Reginald Mengi Lawyers respond (video), goes to Court; sues Rostam Aziz

Hujui kwenye civil case mahakama haina uwezo wakumuita shahidi au kuita ushahidi wowote na mtu akikataa kuitwa hakuna adhabu yoyote huwa wanaenda kwa hiari?

RA sio shahidi kwenye hii kesi bali yeye ni mtuhumiwa
anatuhumiwa kumchafua mengi...
 
Fununu kali. RA anafanya jitihada za kum-approach kiongozi mmoja wa dini mwenye ukaribu na Mengi. Huyu kiongozi wa dini alikuwa instrumental pia kumaliza masuala ya Manji vs Mengi, na la Malima vs Mengi, kwa efforts za Manji wakati huo.

Fununu pia zinasema anayoyafanya Mengi yana deep inside knowledge, and may be baraka, ya wazito juu (I don't know who is juu than RA?)
 
Jamani, Nikifuatilia mambo haya nafikia wakati najiuliza mambo mabaya juu ya RA.
Huyu mtu ana elimu ya kiwango gani??

Hawezi pia kuwatumia waliokwenda shule kuliko yeye? Au ni jeuri ya uhusiano na wana-siasa maana naona kama hata PCCB wameingia na kupokea ushahidi kwa sherehe za kamera na microphone.
 
Tulia wewe mshauri wa mengi, NGOMA bado mbichi, usianze kutafuta wafuasi wako hapa watu tuko DEEP kufuatilia mchezo, hatulali mpaka tujue mwisho wa hili GAME, TUNATAKA MBEGU ZETU ZIRUDI tena na matunda (INTEREST).........

Ninaipokea heshima hiyo kwa fahari kubwa!!
 
Hata Mengi naye katika kesi hii ni kama anazunguka mbuyu. Kwa nini asitafute ushahidi dhidi ya tuhuma za ufisadi za RA na kufungua mashtaka ili kesi iwe kweli ya kiini - ufisadi na si hizi za kutaka kusafishwa?

hili ni jukumu la DPP siyo la Mengi.
 
Ninavyojua mtu baki anaweza kuomba kibali cha kufungua kesi ya jinai kama anaona jamhuri inadolola. Hili limefanyika? Kuomba tu kufungua mashtaka dhidi ya Rostam?

Amandla...........

hatuwezi kuiachia jamhuri idolole.. ifanye kazi yake.. vinginevyo wawafukuze kazi waendasha mashtaka wote wawaache wananchi waendeshe kesi zao wenyewe.
 
Issue iko wazi mahakama iko juu ya PCCB na inajitegemea hivyo iwe PCCB wamemaliza uchunguzi au la hiyo haiusiani na kesi iliyopelekwa mahakamani. Aliyeshitakiwa atatakiwa kujitetea na kutaja mashaidi wake hivyo yeye atakuwa na ushaidi kwani hata hivyo vitu alivyowakilisha PCCB anaweza kuleta kama ushaidi wake. Ila sasa kama alifanya usanii kama kawaida yao kwenye serious issues then ameumia labda watumie njia za panya.

Sasa nadhani hii ndo njia pekee ya kuanza kufichua maovu katika jamii.
mahakama kama zitafanya kazi zake vizuri hakutakuwa na nafasi za siasa,
Tume ya hosea ni chombo ambacho kiko chini ya mkondo mwingine wa mihimili mitatu ta utawala (BUNGE, SERIKALI, MAHAKAMA).Hivyo basi PCCB haina nguvu sana kuizidi mahakama.Rostam anaweza kudhalau PCCB,na wito wa Tume ya Mwakyembe lakini hawezi kuidharau mahakama hapo hata JK hawezi kuingilia hilo.
Hebu tungoje tuone mwisho wake vuguvugu za ukombozi labda ndo zinaanza.
 
Jamani, Nikifuatilia mambo haya nafikia wakati najiuliza mambo mabaya juu ya RA.
Huyu mtu ana elimu ya kiwango gani??

Hawezi pia kuwatumia waliokwenda shule kuliko yeye? Au ni jeuri ya uhusiano na wana-siasa maana naona kama hata PCCB wameingia na kupokea ushahidi kwa sherehe za kamera na microphone.


Hosea naye yuko kwenye payroll ya RA
 
Kwasababu yeye ndio "starring" wenu anayewaburuza, kila atakalosema vidampa kama wewe mnaitikia ameen!:cool:

Mbona hapa JF kila mtu aningia kwa hiari yake mwenyewe? Na login mwenyewe, Nachagua nisome nini nichangie nini?Siasa au Mapenzi Dini au Viloja vya wakubwa.Haya tuseme kwamba ni kweli sisi tulio wengi hapa JF,tunamfuata kasisi wetu Mzee Mwanakijiji, wewe Kasisi wako nani?Rostam Aziz??? Hiii Hiii Hiii Hii Hooo Haaa!Na Dini Yako Krishana??
 
Patakuwa patamu hapo, lets just observe for the moment!! Wish this RA guy gets the full ass whooping.
 
Ingawa nilikosa mengi sana kuhusiana na ugomvi huu baina ya Mengi na Rostam, ninadhani kuwa wote wana makosa yao ingawa kwa viwango tofauti. Vile vile yule mama Simba naye kama kiongozi wa serikali alijiingiza katika malumbano yasiyomhusu.

(1) Mengi alipotoa ile orodha ya mafisadi, inawezekana kuwa alifanya makosa kutegemeana na lugha aliyotumia katika kuwataja. Kama alisema kuwa watu wale wana hatia ya ufisadi basi alikosea na ni haki ya walituhumiwa kwenda mahakamni na kumfungulia mashitaka ya kuchafuliwa majina yao. Ila kama aliwataja kwa kunukuu taarifa zilizopo na kutumia taarifa hizo kutoa hisia zake kuwa wanaweza kuwa ni mafisadi, na wala si hakuwahukumu, basi Mengi may be clean.


(2)Rostam anaweza kuwa na makosa mengi kidogo kuliko Mengi. Kosa la kwanza ni lile la kutoa hadharani taarifa za account za benki za makampuni ya Mengi (kama alifanya hivyo kweli) bila ridhaa ya mwenyewe au kibali cha mahakama. Kosa la pili ni kutoa tuhuma za madeni na kuhukumu kuwa Mengi alikataa kulipa madeni yake hayo kinyume cha ukweli pia ni makosa, hasa baada ya Mengi kuonyesha ushahidi kuwa tuhuma hizo ni za uwongo. Kosa la tatu na baya zaidi ni lile la kupeleka nyaraka hizo TAKUKURU huku akijua kuwa hata kama ni kweli Mengi alikopa na hakulipa madeni yaho, hilo siyo kosa la rushwa na haliko kwenye mamlaka ya TAKUKURU. Kosa la Mengi litakuwa ni kushindwa kutii mkataba baina yake na benki iliyokopesha; chombo pekee chenye haki ya kumshitaki Mengi hapo ni benki iliyomkopesha hela hizo wala si DPP wala TAKUKURU wala mwanasheria wa Serikali.

(3)Kwa vile ugomvi kati ya Mengi na Rostam ni baina ya watu wazima wawili wenye akili timamu, mama Simba kama kiongozi wa serikali hakuwa na sababu ya kuuingilia kabla wagonvi wenyewe hawajaomba msaada wa serikali. Na wala nafasi yake ya uongozi haimpi mamlaka ya kuingilia swala hilo.

.............karibuni mchwa na nguchiro.
 
Ingawa nilikosa mengi sana kuhusiana na ugomvi huu baina ya Mengi na Rostam, ninadhani kuwa wote wana makosa yao ingawa kwa viwango tofauti. Vile vile yule mama Simba naye kama kiongozi wa serikali alijiingiza katika malumbano yasiyomhusu.

(1) Mengi alipotoa ile orodha ya mafisadi, inawezekana kuwa alifanya makosa kutegemeana na lugha aliyotumia katika kuwataja. Kama alisema kuwa watu wale wana hatia ya ufisadi basi alikosea na ni haki ya walituhumiwa kumfungulia mashitaka ya kuchafuliwa majina yao. Ila kama aliwataja kwa kunukuu taarifa zilizopo na kutumia taarifa hizo kutoa hisia zake kuwa wanaweza kuwa ni mafisadi, na wala si hakuwahukumu, basi Mengi is clean.


(2)Rostam anaweza kuwa na makosa mengi kidogo kuliko Mengi. Kosa la kwana ni lile la kutoa hadharani taarifa za account za benki za makampuni ya Mengi (kama alifanya hivyo kweli) bila ridhaa ya mwenyewe au kibali cha mahakama kufanya hivyo linaweza kuwa ni kosa. Kosa la pili ni kutoa tuhumu za madeni na kuhukumu kuwa Mengi alikataa kulipa madeni yake hayo kinyume cha ukweli pia ni makosa, hasa baada ya Mengi kuonyesha ushahidi kuwa tuhuma hizo ni za uwongo. Kosa la tatu na baya zaidi ni lile la kupeleka nyaraka hizo TAKUKURU huku akijua kuwa hata kama ni kweli Mengi alikopa na hakulipa madeni yaho, hilo siyo kosa la rushwa na haliko kwenye mamlaka ya TAKUKURU. Chombo chenye haki ya kumshitaki Mengi ni Benki iliomkopesha Mengi wala si DPP wala TAKUKURU wala mwanasheria wa Serikali.

