Members wa JF waliojiunga 2007 njooni tusemezane

MLAU

JF-Expert Member
Aug 23, 2007
4,726
3,354
Najua ni mwaka 11 sasa tangu tujiunge na Jamii Forum enzi hizo inaitwa Jambo forum iliyoanzishwa na vijana wawili na kubadilishwa jina baadaye na kuitwa Jamii Forum.

Najua ni mengi tumejifunza humu ndani kupitia mada mbalimbali na hata kujua kama familia.

Nadhani kwa sisi tuliojiunga 2007 ni muhimu kutoa maoni,mawazo,ushauri kwa wengine pia kuhusu namna Jamii Forum inavyosaidia jamii kwa ujumla wake hasa hasa katika kujua haki za binadamu,taarifa kuhusu mwenendo wa Taifa letu na fursa mbalimbali zinazopatika nchini na nje ya nchi.

Ni muhimu kuondokana na tabia ambayo ilianza kujitokeza ya lugha chafu na hata kuonekana kama JF ina makundi katika mada kiasi cha kuanza kuonekana ni cha chanzo cha watz kutengana kwasababu tu tofauti za kiitikadi wakati sisi wote tunalipigania Taifa letu katika ustawi wa watu wake na usawa wa haki kwa kila mmoja.

Nawatakia kila la heri members wote wa JF lakini kwa sisi wa mwaka 2007 tuwe mfano katika mijadala na mada mbalimbali kwasababu ya uzoefu wetu ndani ya Jamii Forum.

Karibuni wote tuifanye JF kuwa kimbilio lakila mmoja katika kutaka kujua mambo mengi na taarifa mbalimbali za nchi yetu na dunia kwa ujumla.
 
Hashima kwako MLAU na kwa wengine wa enzi na enzi toka miaka hiyo,
Kila nisomapo posts na comments mbali mbali za wadau enzi hizo mlikuwa mkitoa hoja zenye mashiko sana.

Bahati nzuri ya sasa hivi members wamekuwa wengi, ila bahati mbaya iliyopo kwa wingi huu wa members ni kila iletwapo thread ya maana basi asilimia kubwa ya wachangiaji ni kutema pumba na mashudu tu wachache ndio huchangia points, hakuna tena kubishana kwa hoja kama zamani.
 
nyie ndo mnadai jf imepoteza msisimko wakati enz zenu mlikuwa mnapost thread za kitoto..!
 
Umri wako sio type yetu,,, katafute vibabu/vibibi wenzako mitaani.

2007 kwanza jamiiforums ilikuwa haipo. Nenda zako jamboforums
Naona kuna watu unataka kuwatusi hapo hata waanzilishi wa huu mtandao naona huwaoi heshima yao na hilo ndiyo tatizo la kizazi cha nchi hii.
 
Hashima kwako MLAU na kwa wengine wa enzi na enzi toka miaka hiyo,
Kila nisomapo posts na comments mbali mbali za wadau enzi hizo mlikuwa mkitoa hoja zenye mashiko sana.

Bahati nzuri ya sasa hivi members wamekuwa wengi, ila bahati mbaya iliyopo kwa wingi huu wa members ni kila iletwapo thread ya maana basi asilimia kubwa ya wachangiaji ni kutema pumba na mashudu tu wachache ndio huchangia points, hakuna tena kubishana kwa hoja kama zamani.
tyc ...umeongea cha maana sana na hiyo ndiyo ilikuwa Jambo Forum 2006 na hatimaye Jamii Forum 2008 ni kweli mada zilikuwa na mashiko sana na mengi tulijifunza na hata mabishano yalikuwa hoja kwa hoja.

Kwasasa nadhani members ni wengi na wengi wanataka kusema ilimradi amesema lakini ni muhimu sana kuchangia jambo kwa hoja inasaidia sana.Kuna umuhimu wa kuwa na reference ya mambo tunayoyatoa au hata uhakika wa jambo lenyewe na sio tu kuandika kwasababu watu wanasema mtaani wakati huna uhakika na jambo lenyewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom