Mengi apewa tuzo ya Martin Luther King Jr.

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,461
39,928
Jana, Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP na mwanamazingira Bw. Reginald Mengi amepewa tuzo ya Martin Luther King Jr. Katika Hafla fupi iliyofanyika kwenye Ubalozi wa Marekani.

Tuzo hiyo inayotolewa kila mwaka na Ubalozi huo kwa Mtanzania ambaye ameonesha mchango mkubwa katika masuala ya haki za binadamu, mazingira, na mambo kadhaa mwaka huu nafasi hiyo imemuangukia Bw. Mengi.

Akizungumza wakati wa kumkabidhi Bw. Mengi tuzo hiyo, Balozi wa Marekani Bw. Mark Green alisema kuwa mchango wa Bw. Mengi katika eneo zima la uandishi wa habari hususan ule wa uchunguzi ni mkubwa na ambao unastahili kutambuliwa na kuthaminiwa. Bw. Green alisema kuwa utawala wa demokrasia unaenda sambamba na uhuru wa vyombo vya habari jambo ambalo Bw. Mengi amekuwa akilisimamia.

Pia mchango wa Bw. Mengi katika mazingira, kusaidia wasiojiweza na masuala mengine ulitambuliwa. Watanzania wengine ambao wamekwishapata tuzo hiyo kabla ya Bw. Mengi ni pamoja na Baba wa Taifa, mzee Kawawa, Dr. Salim, na Jaji Warioba.
 
NAdhani hiu tuzo imeenda kwa wrong person ambaye anatumia vyombo vyake vya habari kwa kujitangaza na kutafuta cheap populality,nakumbuka alivyosababisha trphon Maji afukuzwe kazi kisa ni kwa vile kampatia Dewji mdhamana wakati ule Mengi alipodai kuwa anatishiwa kuuwawa na mwishoni ata ushahidi haukupatikana.Mengi anaetoa mishahara midogo kwa wafanyakazi wake na huku akijidai kutoa misaada,imagine toka mwaka 2000 wafanyakazi wa radio one wamekuja kuongezewa mishahara mwaka jana nov.
 
SASA FISADI SI UMWAMBIE BABA awasaidie hao wafanyakazi wa IPP kwa kudeal na Mengi? Nadhani huo ungekuwa mchango wako mkubwa. Maana kama ukimwambia mzee Iam sure anaweza kuingilia kati mpaka kikaeleweka watu wakapata mishahara mizuri! Au unasemaje mheshimiwa FISADI Mdogo?
 
Kuna watu ambao hawawezi kufurahia kitu chochote... na hakuna mtu anachoweza kufanya kikawa vizuri kwa sababu wanataka mtu awe mkamilifu kabisa ndio akubalike.
 
Thank mwanakijiji...nimepata ujumbe huo ni mzito kwa wanaoelewa.

"Kuna watu ambao hawawezi kufurahia kitu chochote..na hakuna mtu anachoweza kufanya kikawa vizuri kwa sababu wanataka mtu awe mkamilifu kabisa ndio akubalike"
 
Kuna watu ambao hawawezi kufurahia kitu chochote... na hakuna mtu anachoweza kufanya kikawa vizuri kwa sababu wanataka mtu awe mkamilifu kabisa ndio akubalike.

Mzee Mwanakijiji hapa Balozi Green katupotosha kwa kutunuku mtu mwenye huba na chuki.

Hatuko tayari kuona wasifu wa mtu kama Martin Luther King Jr unachafuliwa kwa kulinganishwa na watu wa aina ya R.A.Mengi; Balozi Green ktk hili ametulazimisha sasa tuende na tumsome Dkt King na tumfahamu kwa kina zaidi.

Ktk hali ya kawaida naona kilichofanywa na Balozi Green na wenziwe ni kumdhalilisha Dkt.King machoni pa waTZ.

Ktk supremacy na mapungufu yake Mengi hapaswi hata kupewa tuzo ya Edward Moringe Sokoine.

Tutawajibu baada ya kumpambanua Mtaalam Dkt King kwanza.
 
Mzee Mwanakijiji hapa Balozi Green katupotosha kwa kutunuku mtu mwenye huba na chuki.

Hatuko tayari kuona wasifu wa mtu kama Martin Luther King Jr unachafuliwa kwa kulinganishwa na watu wa aina ya R.A.Mengi; Balozi Green ktk hili ametulazimisha sasa tuende na tumsome Dkt King na tumfahamu kwa kina zaidi.

Ktk hali ya kawaida naona kilichofanywa na Balozi Green na wenziwe ni kumdhalilisha Dkt.King machoni pa waTZ.

Ktk supremacy na mapungufu yake Mengi hapaswi hata kupewa tuzo ya Edward Moringe Sokoine.

Tutawajibu baada ya kumpambanua Mtaalam Dkt King kwanza.

U have nailed it right on the head!
 
Kuna watu ambao hawawezi kufurahia kitu chochote... na hakuna mtu anachoweza kufanya kikawa vizuri kwa sababu wanataka mtu awe mkamilifu kabisa ndio akubalike.
Mwanakijiji,awali ya yote nikupongeze kwa ujasiri wa kuamua kutumia Rangi ya chama chetu sisi ccm.

Pia nakupongeza kwa kutoa kauli nzuri na nzito na kwa hilo naamini mapinduzi ya kifikra yanayo endeshwa na ccm yanafanikiwa kumbe si muda mrefu WEMA WETU CCM MTAUKUBALI.

MCHANGO KTK HILI.
Mengi hastahili kupata kupata tuzo hii HIstoria inamuadhibu kwani UFISADI alofanya ktk Bank ya NBC kabla ya Ubinafsishaji hautasahaulika jambo ambalo waandishi wengi naamini wanalifahamu na hawawezi kuandika bcs amefanikiwa kuwanunua.

Mengi anafahamika kwa Wizi,uzinifu,uongo hana uadilifu i belive wamarekani they DID on Purpose bcs Dkt Martin Ni Black kumpa mengi Tuzo hiyo ni kutukana Jitihada za Dk its better angepewa mtu kama KEJO,even TINDU lisu mengi Mosha jana Fisadi Mwenzie anamsifia kua ni Mtu Muadilifu inashangaza sana.

Anasifiwa kua Kuna Investigative Journalism ktk lipi,kwa Gazeti lipi la Mengi,it has come to the point kua wanTanzania Tutangaze kua Mengi hakustahili kupata Tuzo Hii even kwa Reason ya UADILIFU,nani anasahau Ugomvi wa MAMA REGINA na RITA mengi akaruka ukuta Upanga,Nani Hajui Ugomvi ulotokea ktk Msiba WA MAREHEMU MOTIE.

Jana niliona another Movie alofanya Balozi wa Marekeni alipowapongeza AMITABACHAN i mean KUBENEA, na Mzee TEGAMBWAGE, niliona opportunist wa JUKWA LA MA EDITOR kina SAKINA DATTOO na wengine,NAJIULIZA Tuzo hii ni kwa sababu hua anaanda chakula na walemavu?is that all?

Kuna watu wanamengi wamefanya hatuna swali juu ya uadilifu wao ktk nchii hii why Mengi hili ni swali ambalo tunatakiwa tujiulize kwa makini sana.

Kama tuna hitaji sana apate tuzo ingekua Vema EDITORS FORUM wakaanzisha tuzo yao wampatie and NOT DK MARTINS award hana sifa kabisa.

Kwa wasiofaham THIS DAY,KULIKONI ni Project ya kupata pesa from europian union hawa wazungu wana Fund MEDIA ambazo zinafanya INVESTIGATIVE JOURNALISM sasa huyu bwana yeye na FISADI MOSHA,SIMBA wameanzisha MEDIA SOLUTION so that waandike uongo wapelekwe mahakamani then EU inatoa Fungu and then Leo watu wanapiga makofi inasikitisha sana,ok kama alisema FISADI MTOTO ktk mchango wake mmoja ambao si hapa kua THIS IS PRIMITIVE SOCIETY kwa mwendu huu wa mwanakijiji,Kubenea,na waandishi wa this Day ndo our Main source of Information tuanweza kuthibitisha alichosema Fisadi Mtoto.
 
