Mengi: Prof. Muhongo ni muongo

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP,bwana Reginald Mengi,ameseme kauli iliyotolewa na Prof.Muhongo hivi karibuni katika kongomano linalohusu uwekezaji si ya kweli.Katika kongamano hilo,Prof.Muhongo alidai kuwa Mengi anamiliki eneo la mgodi ambalo ukubwa wake ni sawa na mara tatu ya eneo zima la mkoa wa Dar-es-salaam.

Hata hivyo,bwana Mengi amekanusha taarifa hiyo na kudai yeye anamilki eneo la takribani 1 square km tu.Mh.Mengi ametoa maelezo hayo leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Binafsi, niliona kongamano hilo ambalo hata Mengi nae alihudhuria.Katika kongamano hilo, Prof Muhongo alikuwa anajisifu,tena kwa kurudiarudia, kuwa yeye kama mwanasayansi anaongea kwa "facts na data" alafu kumbe data zenyewe ni za kupika!Katika kongamano lile Muhongo alitamka bila aibu kwa kusema "Mengi anamiliki Dar-es-salaam tatu".

Mimi naona huyu waziri si mzigo tu bali ni kizingiti cha maendeleo.

CHANZO:ITV
 
Kweli Dr Mengi anaweweseka facts and figures za last week zilikua siyo Mchezo .... I wish pangekua na video ya alichosema Prof : Muhongo hakusema kampuni ya madini mengi anayomiliki imaukubwa wa dar Es salaam Tatu Bali alisema viwanda anavyomiliki Dr Mengi in total vinaukubwa sawa na dar Es salaam Tatu .... Dr Mengi asipindishe maneno ajibu hoja aseme ukubwa wa viwanda vyake vyote anavyomiliki plus aridhi anavyomiliki wewe kwa shuguli binafsi in total ni ukubwa gani.
 
Wewe na fisadi mengi ni matapeli tu. Mhungo amewapa za uso mnaanza kuweweseka....big up sana muhongo
 
Kweli Dr Mengi anaweweseka facts and figures za last week zilikua siyo Mchezo .... I wish pangekua na video ya alichosema Prof : Muhongo hakusema kampuni ya madini mengi anayomiliki imaukubwa wa dar Es salaam Tatu Bali alisema viwanda anavyomiliki Dr Mengi in total vinaukubwa sawa na dar Es salaam Tatu .... Dr Mengi asipindishe maneno ajibu hoja aseme ukubwa wa viwanda vyake vyote anavyomiliki plus aridhi anavyomiliki wewe kwa shuguli binafsi in total ni ukubwa gani.

Acha uongo na uzushi!Alisema anamiliki vitalu vya gesi vyenye ukubwa sawa na mara tatu ya ukubwa wa mkoa wa Dar-es-salaam.

Kama kuna mtu mwingine ambae aliona kipindi kile tunaomba nae atoe maelezo bila kuchakachua ukweli.
 
mjadala umefanywa tarehe 8 unajibu tarehe 15 ulikuwa wapi kukanusha siku iliyofuata afu kama sijasahau professor hakusema mengi eneo la kitalu cha gesi kama sijasahau alisema mengi ana eneo lenye leseni ya uchimbaji wa madini na sio gesi mengi anatafuta huruma ya wananchi afu simple logic 1 sq km si ni 1000 sq metres hivi mengi na pesa alizonazo ni wakutudanganya hivyo. hayo maeneo si ndo tunayoyasikia yanauzwa kwa million 800 hadi bil 1.hata kama hatumpendi muhongo lakini kuna vitu tunapaswa ku reason with simple logic. Mengi si wakumiliki mita 1000 pekee viwanda vyake tu vinazidi sasa kwenye madini je. na ujue kadri unavyopewa eneo kubwa ndivyo probability ya kutengeneza faida inaongezeka acheni majungu hebu tuache story za vijiweni sio muda wa busara na hekima. Tuheshimu taaluma hizi siasa zimeshatugharimu vya kutosha
 
Mengi ni wa kupuuzwa tu. Alikuwepo kwenye kongamano na alitoa mada. Kwanini hakujibu pale pale anasubiri akafiche na kurekebisha data kwanza. Mfu tu huyo hana mpya
 
Tatizo la Mengi ni kutumia tuvyombo twake twa habari kutaka sympathy ya watu lakini ndiye mwongo na mbinafsi. Nani hajui, anawatumia tu the children in need kwamba ni mwungwana, no.
 
Kweli Dr Mengi anaweweseka facts and figures za last week zilikua siyo Mchezo .... I wish pangekua na video ya alichosema Prof : Muhongo hakusema kampuni ya madini mengi anayomiliki imaukubwa wa dar Es salaam Tatu Bali alisema viwanda anavyomiliki Dr Mengi in total vinaukubwa sawa na dar Es salaam Tatu .... Dr Mengi asipindishe maneno ajibu hoja aseme ukubwa wa viwanda vyake vyote anavyomiliki plus aridhi anavyomiliki wewe kwa shuguli binafsi in total ni ukubwa gani.

Wewe ulikuwa wapi siku hiyo ukasikia kuwa ni viwanda! Muongo na viwanda wapi na wapi?
 
Majina mengine ni majanga matupu. Huyu jamaa ni muongo sana kaa ilivyo jina lake, hilo naungana na Mengi.

mkuu BAK nakuheshimu sana lakini nahisi una negative attitude kwa professor kaa na ufikilie chini hii imekaa kimipasho na pengine nachelea kusema umeteleza baba angu sababu kuna tofauti kubwa kati ya muongo na muhongo. Hebu weka pembeni majina na jadili hoja za hao wote wawili professor na doctor.:smile-big:
 
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP,bwana Reginald Mengi,ameseme kauli iliyotolewa na Prof.Muhongo hivi karibuni katika kongomano linalohusu uwekezaji si ya kweli.Katika kongamano hilo,Prof.Muhongo alidai kuwa Mengi anamiliki eneo la kitalu cha gesi ambacho ukubwa wake ni sawa na mara tatu ya eneo zima la mkoa wa Dar-es-salaam.Bwana Mengi amekanusha taarifa hiyo na kudai yeye anamilki eneo la takribani 1 square km tu.Mh.Mengi ametoa maelezo hayo leo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Binafsi niliona kongamano hilo ambalo hata Mengi nae alihudhuria.Katika kongamano hilo, Prof Muhongo alikuwa anajisifu,tena kwa kurudiarudia, kuwa yeye kama mwanasayansi anaongea kwa "facts na data" alafu kumbe data zenyewe ni za kupika!Katika kongamano lile Muhongo alitamka bila aibu kwa kusema "Mengi anamiliki Dar-es-salaam tatu".

Mimi naona huyu waziri si mzigo tu bali ni kizingiti cha maendeleo.

CHANZO:ITV

Kwa nini asingemjibu kwenye mjadala? Yaani leo ndio anajibu kwenye vyombo vyake habari. Huyu mzee nae hana jipya nae ni dalali tu.
 
Mengi ni mlafi wa kupindukia,he is next to Rostam for his worthness but still exploiting his employees and not paying their salaries at regular and right time !....analilia uzawa?....nashangaa hata CCM bado hawajamfukuza uanachama coz jamaa anafitina balaa,aligombana na Adam Malima sasa kahamia kwa Professor kuna nini kwenye madini?
 
Kweli Dr Mengi anaweweseka facts and figures za last week zilikua siyo Mchezo .... I wish pangekua na video ya alichosema Prof : Muhongo hakusema kampuni ya madini mengi anayomiliki imaukubwa wa dar Es salaam Tatu Bali alisema viwanda anavyomiliki Dr Mengi in total vinaukubwa sawa na dar Es salaam Tatu .... Dr Mengi asipindishe maneno ajibu hoja aseme ukubwa wa viwanda vyake vyote anavyomiliki plus aridhi anavyomiliki wewe kwa shuguli binafsi in total ni ukubwa gani.
Akili ndogo kazini
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom