Mengi yaibuka kiwango cha Simba kwenye mashindano ya kombe la Mapinduzi

Anselm

JF-Expert Member
Nov 16, 2010
1,710
291
Kuendelea kucheza kwa kiwango cha chini kwenye mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayoendela Zanzibar kwa mabingwa zamani wa mashindano hayo kumeibua mambo mengi kutoka kwa baadhi ya wadau wa mchezo huo hapa nchini.

Licha ya kuchezesha kikosi cha kwanza kinachojumuisha wachezaji wao wa kimataifa team hiyo imekuwa ikishindwa kuonyesha kiwango kizuri na matokeo yake kupata ushindi kiduchu kwenye michezo yake.

Simba imeteremka mara 2 kwenye mashindano hayo na kushinda 2-1 na 1-0 dhidi ya team dhaifu za Taifa Jang'ombe na KVZ respectively, huku ushindi wa jana dhidi ya KVZ ukilalamikiwa kuwa haukuwa halali kwakuwa walifunga goli la Offside.

Mdau mmoja wa mchezo huyo ambaye amekuwa akihudhuria match zote za mashindano hayo alisikika akiuliza inakuwaje Simba inayocheza kiwango kibovu hivyo kuongoza Ligi kuu ya Bara ambayo Zanzibar nzima wanaijua kuwa ni ngumu.

Bwana Mohamed Fakhi wa Kibandamaiti naye alisikika akilalamika kutomuona mchezaji anayeongoza kwa kuzifumania nyavu kwenye ligi kuu bara, na kulaumu team hizi kubwa za Bara kwa kudharau haya mashindano na kuwaacha wachezaji mihimili Dar. Hata hivyo alipothibitishiwa kuwa mfungaji huyo muongozaji anayekwenda kwa jina la Shiza Kichuya yupo na amecheza match zote alipigwa na mshangao mkubwa kwa kutoona vitu vyake ambavyo amekuwa akivisikia anavifanya huko kwenye Ligi ya Bara.

Aidha wadau wengine walifika mbali na kuzitaka mamlaka husika kufuatilia mwenendo wa team hiyo kwenye ligi kuu ya mwaka huu Bara wakitilia mashaka matokeo ambayo wamekuwa wakiyapata ambayo kihalisia hayafanani na kiwango chao halisi cha uwanjani, "kwa namna Simba walivyopania kumaliza ukame wa kutwaa ubingwa wa Bara,huenda wakawa wanatumia mbinu mbadala za kuwawezesha kufanikisha hilo.

Haiwezekani team ikawa na kiwango duni hivyo kama inavyothibitika uwanjani hlf ikawa inaongoza Ligi" alisikika akilalamika mdau mwingine ambaye hoja yake iliungwa mkono na Mshabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina 1 la Ahmed ambaye alisema kwa kiwango hiki hata Simba ingekuwa inashiriki ligi kuu ya Zanzibar inayojulikana kuwa ni nyepesi isingeweza kuwa hata kwenye Top 3.

Naomba kuwasilisha.
 
Kuendelea kucheza kwa kiwango cha chini kwenye mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayoendela Zanzibar kwa mabingwa zamani wa mashindano hayo kumeibua mambo mengi kutoka kwa baadhi ya wadau wa mchezo huo hapa nchini.
Licha ya kuchezesha kikosi cha kwanza kinachojumuisha Wachezaji wao wa kimataifa team hiyo imekuwa ikishindwa kuonyesha kiwango kizuri na matokeo yake kupata ushindi kiduchu kwenye michezo yake.
Simba imeteremka mara 2 kwenye mashindano hayo na kushinda 2-1 na 1-0 dhidi ya team dhaifu za Taifa Jang'ombe na KVZ respectively,huku ushindi wa jana dhidi ya KVZ ukilalamikiwa kuwa haukuwa halali kwakuwa walifunga goli la Offside.
Mdau mmoja wa mchezo huyo ambaye amekuwa akihudhuria match zote za mashindano hayo alisikika akiuliza inakuwaje Simba inayocheza kiwango kibovu hivyo kuongoza Ligi kuu ya Bara ambayo Zanzibar nzima wanaijua kuwa ni ngumu.
Bwana Mohamed Fakhi wa Kibandamaiti naye alisikika akilalamika kutomuona mchezaji anayeongoza kwa kuzifumania nyavu kwenye ligi kuu bara,na kulaumu team hizi kubwa za Bara kwa kudharau haya mashindano na kuwaacha Wachezaji mihimili Dar,hata hivyo alipothibitishiwa kuwa mfungaji huyo muongozaji anayekwenda kwa jina la Shiza Kichuya yupo na amecheza match zote alipigwa na mshangao mkubwa kwa kutoona vitu vyake ambavyo amekuwa akivisikia anavifanya huko kwenye Ligi ya Bara.
Aidha wadau wengine walifika mbali na kuzitaka mamlaka husika kufatilia mwenendo wa team hiyo kwenye ligi kuu ya mwaka huu Bara wakitilia mashaka matokeo ambayo wamekuwa wakiyapata ambayo kihalisia hayafanani na kiwango chao halisi cha uwanjani, "kwa namna Simba walivyopania kumaliza ukame wa kutwaa ubingwa wa Bara,huenda wakawa wanatumia mbinu mbadala za kuwawezesha kufanikisha hilo,haiwezekani team ikawa na kiwango duni hivyo kama inavyothibitika uwanjani hlf ikawa inaongoza Ligi" alisikika akilalamika mdau mwingine ambaye hoja yake iliungwa mkono na Mshabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina 1 la Ahmed ambaye alisema kwa kiwango hiki hata Simba ingekuwa inashiriki ligi kuu ya Zanzibar inayojulikana kuwa ni nyepesi isingeweza kuwa hata kwenye Top 3.
Naomba kuwasilisha.
Mtoa mada inaonekana una ushashi ushashi, Bila Shaka utakuwa wa kike ww.
 
Halafu KVZ wamesema wao ni timu changa na kuingizwa mapinduzi cup ni kama kujenga uzoefu (mazoezi) mechi zao mapinduzi cup ni kama bonanza, simba wameshindwa kuifunga hata goal moja la halali, inamaana firimbi ingepulizwa wangetoka suluhu.
 
Kwahiyo mlitaka tuwadhalilishe wazanzibar ndiyo mjue tuna kiwango? Simba tunatatizo la ushambuliaji hilo kila mtu anafahamu.Tusitangulie kusema wakati hili ni bonanza mbona Azam nao wanshinda kiduchu,bingwa naye jana kapigwa naye anahonga.watanzania maneno tuu!
 
Soka limebaki mitandaoni tu, wakiongozwa na sembo
Na huku ...
888d0b2a8f5f2a8dc2461bff0a7f9ec5.jpg
 
Shida yetu watanzania hatupendagi kuambiwa ukweli,team inapata matokeo ndiyo lkn inacheza mpira mbovu...swali linakuja unawezaje kuvuna matokeo mazuri wkt huna kiwango kama si ujanja'ujanja sasa matokeo yake mkikutana na team isiyoingilika na refa muadirifu ndo yanatokea yale ya African Lyon na Mbeya City
 
Shida yetu watanzania hatupendagi kuambiwa ukweli,team inapata matokeo ndiyo lkn inacheza mpira mbovu...swali linakuja unawezaje kuvuna matokeo mazuri wkt huna kiwango kama si ujanja'ujanja sasa matokeo yake mkikutana na team isiyoingilika na refa muadirifu ndo yanatokea yale ya African Lyon na Mbeya City
Isiyoingilika! hahahaha
 
Halafu KVZ wamesema wao ni timu changa na kuingizwa mapinduzi cup ni kama kujenga uzoefu (mazoezi) mechi zao mapinduzi cup ni kama bonanza, simba wameshindwa kuifunga hata goal moja la halali, inamaana firimbi ingepulizwa wangetoka suluhu.
Acha kelele muhimu point tatu
 
Shida yetu watanzania hatupendagi kuambiwa ukweli,team inapata matokeo ndiyo lkn inacheza mpira mbovu...swali linakuja unawezaje kuvuna matokeo mazuri wkt huna kiwango kama si ujanja'ujanja sasa matokeo yake mkikutana na team isiyoingilika na refa muadirifu ndo yanatokea yale ya African Lyon na Mbeya City
Muhimu point tatu mdogo mdogo mtatuelewa tu
 
Kwahiyo mlitaka tuwadhalilishe wazanzibar ndiyo mjue tuna kiwango? Simba tunatatizo la ushambuliaji hilo kila mtu anafahamu.Tusitangulie kusema wakati hili ni bonanza mbona Azam nao wanshinda kiduchu,bingwa naye jana kapigwa naye anahonga.watanzania maneno tuu!
Heheheeeee! Simba ni wa kuliita kombe la Maulid bonanza? Nyinyi si ndio kombe lenu hili? Miaka kadhaa mmekuwa mnalibebea sifa Yanga ikipeleka kikosi cha pili. Sasa baada ya kuingiliwa kwenye kombe lenu mnaliita bonanza...sizitaki mbichi hizi.

Tulieni tuwabandue
 
Back
Top Bottom