Nilikuwa naangalia watu waliokuwapo hapo.Sikumuona Mke wa Mengi.Kulikoni?hata madame Rita(yule kimada wa mengi(ATM)) hakuwapo.ila Nampongeza kwa kupata Tuzo beside ya haya yote.Next person will be Mwanakijiji au Lissu.?
 
Watanzania wengine ambao wamekwishapata tuzo hiyo kabla ya Bw. Mengi ni pamoja na Baba wa Taifa, mzee Kawawa, Dr. Salim, na Jaji Warioba.

Nani atafuatia baada ya hao?
Naona Mengi ashachambuliwa na wachangiaji wa kwanza hapo juu
 
Nampongeza ila anapaswa kuhakikisha kuwa vyombo vyake na haswa ze comedy hawahusiki tena kuutetea ufisadi na kuwatetea mafisadi kama walivyofanya hapao awali.

Pili amwombe Dr.Slaa msamaha kwani vyombo vyake vilitumiwa na mafisadi na kumchafua haswa ze comedy nafikiri tangu wakati huo nimekuwa namtazama kwa jicho la pembeni na huwa nilimpunguzia maksi nyingi sana .
 
Watanzania,

Hivi Mengi amewakosea nini ambacho mimi sikijui?

Nimeona baadhi ya comments za watu hapa ambazo ni negative sana kuhusu Mengi.

Hakuna mwanadamu asiye na makosa lakini Mengi ni shujaa wetu Tanzania. Tunahitaji akina Mengi wengine kama 1000.

Miaka na miaka kwa mimi Mengi amekuwa my hero, labda mniambie ambacho sikijui, vinginevyo mnamwonea bure huyu mzee wetu.

Hongera sana Mengi.
 
Nimeona kiherehere kapeleka issue Bungeni na kampa pongezi leo waziri wa habari
 
Watanzania,

Hivi Mengi amewakosea nini ambacho mimi sikijui?

Nimeona baadhi ya comments za watu hapa ambazo ni negative sana kuhusu Mengi.

Hakuna mwanadamu asiye na makosa lakini Mengi ni shujaa wetu Tanzania. Tunahitaji akina Mengi wengine kama 1000.

Miaka na miaka kwa mimi Mengi amekuwa my hero, labda mniambie ambacho sikijui, vinginevyo mnamwonea bure huyu mzee wetu.

Hongera sana Mengi.
Mtanzania ya MENGI NI MENGI,na hatujamuonea ila MAREKANI wametuonea kwa kumpatia mtu kama huypo tuzo ya aina hiyo.

Halafu jana alijisahau akatamka ZAWADI badala ya TUZO then akajirekebisha inanikumbusha Kibaki alivokosea kiapo HII YOTE nia kutuonyesha kua huyu jamaa hata yy anajua kua hakustahili.
 
Mtanzania ya MENGI NI MENGI,na hatujamuonea ila MAREKANI wametuonea kwa kumpatia mtu kama huypo tuzo ya aina hiyo.

Halafu jana alijisahau akatamka ZAWADI badala ya TUZO then akajirekebisha inanikumbusha Kibaki alivokosea kiapo HII YOTE nia kutuonyesha kua huyu jamaa hata yy anajua kua hakustahili.

Mtoto wa Mkulima,

Si utuambie kwanini unaona hakustahili? Kama yeye hastahili, je ni Mtanzania gani mwingine alikuwa anastahili hiyo tuzo?

Kufanya biashara TZ ni ngumu sana, Mengi ana makosa yake lakini bado kajitahidi sana. Ukiishi na mafisadi na kulala na mafisadi, utaambukizwa tu japo harufu.

