Samcezar
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 13,096
- 22,621
Unajua mambo mengi ni upuuzi na kukosa shukrani.LATRA wako sahihi, asilimia 20 anayochajiwa dereva ni nyingi, angalau hiyo 15 inakua fair kiasi. Labda iwe asilimia 20 na nauli itabidi ipande zaidi.
Hao bolt na Uber ni makampuni binafsi ambayo waanzilishi wake walikuja na idea ya watu binafsi kutumia magari yao binafsi kujipatia passive income na sio kuajiri madereva tax na kuwapa mishahara. Hata ukisoma utambulisho wa wamiliki wa hizi apps utaona wanakuelezea idea yao ni very simple,haijakaa kimambi mengi. Ni simply a hobby thing na sio Career au fulltime job or occupation ingawa wewe ukitama iwe hivyo ni sawa but according to u personally sio according to them.
Haya mashirika si mashirika ya uma au ya serikali kusema hawa madereva wana haki ya kuwacontrol kwa lolote lile.
Its a free economy and tuna expect forces of Demand and Supply ndizo zitafanya kazi yake. Inasikitisha sana tena sana mamlaka ya kiserikali kama Latra kuamua kuyapangia haya mashirika ambayo kimsingi serikali nadhani walitakiwa kuyapa kila aina ya support sababu yamesaidia serikali kuwapatia raia kipato cha ziada katika uchumi huu wa ajira chache na mishahara finyu.
Hivi haya makampuni yakifunga biashara na kuondoka serikali na hawa madereva wa hizo gari watapata nini zaidi ya kurudi nyuma mara dufu maana hizo gari hazitakuwa na kazi tena kibiashara na mapato yaliyokuwa yakipatikana yatatoweka.
Kwann serikali huwa inaingilia mambo na kuyaharibu kisha wanajifanya wao ndio wanakuja kutoa msaada wakati wao ndio chanzo.
Sasa unalalamika bolt au uber kuchukua hiyo 20% hivi kubabako wewe na hiyo serikali yako ya CCM mlishawahi kuja na wazo gani ambalo linaweza kuwapatia kipato cha 80% kama hicho mnacholalamikia.
Shida hapa sio Uber na Bolt bali shida ni serikali na hawa madereva wasiojua mchawi ni nani.
Mtu anakupa deal halafu yeye katika kipato anachukua 20% anakuachia 80% then unasema anakunyonya. Aisee hivi mtu unatakiwa kuwa selfish kiasi gani. Hii 80% inatafunwa na serikali ndio maana haonekani kuwa ina faida. Hebu wazia bei za mafuta, gharama za vipuri, service za gari, vibali, tiketi za matrafiki, bima ya gari, hela ya m'miliki wa gari. Hivi vyote ndivyo vinakamua faida ya huyu dereva na si hawa makampuni.
Mbona watu ambao wanamiliki magari yao binafsi na wanafanya hizi vitu huwezi sikia wanalalamika sana sababu hawana mahesabu kama ya hawa madereva wanaopewa magari kimkataba na wamiliki.
Sasa leo watu wachache wasiokuwa na shukurani wala akili wanaona bora kampuni ifungwe kila mtu akose kulikoni wangeacha kampuni zifanye biashara kwa mujibu wa kanuni za soko huria.
Kama mtu hautaki au unaona unanyonywa simply futa tu hiyo app achana nayo weka app ya CCM wakupe abiria na wakukate hiyo 15% maana wao ndio wanajua sana biashara na si Uber na bolt.
Kila kukicha mnalalamikia uwekezaji mzuri Tanzania ambao hauwagharimu rasilimali zenu , mnaupata kama huu mnaleta ufala. Ila wakija wawekezaji wanapiga madini, mawe mafuta gesi wala hatuoni kama hapo tunanyonywa. Ila huyu ambaye anakupa mchongo kwa kutumia technology mnamuona mnyonyaji.
Aiseeeeeee hii inchi ina ufala mwingi sana. Wacha jamaa wakimbilie nchi zingine wanazojielewa. Mtu anakupa lift unampangia ruti ya kupita.