(3)Kwa vile ugomvi kati ya Mengi na Rostam ni baina ya watu wazima wawili wenye akili timamu, mama Simba kama kiongozi wa serikali hakuwa na sababu ya kuuingilia kabla wagonvi wenyewe hawajaomba msaada wa serikali. Na wala nafasi yake ya uongozi haimpi mamlaka ya kuingilia swala hilo.

.............karibuni mchwa na nguchiro.

mwalimu jiandae kukiri uko kwenye payroll ya nani..
 
Kichuguu,
Mkuu wangu yaani hapo umeyasema yote... Kubwa kuliko lote naloliona hapa ni Rostam kuwa na nyaraka za benki zinazohusiana na accounts ya mtu..Hapa mkuu wangu amelikoroga kichizi hasa pale alipozikabidhi PCCB ndio kabisaaa kaharibu..Huu ni ushahidi ambao Rostam hakutakiwa kabisa kuugusa kwa sababu hana Utaalam wa kukusanya ushahidi na pili haifahamiki amezipata vipi nyaraka hizo bila idhini ya mhusika au mahakama..
Yaani ni vichekesho vitupu, sijui nani kamtuma Rostam kukiwasha mahala ambapo alitakiwa kukaa kimya kabisa..Jamani kama Mkapa ambaye alikuwa rais kaitwa fisadi na magazeti yote nchini pamoja na baadhi viongozi na wananchi, imefikia hadi katupiwa mawe na kuzomewa lakini he never open his mouth.. Huyu Rostam anafikiria yeye nani au ana nguvu gani against mitungo ya FITNA ambayo tayari ilikwisha andaliwa kama chambo kwenye ndoana..Hivi kweli anafikiria Mengi ni mjinga aliyeibuka toka usingizini na kutoa maneno yale!..
 
Huyu Rostam anafikiria yeye nani au ana nguvu gani against mitungo ya FITNA ambayo tayari ilikwisha andaliwa kama chambo kwenye ndoana..Hivi kweli anafikiria Mengi ni mjinga aliyeibuka toka usingizini na kutoa maneno yale!..

.... mzee.... Nilipozungumza na Mkuchika baada ya kufungiwa MwanaHalisi alieleza sababu mojawapo ni gazeti la MwanaHalisi kutangaza taarifa za kibenki za wateja. Kwamba, ilikuwa ni makosa kwa Mwanahalisi kutangaza fulani akaunti yake ni x,y na inakiasi m,n! Labda RA hafungwi na sheria zile zile... On the other hand, Mkuchika alishajitokeza na kusema Mengi ndiye mwenye makosa.. so sitegemei akasema vinginevyo ataonekana kigeugeu..
 
Du sijui nihame kambi?Check yangu ya nyongeza Mwezi huu, kutoka kwa Reginarnd Mengi ili niendelee kumpigia Debe hapa JF imekosewa jina hii ni karibu wiki ya 2 Benki hawataki kunilipia.Nikiwapigia simu hapo Dar wananiambia wako Bussy, wakati mimi kazi yangu hapa JF inaonekana na kung'ara vizuri.Jina linasomeka Madela wa Matelu badala ya Madela wa Madilu.Vipi wenzangu wengine mlioko kwenye PayRoll Check zenu zimekosewa majina vile vile???Maana kuwamo kwenye Pay Roll ya Mengi ndo kunnifanya nitembee kifua mbele hapa Ughaibhuni.Makosa haya madogo madogo yakiendelea nitahamia kwenye Pay Roll ya Rostam Azizi, nasikia analipa vizuri kweli, kizuri zaidi ni ule mtindo wake wa kulipa Hard Cash.
 
Madela wa Madilu,
Tazama vizuri cheque yako pale kwenye jina lako wameweka initials hivyo ni lazima Benki watakupa.. Ila tu soma maelezo ya juu kabisa utaona imetoka Caspian.. Benki wameshindwa kukulipa kwa sababu wamejaribu kuwasiliana na mkulu hapatikani..
Mengi hawezi kukuandikia Cheque wewe, jina tu linaonyesha wewe ni mwenyeji wa Igunga!..... Lol
 
Madela.. yaani umenishtua mzee maana check yangu imebounce maana Mengi ameua makampuni yake mengi na sasa hana tujisenti. Ila kambi ya RA siiwezi bwana labda nijiunge na Bakhresa....
 
Back
Top Bottom