Hata sisi Watanzania wote tunaopiga kelele hapa JF hatuko clean kama ambavyo
wenzetu nchi zingine wako. Inafika mahali mambo mengine yanakuwa ni culture, inabidi tufanye mabadiliko makubwa mno kuweza kuondoa ufisadi, rushwa, unyanyasaji na mambo mengine.
 
Kuna watu ambao nadhani wanachuki za binafsi tu na ambao hawako tayari kukiri ukweli hata kama unawatumbulia macho. Ni Mtanzania gani mwingine aliyeinua wigo wa vyombo vya habari nchini? Rostam Aziz? Wengine wote wamekuja baada ya Mengi..

Hivi Mengi anaajiri watu wangapi katika vyombo vyake vya habari na makampuni yake mengine? Maana hili la "wafanyakazi wake hawalipi vizuri" naomba tuambiwe wanalipwa kiasi gani?

Hivi majuzi tangu mabadiliko ya mishahara yatangazwe nimeona wafanyakazi wa viwanda kadhaa ambao wamegoma, au wametishiwa kuachishwa kazi. Bado sijaona kutoka Bonite, IPP n.k

Je Mengi anawalipwa wafanyakazi wake below the minimum wage? Na wafanyakazi hao bado wanaendelea kufanya kazi kwake? Siku hizi kuna ushindani, kama kuna nyasi nzuri za kijani upande wa pili kwanini waendelee kufanya kazi ITV na kwingineko si wangetimka tu!?
 
Mwaka jana nilishiriki ktk msiba wa aliyekuwa PS wa Home Affairs 90s pale Sinza ,mzee Silvanus Adely.

It was shame to experience some of Mengi's past abuses, alichomfanyia yule bwana watajuana huko Ahera wakikutana.

NBC haitamsahau na ndio maana hata hayo magazeti yake hayapendi sana kulifuatilia suala la Rubambe ktk uuzwaji wa NBC akijua watamuanika na yeye kwa kuangalia ya nyuma yake.

Ni wazi pamoja na kipaji chake cha ujasiliamali tulio wengi tuna mashaka na mahusiano yake na Mzee CDM,kuna zivumazo kwa kina CDM alimfanya yeye ndiye mhazini ktk yale yale tunayoyaita leo ufisadi tangu zama za Mwalimu na Mzee Ruksa.

Niwaombe ninyi watafiti wa habari tusiishie hapa 95 kuja huku ,tuangalie 80- kuja leo nadhani tutamuona Sokoine na watesi wake , wakubwa licha ya kuwa na umri mdogo lakini tunahitaji kuiona trend inayojieleza kwa miongo halisi na si vipande.

Atueleze na yeye fedha hizi anazozigawa alizitoa wapi?

Election 1995 alikuwa nyuma ya nani? Na kwa sababu zipi?

Hatujasahau alichotaka kumfanyia Masilingi ktk awamu iliyopita,tushukuru mungu aligonga ukuta kwa Benjamin Netanyahu who was 100% not his type .

Mark Green anapaswa atuambie ktk hili ,ana lengo gani Dkt.King?
 
Hongera na Asante tumeshasikia maanake bado tu kuweka billboard! mara kipindi maalum .....mara taarifa ya habari mara bungeni.....
Alimradi kila ukipita Mwenyekiti mwenyekiti ...tuzo ...tuzo Martin Luther King..
 
kabla ya kukurupuka kupongeza au kukandia cha muhimu tungependa kujua nature ya hiyo tuzo , vigezo gani hutumika na je Mengi amekidhi vigezo. Hatuwezi kukurupuka ooh hongera au ooh analipa wafanyakazi kidogo? thats so low, njoo na data onyesha ukumbi kuwa mtu huyu kanyanyasa wafanyakazi na proof hi hapa au mtu huyu anapenda yatima na proof hii hapa. Thats JF and it will stand to be a place for hoja si udaku.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom