Meneja wa kampuni kubwa Somalia auawa na ndege zisizo na rubani za Marekani

STRUGGLE MAN

JF-Expert Member
May 31, 2018
8,638
16,566
Meneja wa kampuni kubwa Somalia auawa katika shambulio la droni la Marekani

Meneja wa shirika kubwa zaidi la mawasiliano nchini Somalia ameuawa katika shambulio la droni (ndege zisizo na rubani) za Marekani katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.

Mtandao wa habari wa Military Times umeripoti kwamba, Marekani inadai kuwa inashambulia ngome za magaidi wenye mfungamano na mtandao wa al Qaida huko Somalia, lakini sehemu kubwa ya mashambulizi ya Marekani nchini humo yanaua raia akiwemo Mohamud Haji Sirad mwenye umri wa miaka 55 ambaye alikuwa meneja wa shirika kubwa zaidi la mawasiliano nchini Somalia. Meneja huyo ameuawa baada ya droni za Marekani kumshambulia kwa makombora mawili akiwa katika shamba lake wilayani Jilib.

Komandi ya Kijeshi ya Marekani barani Afrika AFRICOM ilidai kuwa imemuua kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa genge la kigaidi la al Ashabab na mkewe lakini shirika kubwa zaidi la mawasiliano la Somalia limekanusha madai hayo na kusema kuwa, aliyeuliwa katika shambulio hilo ni meneja wa kampuni hiyo, si kiongozi wa al Shabab na mkewe.

Jana Jumamosi, kundi la kigaidi na ukufurishaji la al Shabab ambalo limetangaza utiifu wake kwa mtandao wa kigaidi wa al Qaida lilisema kwamba, Marekani imekuwa ikiua raia wa kawaida kwenye mashambulizi yake nchini Somali kwa kutumia ndege zisizo na rubani (droni), na kisha kuhalalisha mashambulizi hayo kwa kusema kuwa imelenga ngome za magaidi

Taarifa hiyo iliyosainiwa na msemaji wa al Shabaab, Ali Muhamud Rageh 'Ali Dhere' imedai kuwa, asilimia 82.7 ya mashambulizi ya droni za Marekani ndani ya miezi 34 iliyopita nchini Somalia yamelenga raia wasio na hatia

4bv786c433cda51lyy3_800C450.jpeg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa huyo mtu mkubwa ni wa kampuni gani hata umeshindwa kumtaja?Bila shaka huyo tajiri anajihusisha na Al shabaab ndio maana amefyekwa.Lingekuwa kosa kama Huyo mtu wako angeuawa kimakosa ila kwa kuwa yeye binafsi ndiye aliyelengwa basi lazima anahusisshwa na magaidi.Halafu Marekani sio wanyama kiasi hicho kwamba wao wanenda tu somalia na kuanza kuua raia wasio na hatia hiyo sio kweli.

Tusubiri ukweli halisia huu uliotuletea haujajitosheleza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa huyo mtu mkubwa ni wa kampuni gani hata umeshindwa kumtaja?Bila shaka huyo tajiri anajihusisha na Al shabaab ndio maana amefyekwa.Lingekuwa kosa kama Huyo mtu wako angeuawa kimakosa ila kwa kuwa yeye binafsi ndiye aliyelengwa basi lazima anahusisshwa na magaidi.Halafu Marekani sio wanyama kiasi hicho kwamba wao wanenda tu somalia na kuanza kuua raia wasio na hatia hiyo sio kweli.
Tusubiri ukweli halisia huu uliotuletea haujajitosheleza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Na ni kwanini wamlenge yeye na sio mwingine huko Somalia. Lazima alikuwa na dili chafu na magaidi. Unaweza kuta mawasiliano muhimu yanayopitia kwenye huo "mtandao mkubwa" alikuwa anawa-feed magaidi. In short atakuwa alikuwa mtu wao kwenye mifumo ya mawasiliano.
 
