. Watoto walio chini ya miaka 2 wanaweza kuwa na joto tu pamoja na kulia.
  • Ugonjwa wa utandu unaweza kuua kati ya saa au siku chache. Iwapo unaushuku, mkimbize mtoto au mtu mzima hospitalini kwa ajili ya kupimwa. Wanaweza kulazwa kwa ajili ya matibabu.
 
Back
Top Bottom