Membe ulisema ‘’NIGUSE NINUKE’’, Kwa sasa tunasubiri hiyo harufu uliyoahidi!

Ng'wamapalala

JF-Expert Member
Jun 9, 2011
6,808
6,500
Baada ya kuvujishwa sehemu ya maongezi ya Bernard Membe na Katibu katika kijiji Rondo kata ya Chiponda katika mkoa wa Lindi akijidai na kumwambia, ‘’tunagonja sijui watatufukuzwa, mbona hawatugusi? Wapendekeze watufukuze waone moto wake’’ na kumaliza maongezi kwa kusema ‘’tuna vita kati ya asilia na wahamiaji na huu ndio mwanzo na ajenda yenyewe’’.

Kwa sasa majibu aliyokuwa anayasubiri yamepatikana baada ya miezi ya miezi saba ambapo CCM imeamua kumfukuza uanachama wa CCM. Aliokuwa anadai ni wahamiaji wameamua kuchukua uanachama wake!

Ikumbukwe kuwa baada ya maongezi ya Membe kusikika, Mbunge wa Mtera (CCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Livingstone Lusinde alijitokeza mbele ya waandishi wa habari na kutoa maoni yake lakini pia aliomba CCM iwaite na kuwahoji wale wote waliosikika kwenye audio na alimaliza kwa kusema anamjua sana Membe na anamuweka kiporo mpaka atakaporudi kutoka China.

Baadaye Membe alijitokeza kupitia mtandao wa twitter na kumjibu Lusinde kwa maneno haya;
Membe niguse ninuke.png
Hitimisho la ujumbe wake wa twitter linalosema, ‘’NIGUSE NINUKE’’ lilitoa tafsiri kuwa kama kuna mtu/taasisi itamgusa basi ijiandae kusikia harufu yake mbaya!

Kufukuzwa kwa Membe katika CCM sio kwamba wamemgusa tu bali pia wameamua kuitoa nje ya nyumba ya CCM harufu yake.

Ieleweke kuna tofauti kati ya KUNUKA na KUNUKIA. KUNUKA ni kutoa harufu mbaya na KUNUKIA ni kutoa harufu nzuri! Kwa hiyo Membe alijua alichokuwa anamaanisha!

Kwetu sisi ambao tuko nje ya CCM, kwa sasa tunasubiri kwa hamu kusikia harufu mbaya (kunuka) ya Membe ambayo CCM wameamua kuitoa nje ya nyumba yao!

Ikumbukwe pia baada ya audio ya Makamba snr, Makamba Jnr na Nape kusikika, niliandika thread hii;

GONGA LINK>>Kwa sasa tutajua weledi na nguvu za January Makamba kwenye siasa nchini!

Haikupita muda mrefu andiko langu lilipata majibu halisi baada ya January Makamba kuomba msamaha kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, John Magufuli kwa yote aliyoyasema na kuyatenda baada ya kugundua weledi na nguvu zake za kisiasa zimebebwa na CCM!

Ikubukwe kuwa, Mwaka 2012, Nape Nnauye aliwahi kusema kwenye kipindi cha Jambo Tanzania, TBC kuwa, "Samaki ukimtoa majini hana nguvu, CCM ni taasisi na ina nguvu, ukitaka kuwa na nguvu inabidi uwe ndani ya CCM, bila CCM mwanasiasa huwezi kuwa na nguvu, tutawatoa majini hawa samaki".

Maneno ya Nape Nnauye yalililenga kundi la Edward Lowassa na timu yake (Timu Lowassa) wakati wa vurugu za kisiasa ndani ya CCM. Maneno ya Nape yalidhihirisha ukweli baada ya Lowassa na kundi lake kuondoka CCM na kujikuta hana nguvu mpaka kuamua kurudi tena CCM.

Nape pia hakuchukua muda mrefu kuyafanyia kazi maneno yake katika sakata lake akiongea na Makamba Snr, Kinana na Makamba Jr ambapo alienda Ikulu na kuomba msamaha kwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, John Magufuli kuhusiana na audio zilizovujishwa kwenye mitandao ya kijamii.

Kusikiliza Audio;
GONGA LINK>>Imevuja sauti inayodaiwa ni Maongezi ya Simu ya Nape Nnauye na Abdulrahman Kinana kuhusu njama za kuichafua CCM

GONGALINK>>Sauti inayodaiwa ni ya Mzee Makamba na Mwanaye January Makamba kuhusu Waraka

Kwa sasa ni wakati wa kumpima ‘’Samaki’’ Bernard Membe kama ana nguvu nje ya maji yanayoitwa CCM lakini kikubwa zaidi, harufu yake ni mbaya kiasi gani kama alivyodai itakayoifanya CCM inuke mpaka ikimbiwe na wapiga kura wengi mpaka ikose dola!
 
Tumpe muda anajiandaa kunuka!!, Kwan hata hao waliomfukuza hawakuchukua maamzi hayo siku hiyohiyo. Walitafakari wakaamua juzi, nafikiri anasubiri wambambikizie hizo money laundering ndio aanze kunuka.suala la yeye kufukuzwa ccm alilijua mapema na alitaafuta mlango wakutokea ili awe huru kuisema.
 
Tumpe muda anajiandaa kunuka!!, Kwan hata hao waliomfukuza hawakuchukua maamzi hayo siku hiyohiyo. Walitafakari wakaamua juzi, nafikiri anasubiri wambambikizie hizo money laundering ndio aanze kunuka.suala la yeye kufukuzwa ccm alilijua mapema na alitaafuta mlango wakutokea ili awe huru kuisema.
Ngoja tuendelee kumsubiri. Subira yavuta heri sio?
 
It's true ameguswa, na alikuwa anuke, au akinukishe, lakini tumeisha mshauri


P
 
Back
Top Bottom