Na ni kwanini wamlenge yeye na sio mwingine huko Somalia. Lazima alikuwa na dili chafu na magaidi. Unaweza kuta mawasiliano muhimu yanayopitia kwenye huo "mtandao mkubwa" alikuwa anawa-feed magaidi. In short atakuwa alikuwa mtu wao kwenye mifumo ya mawasiliano.
Na kama angelengwa mwingine basi ungeuliza hivyo hivyo, kwanini wamlenge huyo na si mwingine!
 
Kama wao wenyewe huwa wanakiri na kuuwa raia wasiokua na hatia kwa kutumia drone ww ni kama nani unapinga kuwa hawauwi raia wasiokua na hatia? Unafkiri hio drone ikishambulia sehemu inatambua sura kwanza ndio inashambulia? Kwa taarifa yako drone nyingi za marekani zaidi zinauwa watoto na akina mama ambao hawana hatia, UKITAKA USITAKE MAREKANI NDIO MAGAIDI NAMBA 1 DUNIANI KWA KUUWA WATU NA KUSABABISHA MAKUNDI YA KIGAIDI.
Sasa huyo mtu mkubwa ni wa kampuni gani hata umeshindwa kumtaja?Bila shaka huyo tajiri anajihusisha na Al shabaab ndio maana amefyekwa.Lingekuwa kosa kama Huyo mtu wako angeuawa kimakosa ila kwa kuwa yeye binafsi ndiye aliyelengwa basi lazima anahusisshwa na magaidi.Halafu Marekani sio wanyama kiasi hicho kwamba wao wanenda tu somalia na kuanza kuua raia wasio na hatia hiyo sio kweli.
Tusubiri ukweli halisia huu uliotuletea haujajitosheleza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni nani asiejua kuhusu hilo, Marekani ni wanyama tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha upuuzi ww, Hao wamama na watoto wanauliwa kila siku na hizo drone wana dili chafu, ni kwamba hao marekani wenyewe ni magaidi kwa kuuwa watu wasiokua na hatia
... na ni kwanini wamlenge yeye na sio mwingine huko Somalia. Lazima alikuwa na dili chafu na magaidi. Unaweza kuta mawasiliano muhimu yanayopitia kwenye huo "mtandao mkubwa" alikuwa anawa-feed magaidi. In short atakuwa alikuwa mtu wao kwenye mifumo ya mawasiliano.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nothing New

Gaidi Namba Moja Ulimwenguni ni US
Wauaji Namba Moja Ulimwenguni Ni US

Bila Uwepo wa US na ISRAEL Dunia na Ulimwengu Kwaujumla Wake Pangelikua Mahala Salama Na Amani Mnoooo


Sent using Jamii Forums mobile app
Nothing New

Gaidi Namba Moja Ulimwenguni ni US
Wauaji Namba Moja Ulimwenguni Ni US

Bila Uwepo wa US na ISRAEL Dunia na Ulimwengu Kwaujumla Wake Pangelikua Mahala Salama Na Amani Mnoooo


Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kabisa mkuu
 
Naona asilimia kama sabini ya comments ni za mleta mada mwenyewe, yamkini unatumia ID tofauti basi,

Una chuki mno na Mmarekani, wewe tulia haohao unaowachukia bado unatumia teknolojia zao karibu zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mm ninachofanya ni kuwajibu kwenye hizo comments zao, mm sina chuki na marekani ila ninachoongea ni ukweli ndio maana unakuuma, natumia technology ya mchina na sio marekani, unaposemwa ukweli unakakua inakuuma??
Naona asilimia kama sabini ya comments ni za mleta mada mwenyewe, yamkini unatumia ID tofauti basi,

Una chuki mno na Mmarekani, wewe tulia haohao unaowachukia bado unatumia teknolojia zao karibu zote

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona asilimia kama sabini ya comments ni za mleta mada mwenyewe, yamkini unatumia ID tofauti basi,

Una chuki mno na Mmarekani, wewe tulia haohao unaowachukia bado unatumia teknolojia zao karibu zote

Sent using Jamii Forums mobile app
Naona asilimia kama sabini ya comments ni za mleta mada mwenyewe, yamkini unatumia ID tofauti basi,

Una chuki mno na Mmarekani, wewe tulia haohao unaowachukia bado unatumia teknolojia zao karibu zote

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata wewe pia unachukiwa na marekani
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom